CHADEMA muacheni Lowassa apumzike, uchokonozi utawaponza

Wakuu,

Chadema kati ya mambo yanayosikitisha ni kutojifunza kupitia makosa wanayofanya. Wanapokosea zinatumika nguvu nyingi kuhalalisha makosa yao na kugeuza wakosoaji wao wenye nia njema maadui.

Mlipoingia kwenye mgogoro na Dr Slaa mwezi july 2015 mlianza kumchokonoa kwa kila namna kila mahali wakati Dr Slaa kwa heshima aliamua kukaa kimya. Baada ya miezi miwili ya propaganda ikalazimika Dr Slaa afunge mjadala kwa pigo la karne pale Serena.

Sasa mnaanza kufanya yale yale kwa Lowasa. Tunaona wanachama wenu maarufu na wabunge wanachofanya mitandaoni. Mnasahau mnadeal na mtu ambaye anakijua chama chenu kabla hata wengine hamjajua siasa ni mdudu gani.

Chadema narudia tena kuwaasa, wekeni utaratibu wa chama kutoa matamko na misimamo. Katibu mkuu Mashinji ameshaongea na kutoa msimamo tena kwa weledi mkubwa. Lakini akina Lema na wengine wameshaanza kuropoka na kukejeli kwa mtu ambaye hamjui anajua nini!

Msipojidhibiti mkaendelea na hizo kejeli mnataka kujikuta mnaingia kwenye vita na vijana wake ambao mnajua kazi yao kwenye propaganda. Mtajikuta badala ya kujenga chama kuelekea uchaguzi mkuu mnawekwa kwenye kona ya kujibu tuhuma muda wote.

Hili la EL mliingia cha kike kubalini makosa msonge mbele na msianze kazi ya kumchafua mtu ambaye mlimchafua wenyewe na kisha mkamsafisha! Hamuwezi tena kumchafua zaidi ya nyie kuabika zaidi.

Muacheni Lowasa apumzike na nyie jipangeni namna ya kukihuisha upya chama chenu ambacho kwasasa kimejaa ukakasi mbele ya wananchi ambao nyie ndio mlikuwa tumaini lao pekee.

Mkishupaza shingo muda utaongea!

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa wanateseka sana...Sema hawakutegemea kama mzee angerudi ghafla..
 
Ngoja waendelee kumchezea Lowassa halafu alipuke hasira za kimasai atoe flash yenye siri zote za chadema aduplicate flash nyingi aitishe press conference halafu amwage kwa waandishi wa Habari siri zote na awagawie Kila Mwandishi flash yake yenye siri zote za chadema ndipo vichwa vyao vitakaa sawa
Siri gani zilizoko Chadema ambazo zitakuwa hatari kwa nchi? Je, ni ugaidi?
 
Hakuna mtu anaweza kutoa siri za baraza la mawaziri hata kama ni Mbowe. Ukishakuwa waziri mkuu unabanwa na kiapo hadi kifo. Hiyo ni tofauti na Chadema, anaweza kusema lolote na si lazima aseme yeye!

Mtatafutana, hamjui kwenye siasa partners hufanya nini! Umeshaona Mbowe na Dr Slaa wakishambuliana? Mashabiki tusiojua lolote ndio wanaumizana kwa matusi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Siri gani ambazo Lowassa atakuwa nazo ambazo akina Zitto, Arfi, Dr Kaboru, Dr Slaa n.k hawakuwa nazo? Naona hoja zako zimejikita katika kutoa vitisho visivyokuwapo
 
Usipangie watu cha kuchangia, maana ametukanwa sana na wanaccm na hukuwahi kuwaonya zaidi ya kuona sawa kisa Slaa alihukumiwa nafasi. Acha unafikia maana haulipi.
Povuuu ! Hapo Mtazamo amesema ukweli ulio wazi , kuna watu wenye matusi vinywani mwao kuliko wana ufipa?
 
