Chadema Mwanza inahesabu siku za uhai wake trust me....

Sitegemei kutoka kwako ufinyu kama huo, huyu ni nani na alikuwa chama kipi kabla ya kurudi CCM?

8.%2BWaziri%2Bwa%2BNchi%2BOfisi%2Bya%2BRais%2B%2BStephen%2BWasira%2Bakizungumza.jpg


Wewe hujaelewa alichokiandika Kitila Mkumbo.
Kitila Mkumbo ameandika hivi "Hakuna mwanasiasa aliyekuwa upinzani akarudi ccm akaendelea kuwa mwanasiasa ! "
Sasa wewe unaweka picha ya huyo jamaa kwani alishawahi kuwa upinzani na akarudi ccm ??
Umeelewa sasa ??
 
Jamaa kaona kitu au amerubuniwa. Sidhani angekuwa "potential" angeondoka pekee yake!!!!!!!!!!!!!!.

Kwa muono wangu hana ushawishi kama wengi wanavyo exaggerate.

Alale peponi.
 
kitila atujibu kwanza kwanini ameua kijana wa watu huko iramba ndio aendelee kuchangia hapa jf,otherwise akalale kwanza
 
Unatia haibu!


tukiendeleza majina ukoo huu utapanuka sana, huko mbele utawakuta akina, Halima mdee, Zito kabwe, Prof Safari, Msigwa, Heche, Mbilnyi.

Hatimae utagundua ni kutoka pande zote za inchi, yaan chama cha watanzania wote, kunatatizo hapo mkuu? bilashaka hakuna tatizo.
 
MFADHILI MKUU WA CHADEMA SENGEREMA AHAMIA CCM
MLEZI na Mfadhili Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Sengerema, mkoani Mwanza, Bw. Alex Manji, ametangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi (CCM).
.
.
Katika mkutano huo, Bw. Manji alipewa kadi yenye namba 0136371 iliyotolewa Novemba 5,2010, na mgeni rasmi Kamanda wa Vijana wa CCM wilayani hapa, Bw. William Ngeleja, ambaye alisema uamuzi aliochukua ni wa busara na unastahili kupongezwa.
.
.
.

Mwandish wa 'makala' hii alikuwa na haraka sana ya kuandika na kuweka 'makala' hii hapa JF, kiasi kwamba amejikuta 'anajikwaa' na kuandika 'siri' ambazo hazikutakiwa kutolewa.
Kumbe Bw. Manji alishakuwa mwanachama wa CCM tangu November 5, 2010 !!
 
Mzee anapishana na upepo! Ni sawa na kuumwa njaa ya mabadiliko halafu unapishana na masinia yaliyo jaa biriani ya matumaini njiani!
 
Ngeleja yupo sengerema
mpaka sasa hajaongea na wananchi
ata tu kushuka kwenye gari upita juu
kwa juu na analala guest house.....

Na siasa jamaa hajui kwani cdm
sengerema ilishamfukuza indirect
na kutomshirikisha katika mambo
mbalimbali ya chama bwana huyo
naye akaona ni adv kutumia mwanya
huo kupotosha uma kwa kujichukulia ujiko lahasha mambo sengerema
ni safi kwa chadema na elimu ya uraia
na M4C Twanga kote kote inasonga
mbele sasa inapita vijijini na kila kata
..........

Peoplessssss powerrrrr

V
SENGEREMA
LIVE....
 
MFADHILI MKUU WA CHADEMA SENGEREMA AHAMIA CCM
MLEZI na Mfadhili Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Sengerema, mkoani Mwanza, Bw. Alex Manji, ametangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Bw. Manji ambaye hivi karibuni alitangaza kuwania ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CHADEMA, katika Uchaguzi Mkuu ujao, alifikia uamuzi huo kwenye Mkutano Mkuu wa Uchaguzi Jumuiya ya Wazazi wa CCM, wilayani hapa, uliofanyia jana.

