CHADEMA Mwanza walaani upotoshaji unaofanywa na maadui wa chama...

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Chama cha Demokrasia na Maendeleo mkoani Mwanza kupitia Viongozi wa Chadema wilaya ya Ilemela wamesema mtu anayeitwa Robert Gwanchele aliyetoa taarifa ya kupinga maamuzi ya Kamati kuu jana siyo kiongozi ndani ya chama na kwamba amefanya hivyo kwa kutumiwa na watu ambao ni wapinzani wa Chadema.

Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Ilemela, Damas Kimenyi na Katibu Froling Rwela, wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti walisema Gwanchele siyo kiongozi ndani ya chama na hata cheo cha Mwenyekiti wa Vijana Kanda ya Ziwa Magharibu hakipo ndani ya chama.

Walisema Gwanchele alikuwa Katibu wa Chadema kata ya Nyamanolo lakini alivuliwa wadhifa huo mwaka 2011 baada ya kubainika alikuwa akitumiwa kukihujumu chama na hivyo kubakia kuwa mwanachama wa kawaida.

"Ndani ya chama Mwenyekiti wa Kanda ya Ziwa Magharibi ambaye ni Peter Mekele, Katibu ni Renatus Bujiko, kwa hiyo cheo cha Mwenyekiti wa Vijana wa Kanda ya Ziwa Magharibi hakipo katika Chadema, taarifa aliyoitoa anatumiwa na CCM," walisema.

Viongozi hao walisema kuwa Chadema wilaya ya Ilemela na mkoa wa Mwanza kwa ujumla ilishatoa taarifa ya kuunga mkono uamuzi uliotolewa na Kamati Kuu ya kuwavua nyadhifa Zitto na Dk. Mkumbo.

Zitto na Dk. Mkumbo walivuliwa nyadhifa zao wiki iliyopita kwa kile kilichodaiwa wamekisaliti chama kwa kuandaa 'Waraka wa Mabadiliko mwaka 2013' ambao ulilenga kuandaa mtandao wa ushindi kwenye uchaguzi wa ndani ya chama mwakani.

Source:Nipashe Jumatatu.


Wana JF mambo?. Muda mfupi uliopita, viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, wakishirikiana na viongozi wa chama ngazi ya Kanda ya Ziwa Magharibi na Taifa kwa ujumla, wametoa tamko kali la kukanusha taarifa zilizoitwa za 'kipuuzi na kihuni', zilizotolewa jana na Robert Gwanchele kuzuia Mbowe na Dk. Slaa wasikanyage Mwanza!.

Katika tamko hilo lenye ukurasa mmoja, limesainiwa na mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Nyamagana, Nestory Sukari pamoja na katibu wa chama wilaya hiyo, Fred Lukanga, linasema: "Waliotangaza zuio hilo, Chama hakiwatambui". Pia wamejibu maswali ya waandishi waliotaka kujua Gwanchele ni nani ndani ya Chadema, ambapo mwenyekiti wa chama Nyamagana, Sukari alisema: "Kwanza Chadema haina kitengo wala nafasi ya uongozi wa Vijana ngazi ya Kanda ya Ziwa, wala Umoja wa Matawi Mkoa wa Mwanza. Waliotoa tamko hilo ni wahuni.

Katibu wa Mbunge wa Nyamagana, Robert Mwinamila naye akaongeza kwa kusema: "Hao vijana waliotoa tamko jana yawezekana ni wagonjwa wa akili, na wanapaswa kupelekwa hospitali ya Mirembe wakapimwe akili. Unapoona mtu mwenye kichaa anaanguka anguka ovyo, anatakiwa awahishwe haraka hospitalini, maana ipo siku ataangukia moto". Ila Chadema kimeapa kuchukuwa hatua za kisheria dhidi ya Gwanchele maana amejiita ni kiongozi wa Chama wakati akijua siyo kweli na alishahamia chama cha ADC. Tamko halisi nitawaleteeni muda si mrefu waungwana!.
 
Waandishi wengi makanjanja!!!! Maana hata magazeti ya serikali pia inamaana yaliingia king?

Roma sijui ulifikiria nini. Anyways thank Molemo.
 
