Mzyondi
Member
- Nov 24, 2016
- 40
- 64
Chama cha mapinduzi ni chama ambacho kimefanikiwa sana kujijenga kuanzia ngazi ya mjumbe wa nyumba kumi hadi ngazi ya taifa, na kimekuwa kikiwatumia wajumbe wa nyumba kumi wakati wa uchaguzi na hata kwenye shuguli za serikali.
Sasa ili kuwanyoosha au kuwadhibiti wajumbe hao ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa CCM nawashauri viongozi wa mitaa wanotokana na CHADEMA wasiwatumie wala kuwatambua wajumbe wote wa CCM kwa kufanya hivyo watakuwa wanangoa mizizi ya CCM kuanzia chini kwa kuwa wajumbe hao hutegemea sasa shilingi elfu mbili wanazotoza kwa kila barua ya utambulisho kwenda serikali ya mtaa, Badala yake wawatumie wajumbe wanaotokana na UKAWA.
Kwa kufanya hivyo kutawezesha kukiimarisha chama kuanzia ngazi ya msingi hali itakayoisaidia CHADEMA wakati wa uchaguzi.
Mahali ambako CCM inaongoza huwatumia wajumbe wake pekee , sasa kwanini CHADEMA na UKAWA mkubali kuwatumia wajumbe wa CCM?
Sasa ili kuwanyoosha au kuwadhibiti wajumbe hao ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa CCM nawashauri viongozi wa mitaa wanotokana na CHADEMA wasiwatumie wala kuwatambua wajumbe wote wa CCM kwa kufanya hivyo watakuwa wanangoa mizizi ya CCM kuanzia chini kwa kuwa wajumbe hao hutegemea sasa shilingi elfu mbili wanazotoza kwa kila barua ya utambulisho kwenda serikali ya mtaa, Badala yake wawatumie wajumbe wanaotokana na UKAWA.
Kwa kufanya hivyo kutawezesha kukiimarisha chama kuanzia ngazi ya msingi hali itakayoisaidia CHADEMA wakati wa uchaguzi.
Mahali ambako CCM inaongoza huwatumia wajumbe wake pekee , sasa kwanini CHADEMA na UKAWA mkubali kuwatumia wajumbe wa CCM?