CHADEMA msisuse uchaguzi mkuu wa 2025 na wa Serikali za mitaa 2024

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,170
CHADEMA jipangeni kuingia uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 bila hata Katiba mpya. Ni wazi kwamba uwezekano wa kupatikana katiba mpya ni kuanzia mwaka 2026, hii ni kwa kuangalia mahesabu ya kisiasa ya chama tawala.

Hata hivyo mazingira ya kisiasa yamebadilika sana katika kipindi hiki cha miaka miwili. Jipangeni vizuri kuingia katika chaguzi zinazofuata, dalili zote zinaonyesha refa wa mchezo hatapendelea sana timu moja.

Kwa sasa pazeni sauti tu mabadiliko ya kisheria yafanyike katika tume ya uchaguzi.

Nyie ndio chama kinachotegemewa sana kutoa upinzani kwa chama tawala, mkikosekana mtawanyima raia wengi fursa ya kushiriki kuamua uongozi wa nchi yao hasa katika mhimili wa bunge.

Kuna nchi pia wapinzani waliwahi kushinda katika aina ya mazingira mliyopo nyie kwa sasa.
 
Siasa ni hesabu, kuna gain and lose, huwezi kupata vyote kwa pamoja.

Lipumba aliwqingiza king UKAWA wakatoka bungeni na kuiacha Ccm peke yake na mchakato wa katiba ukafia hapo.
 
Wananchi wanataka maendeleo katiba si kipaumbele Chao, cha muhimu mama anachapa maendeleo katiba itazibwa viraka palipotoboka.
 
Hakuna mwanasiasa wa kunipambania ama kuniwakilisha

Najipambania mwenyewe na najiwakilisha mwenyewe pia

Wao wanajali matumbo yao tu
 
Siasa ni hesabu, kuna gain and lose, huwezi kupata vyote kwa pamoja.

Lipumba aliwqingiza king UKAWA wakatoka bungeni na kuiacha Ccm peke yake na mchakato wa katiba ukafia hapo.

Mkuu get your facts right, ukawa walipotoka mchakato wa katiba mpya haukusimama, bali ulipoteza imani kwa wengi.
 
Wananchi wanataka maendeleo katiba si kipaumbele Chao, cha muhimu mama anachapa maendeleo katiba itazibwa viraka palipotoboka.

..Ccm imesha-prove failure ktk kuleta maendeleo.

..Sasa Ccm wakiendelea kung'ang'ania madarakani bila wananchi kuwa na tumaini la kuwabadilisha kuna hatari ya kutokea machafuko.
 
CHADEMA kama chama wanaweza kushiriki, lakini wananchi walio wengi hasa wapiga kura wa upande wa upinzani ni kama wamepuuza hilo zoezi liitwalo uchaguzi. Kile kitendo cha wagombea wa upinzani kupewa kura tena kwa watu kupata matatizo kisha wakaenda kuunga juhudi, sioni watu wakiendelea kujitokeza kupiga kura. Ile unaona kabisa mgombea wa upinzani kashinda kisha anatangazwa wa CCM, sioni mtu mwenye muda mchafu wa hivyo.

Bila tume huru ya uchaguzi na katiba mpya itakayorudisha imani ya wapiga kura, sioni watu wakishiriki huo uhuni. Mabadiliko ya kweli yatatokea iwapo kutakuwa na machafuko au jeshi kupindua serikali, na sisi kama nchi kuanza upya kiutawala. Hivyo tegemea wapiga kura wachache kuliko maelezo.
 
Katiba inazuia maendeleo? Kwa miaka 60 kipaumbele kimekuwa kipi?
Wananchi wanataka maendeleo katiba si kipaumbele Chao, cha muhimu mama anachapa maendeleo katiba itazibwa viraka palipotoboka.
 
CHADEMA jipangeni kuingia uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 bila hata Katiba mpya. Ni wazi kwamba uwezekano wa kupatikana katiba mpya ni kuanzia mwaka 2026, hii ni kwa kuangalia mahesabu ya kisiasa ya chama tawala.

Hata hivyo mazingira ya kisiasa yamebadilika sana katika kipindi hiki cha miaka miwili. Jipangeni vizuri kuingia katika chaguzi zinazofuata, dalili zote zinaonyesha refa wa mchezo hatapendelea sana timu moja.

Kwa sasa pazeni sauti tu mabadiliko ya kisheria yafanyike katika tume ya uchaguzi.

Nyie ndio chama kinachotegemewa sana kutoa upinzani kwa chama tawala, mkikosekana mtawanyima raia wengi fursa ya kushiriki kuamua uongozi wa nchi yao hasa katika mhimili wa bunge.

Kuna nchi pia wapinzani waliwahi kushinda katika aina ya mazingira mliyopo nyie kwa sasa.
Mkuu hiki chama kinaitwa chadema hapana kwakweli hawafai kuwa au kuitwa chama kikuu cha UPINZANI,bora kuongozwa na CCM ila watubadilishie tu Rais huyu mama hapana.
 
Unawaingiza CDM Chaka. Wagombee 2025 watampata wapi mgombea Urais? Labda wampigie magoti John Shibuda aokoe jahazi maana anaheshimika Kanda ya Ziwa.
 
Wapinzani wala hawana shida na katiba mpya wala Maendeleo..
Wapinzani wanachotaka ni kuingia madarakani. Na wanaamini katiba mpya itawapa ahueni kufikia huko...


Hiyo katiba mpya ikija na bado hawawezi kuingia madarakani watakuja na jipya au kuiponda hiyo katiba mpya..au mahakama nk..


Watu wenye akili wanadai katiba Bora bila kujali kama wapinzani watapata faida au la
 
Ngoja tuone...
.
JamiiForums-62660108.jpg
 
Back
Top Bottom