Last edited by a moderator:
Molemo, mbona akina kafulila na akina juliana wamlivyofukuzwa hatukusikia haya??

mmefanya hesabu zenu vizuri, miaka miwili ijayo msikimbie humu


kuna wengine wameishakaa kimya

naona unapigana kiume, mshahara wa mbowe usiende bure

mmekwisha
 
Molemo, mbona akina kafulila na akina juliana wamlivyofukuzwa hatukusikia haya??

mmefanya hesabu zenu vizuri, miaka miwili ijayo msikimbie humu


kuna wengine wameishakaa kimya

naona unapigana kiume, mshahara wa mbowe usiende bure

mmekwisha

Huna hadhi ya kujibu Posti yangu yoyote.Shame on you!
 
Molemo, mbona akina kafulila na akina juliana wamlivyofukuzwa hatukusikia haya??

mmefanya hesabu zenu vizuri, miaka miwili ijayo msikimbie humu


kuna wengine wameishakaa kimya

naona unapigana kiume, mshahara wa mbowe usiende bure

mmekwisha
Ze Mburulaz!
 
Molemo, mbona akina kafulila na akina juliana wamlivyofukuzwa hatukusikia haya??

mmefanya hesabu zenu vizuri, miaka miwili ijayo msikimbie humu


kuna wengine wameishakaa kimya

naona unapigana kiume, mshahara wa mbowe usiende bure

mmekwisha

We kweli hazikutoshi,watu wenye akili zao wapoteze muda kuwajibu wajinga wasio na kazi wanaoishi
kwa kulipwa kwa kupost JF'
 
Molemo, mbona akina kafulila na akina juliana wamlivyofukuzwa hatukusikia haya??

mmefanya hesabu zenu vizuri, miaka miwili ijayo msikimbie humu


kuna wengine wameishakaa kimya

naona unapigana kiume, mshahara wa mbowe usiende bure

mmekwisha

Lumumba fc buku 7 @work
 
Ccm kazi wanayo badala ya kuwapa watu maendeleo wnakazana na prop. afu na wapuuzi wa magazeti ya serikaili wanahangaika kupika prop utadhani media hizo ni zao kumbe zetu(umma) our days will come kila mtu atalipa kwa kiwango cha uharibifu aliosababisha
 
Countdown to 14 days....

Zitto akifukuzwa kwangu itakuwa sherehe kubwa kama ile ya wakati wanajeshi wetu wanatoka vitani Uganda huku wakiimba ule wimbo maarufu wa Idd Amin akifa mimi siwezi kulia...
 
nilijua lile tamko ni la ccm na siyo na wana chadema wanachama makini hawawezi tomko la kijinga kiasi hicho..
 
Ccm kazi wanayo badala ya kuwapa watu maendeleo wnakazana na prop. afu na wapuuzi wa magazeti ya serikaili wanahangaika kupika prop utadhani media hizo ni zao kumbe zetu(umma) our days will come kila mtu atalipa kwa kiwango cha uharibifu aliosababisha
Wanaotoa 'matamko' uenda wakawa wanapata kiasi fulani cha pesa lakini kimahesabu haiwezi kuwapeleka miaka hata mitatu mbele. Tatizo kubwa 'matamko' haya yamejaa sumu mbaya sana (udini, ukabila, ukanda, kutowajibika) ambapo matokeo yake yatatugeuka sote hata wale wanaoyatunga.
Kama kweli uvccm waliandaa mkutano wa Serena basi sio ajabu kuwa nyuma ya haya yote na wakumbuke kubeba madhara yatokanayo nayo.
 
Ccm-agamba hoi,wamebaki na propaganda za mwaka 47 ambazo haziwasaidii kwa karne hii na huku mkekani wamejaza manunda yaliyovimbiwa walichonacho ni mashuzi tu kwa mashindano,piuu,piu."watataga".
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo mkoani Mwanza kupitia Viongozi wa Chadema wilaya ya Ilemela wamesema mtu anayeitwa Robert Gwanchele aliyetoa taarifa ya kupinga maamuzi ya Kamati kuu jana siyo kiongozi ndani ya chama na kwamba amefanya hivyo kwa kutumiwa na watu ambao ni wapinzani wa Chadema.

Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Ilemela, Damas Kimenyi na Katibu Froling Rwela, wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti walisema Gwanchele siyo kiongozi ndani ya chama na hata cheo cha Mwenyekiti wa Vijana Kanda ya Ziwa Magharibu hakipo ndani ya chama.

Walisema Gwanchele alikuwa Katibu wa Chadema kata ya Nyamanolo lakini alivuliwa wadhifa huo mwaka 2011 baada ya kubainika alikuwa akitumiwa kukihujumu chama na hivyo kubakia kuwa mwanachama wa kawaida.

“Ndani ya chama Mwenyekiti wa Kanda ya Ziwa Magharibi ambaye ni Peter Mekele, Katibu ni Renatus Bujiko, kwa hiyo cheo cha Mwenyekiti wa Vijana wa Kanda ya Ziwa Magharibi hakipo katika Chadema, taarifa aliyoitoa anatumiwa na CCM,” walisema.

Viongozi hao walisema kuwa Chadema wilaya ya Ilemela na mkoa wa Mwanza kwa ujumla ilishatoa taarifa ya kuunga mkono uamuzi uliotolewa na Kamati Kuu ya kuwavua nyadhifa Zitto na Dk. Mkumbo.

Zitto na Dk. Mkumbo walivuliwa nyadhifa zao wiki iliyopita kwa kile kilichodaiwa wamekisaliti chama kwa kuandaa 'Waraka wa Mabadiliko mwaka 2013' ambao ulilenga kuandaa mtandao wa ushindi kwenye uchaguzi wa ndani ya chama mwakani.

Source:Nipashe Jumatatu.
CCM wanahangaika sana kuuchochea.Mara tamko la chuo kikuu kupinga kuvuliwa zzk.baadaye wanatokea viongozi halali kutomtambua mtoa tamko.Ni michezo ya akina Mwigulu.wana fight utafikiri wataishi milele hapa duniani.The way wanavyo hangaika utafikiri wapinzani siyo Watanzania.Kama vile mkoloni anataka kurudi.Ni umbumbumbu wa kiwango cha juu sana
 
Wananchi mwanza wanailaani chadema, halafu kanusho linatolewa na viongozi makao makuu pale ufipa, raha tupu
 
nilijua lile tamko ni la ccm na siyo na wana chadema wanachama makini hawawezi tomko la kijinga kiasi hicho..
kweli mkuu sasa hivi tunaanza tunawazoea Mara Chunya wanamuandaa mtu aonekane anatoka cdm kuhamia ccm mara wanatokea viongozi halali kukanusha kuwa huyo siyo mtu wao.Ni alimradi tu ni vituko vya ccm.Makamba yule mzee alijitahidi sana mchezo kama huo lakini wapi!wanahangaika kutetea vitumbua vyao
 
Sehemu ya tamko hilo hii hapa....

KATIKA RIPOTI YA MATAWI YA MWANZA YOTE KIPENGELE HIKI CHA HITIMISHO NI HATARI SANA NANUKUU:-


"Hitimisho: Tunataka maamuzi haya HARAMU yaliyofanywa na kamati kuu yabatilishwe na mchakato wa kuwavua viongozi hawa nyazifa zao ufuate taratibu na kanuni kwa mujibu wa katiba.


Tofauti na hapo tarehe 4/12/2013 tutaungana na wapigania Demokrasia kote nchini kufanya maandamano yasiyokuwa na ukomo mpaka uongozi uliopo utoke madarakani.
Baada ya tarehe hiyo tunataka mhakikishe mnawahamisha wabunge vibaraka wote wa chadema mkoa wa mwanza.


Mchukueni Wenje mkamtafutie jimbo Moshi na Highness Kiwia mkamtafutie jimbo HAI na MACHAME.Hii ardhi ya kanda ya ziwa sio saizi yao na tunataka waondoke mara moja. Kinyume na hapo tutawaondoa huku wakishuhudia kwa macho yao.


Pia tunamuagiza Mbowe na Slaa wasithubutu kukanyaga ardhi hii ya kanda ya ziwa ikiwa bado hawajajiuzulu ama kubadili maamuzi yao HARAMU haraka iwezekanavyo. Hatuna sababu ya kuendelea kuwa watumwa wa fikra ndani ya chama chetu."
 
Back
Top Bottom