He anazo CD ngapi kuliko Slaa?? wewe kichwa chako kizito kutunza kumbukumbu zako mwenyewe. Tangu ahamie Chadema ulikuwa unatuaminisha hana lolote na krshazeeka na ni fisadi aliemkimbia Simba the Koroshow man, Leo karudi huko huko kwenu ghafla akawa na ujana na nguvu kiasi hicho?? Kweli sifa ya kwanza ya mashabiki mfano wako ni unafiki
unafiki[/QUOTE]
Soma hiyo!
 
Wakuu,

Chadema kati ya mambo yanayosikitisha ni kutojifunza kupitia makosa wanayofanya. Wanapokosea zinatumika nguvu nyingi kuhalalisha makosa yao na kugeuza wakosoaji wao wenye nia njema maadui.

Mlipoingia kwenye mgogoro na Dr Slaa mwezi july 2015 mlianza kumchokonoa kwa kila namna kila mahali wakati Dr Slaa kwa heshima aliamua kukaa kimya. Baada ya miezi miwili ya propaganda ikalazimika Dr Slaa afunge mjadala kwa pigo la karne pale Serena.

Sasa mnaanza kufanya yale yale kwa Lowasa. Tunaona wanachama wenu maarufu na wabunge wanachofanya mitandaoni. Mnasahau mnadeal na mtu ambaye anakijua chama chenu kabla hata wengine hamjajua siasa ni mdudu gani.

Chadema narudia tena kuwaasa, wekeni utaratibu wa chama kutoa matamko na misimamo. Katibu mkuu Mashinji ameshaongea na kutoa msimamo tena kwa weledi mkubwa. Lakini akina Lema na wengine wameshaanza kuropoka na kukejeli kwa mtu ambaye hamjui anajua nini!

Msipojidhibiti mkaendelea na hizo kejeli mnataka kujikuta mnaingia kwenye vita na vijana wake ambao mnajua kazi yao kwenye propaganda. Mtajikuta badala ya kujenga chama kuelekea uchaguzi mkuu mnawekwa kwenye kona ya kujibu tuhuma muda wote.

Hili la EL mliingia cha kike kubalini makosa msonge mbele na msianze kazi ya kumchafua mtu ambaye mlimchafua wenyewe na kisha mkamsafisha! Hamuwezi tena kumchafua zaidi ya nyie kuabika zaidi.

Muacheni Lowasa apumzike na nyie jipangeni namna ya kukihuisha upya chama chenu ambacho kwasasa kimejaa ukakasi mbele ya wananchi ambao nyie ndio mlikuwa tumaini lao pekee.

Mkishupaza shingo muda utaongea!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukweli ni kwamba hadhi kidogo aliyonayo EL ni kwa sababu ya kujiunga na Chadema. CCM ilimchafua kwa kiasi kikubwa sana hadi kuuaminisha umma kwamba wanaanzisha mahakama ya mafisadi ilikuwa ni kwa ajili yake mwenyewe. Kumbuka CCM hao hao walisema chama chao kimesafishika kwa kuondoka EL. Mtakumbuka Polepole alivyomshambulia EL kwamba ndiye alikuwa kikwazo hata cha kupatikana kwa katiba mpya. Polepole alitamka wazi kabisa kwamba amejiunga rasmi kwenye ulingo wa siasa za CCM baada ya chama hicho kuondokewa na mafisadi akina EL.

Dr. Slaa naye alisema amekimbia Chadema kwa sababu ya EL na sasa DR Slaa ni MwanaCCM na balozi wa Sweden. Sasa tunasubiri kuona kama kweli Dr. Slaa alimkimbia Lowassa tuone kama ataachia na huo ubalozi aliopewa na mwenyekiti wa CCM
 
Ushauri Mzuri Mkuu, ingawa hukuwahi kuwapa CCM wakati wanamkejeli..
Makonda, Polepole, Msukuma..nk Walivuka mipaka Walitukana kabisa..
Jiwe angepata heshima kubwa sana kama angetupilia mbali Maombi ya EL kurejea CCM ..
Chadema haijaathiriwa kuondoka kwa EL ila CCM ndiyo wanaaminisha hivyo..
Kuondoka kwa Dr. Slaa Kuliathiri CDM lakini si EL..
2020
Acha hizo maneno zako.
Wakati Dr. Slaa anaondoka mlisema sio chochote na hana athari yoyote.
Bado tunakumbuka sana.
Lowassa naye katoka bado mnarudia makosa yale yale.
Siku jamaa akimwaga mboga mtatafuta pa kujificha.
 