Alisema hajashawishiwa na mtu kukihama chama hicho bali amebaini kuwa kuendelea kukaa huko ni sawa na kupoteza muda wake kwani CCM ndio chama kilichomlea tangu utoto wake.

“Nimeamua kurudi nyumbani CCM kwa hiari yangu, nitakuwa bega kwa bega na wanachama wote kuhakikisha tunaisambaratisha CHADEMA hapa Sengerema.

“Ninaijua vizuri CHADEMA kwa sababu nimekuwa mdhamini wao mkuu katika jimbo hili,’’ alisema Bw. Manji ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa chama hicho Kata ya Nyampulukano.

Katika mkutano huo, Bw. Manji alipewa kadi yenye namba 0136371 iliyotolewa Novemba 5,2010, na mgeni rasmi Kamanda wa Vijana wa CCM wilayani hapa, Bw. William Ngeleja, ambaye alisema uamuzi aliochukua ni wa busara na unastahili kupongezwa.

Akizungumzia uchaguzi huo, Mbunge wa jimbo hilo, Bw. William Ngeleja, aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi ambao watasaidia kuimarisha chama katika Uchaguzi Mkuu ujao.

“Ndugu wajumbe, naomba tuwe makini tunapochagua viongozi ambao watakuwa msingi imara wa chama chetu huko tunakokwenda ili tuendelee kuwatumikia wananchi,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM wilayani humo, Bw. Jaji Tasinga, aliwataka wajumbe wa mkutano huo wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao kwenye tume ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya.

Hapo kwenye red sijui imekaaje? kadi ya mwaka 2010?

All in all katika movement ya mabadiliko, wasaliti wote na waoga wote wanatakiwa wapukutike njiani kabla hatujafikia ile nchi ya ahadi. M4C ni mafuriko kama Hurricane Isaac, hata ufanyeje lazima miti ianguke na maji yafurike. MAKAMANDA HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE
 
Huyo Manji kapokelewa na Ngeleja,ambaye si shida kujua ni mtu wa namna gani wakati mfadhili wake ni ROSTAMU.Lazima ndege wa wanaofanana waruke pamoja na kwa hili, Manji amejipambanua na kujiona ni doa kuwapo CDM kwani mende kwake ni kwenye karo la maji taka(kinyesi cha juzi).Mtoa mada akumbuke tu kuwa aliondoka Dr. Warid ndipo CDM ikachupa zaidi.
Nampongeza Manji kwa kujiunga na chama cha mafisadi wenzake.
 
mbona kadi yake inatajwa kutolewa mwaka 2010, au alitumwa kuvuruga chama aliposhindwa kutekeleza majukumu yake akaamua kujitoa? M4C forever
 
Sababu zake sio za msingi aende tu.
..CCM iko kimaslahi Binafsi na si Raia wake
 
Uhitaji kuwa na Degree kumwelewa huyu Bw. Manji....alijitoa CCM 2010 baada ya kukosa uongozi na Kujiunga na CDM kwa gea ya ufadhili njaa...akiwa na lengo kugombea ubunge kupitia CDM 2015, amesoma upepo kuwa asingeweza kupata either kwa sababu ya sifa alizonazo azikidhi viwango,amerubuniwa na Ngeleja akijua kwakufanya hivyo atakuwa amepunguza nguvu ya CDM kitu ambacho CCM wanashindwa kuelewa ni Kwamba CDM waanzilishi walijenga Mfumo na Institution na siyo watu.... watu wataondoka CDM itabaki. Kama unaweza jidanya kuwa kwakuondoka mwanachama ambaye amekaa CDM chini ya miaka 2 basi utakuwa unajidanganya sana...ILi kudhibitisha nguvu ya CDM subiri M4C itakavyo kuja Sengerema. Unamkumbuka Gamba Shitambala?Yupo wapi?na wapi ilipo CDM?:wacko:
Chunguza utabaini
 
Huyo ameingia choo cha kike na akigundua kapotea akitaka kuingia cha kiume atakuta kina mtu na sijui ataenda wapi.
 
Back
Top Bottom