CCM wanazidi kuudhihirishia umma sura yao halisi. Yaani viongozi wote wa chama na serikali wanafunga ofisi zao wasiwahudumie watanzania kisa tu kwenda kumpokea Lowassa! Hivi Polepole wewe na wenzako, hamuoni aibu kwa jinsi mlivyopiga hata push up kumdhihaki Lowassa?
 
Ushauri Mzuri Mkuu, ingawa hukuwahi kuwapa CCM wakati wanamkejeli..
Makonda, Polepole, Msukuma..nk Walivuka mipaka Walitukana kabisa..
Jiwe angepata heshima kubwa sana kama angetupilia mbali Maombi ya EL kurejea CCM ..
Chadema haijaathiriwa kuondoka kwa EL ila CCM ndiyo wanaaminisha hivyo..
Kuondoka kwa Dr. Slaa Kuliathiri CDM lakini si EL..
2020
Kumkubali Mzee Lowassa kurudi CCM hiyo ndio picha kamili ya Demokrasia iliyotukuka ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Chadema imeathirika vibaya sana kuondoka kwa EL...muda utaongea katika hili.
 
CCM wanazidi kuudhihirishia umma sura yao halisi. Yaani viongozi wote wa chama na serikali wanafunga ofisi zao wasiwahudumie watanzania kisa tu kwenda kumpokea Lowassa! Hivi Polepole wewe na wenzako, hamuoni aibu kwa jinsi mlivyopiga hata push up kumdhihaki Lowassa?
Siku ile Mzee Lowassa alipotua Ufipa ilikuwaje!?
 
Siku ile Mzee Lowassa alipotua Ufipa ilikuwaje!?
Jibu swali. Mtaendelea kujenga mahakama ya mafisadi? Mlisema CCM imekuwa safi kwa Lowassa kuondoka. Leo mnatwambia nini? Mlisema Chadema imempokea fisadi. Leo mnatwambia nini?
 
Na kwasababu hakukuwa na risiti ya mauziano pia ni rahisi tu kukana, EL amejishushia heshima sana
Sijakuambia atoe siri za serikali bali siri za ccm. Ni hivi, siungi mkono Lowassa au yoyote kutukanwa, lakini usilete matisho eti ana siri za cdm. Hiyo cdm ina siri gani ambazo Lowassa au hao vijana wake wakisema nchi itayumba? Siri kubwa ambayo tunataka kuisikia ni yeye alitoa shilingi ngapi kuwahonga hao viongozi wa cdm mpaka akapewa nafasi ya kugombea urais. The rest will be repitition of cdm having a poor office, tribalism and such fuckin stories, nothing else he has in his bag.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jibu swali. Mtaendelea kujenga mahakama ya mafisadi? Mlisema CCM imekuwa safi kwa Lowassa kuondoka. Leo mnatwambia nini? Mlisema Chadema imempokea fisadi. Leo mnatwambia nini?
Unapotumia neno "Mlisema" unamaanisha nini!? Ni wapi niliposema hayo uliyoainisha hapo juu!? Hao waliosema ni kina nani?
 
Kumkubali Mzee Lowassa kurudi CCM hiyo ndio picha kamili ya Demokrasia iliyotukuka ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Chadema imeathirika vibaya sana kuondoka kwa EL...muda utaongea katika hili.
Mbona haikua Demokrasia alipohamia CDM!!
Mkuu hakuna athari yoyote, Muda utasema 😂
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom