Chadema msirudi nyuma mpo kwenye njia sahihi wananchi wengi tupo pamoja nanyi

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,856
401
Kumekuwepo na porojo mbalimbali kupitia kwenye vyombo uchwara vya habari kwamba chadema imegawanyika kutokana na kitendo chake cha kususia hotuba ya jk bungeni hivi karibuni. Porojo hizo ni mbinu ya kuvuruga 'move' nzuri iliyobuniwa na kutekelezwa na chadema ili kuleta mabadiliko makubwa kwenye uwanja wa siasa hapa nchini. Ninachowaomba viongozi wa chadema msikubali na msijaribu kukata tamaa. Hatua mliyochukua bungeni imeungwa mkono sana na wazalendo wa nchi hii. Endapo mngeandaa maandamano ya kuunga mkono ususiaji wenu wa hotuba ya jk, mngeamini hiki ninachosema. Wananchi wengi mitaani wanawasifu sana kwa ushujaa wenu huo. Tafadhali endelezeni mapambano. Wanaowapinga ni vibaraka wa mafisadi wanaonufaika na mianya ya ubovu wa katiba yetu na tume ya uchaguzi. Wananchi wengi ambao ndiyo wanyonge wapo nyuma yenu.
 
Nakubaliana na mr. Gosbertgoodluck hapo juu. Hicho kilichofanywa ni ushujaa na kinapaswa kutiwa shime. MSIKATE tamaa na songa mbele. Katika kuunganisha zaidi wa tanzania UMOJA miongoni mwenu ni SILAHA na NGUZO ya mstkari wa CDM na Mageuzi ya nchi yenye manufaa. KUMBUKENI kuwaondolea kitumbua watu hawapendi, na watatumia mbinu kadhaa kuwagawanya ninyi kwa kisingizio cha DEMOKRASIA ndani ya chama ili baadae yawe ya NCCR MAGEUZI baada ya uchaguzi mkuu wa 1995. Ni hilo ndo lengo la ccm na wapambe wake. NASHAURI, kuwa na maoni tofauti kwenye msimamo fulani SIYO MBAYA, bali demokrasia ni wengi wape. IKITOKEO WAZO na MSIMAMO wako umeshindwa KUBALIANA na MAWAZO YALIYOSHINDA na KUYASIMAMIA!! HOJA YA ZITO NA WENZAKE KUWA NA MAONO TOFAUTI NA MSIMAMAMO FULANI SI KOSA, BALI NAWASHAURI KWA KUWA UAMUZI ULIKUWA NI WA WALIOWENGI KWENYE KIKAO WALIPASWA KUKUBALIANA NA KUUSIMAMIA! HAKUNA HAJA TENA YA KURUMBANA KATIKA VYOMBO VYA HABARI KUWA MIMI AU FULANI ALIONA HIVI AU VILE. HII NI KUONGEZA "GAP" AU MPASUKO MIONGONI MWENU WENYEWE NA NI HATARI KWA MSITAKABARI WA SISI TUNAOTEGEMEA MWONGOZO WENU KUTUPELEKA KWENYE TZ YANYE ASALI TUNAYOTEGEMEA KUIJENGA. "KUTENDA KOSA SI KOSA BALI KURUDIA KOSA NDO HATARI". NISHAURI KUWA NYAKATI ZA USONI KUJIEPUSHA KUTOA TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA HABARI ZINAZOKINZANA NA MTAZAMO ULIOKUBALIKA KI CHAMA. HII ITAWAONGEZEA UIMARA NA KUAMINIWA NA WANANCHI AMBAO NI SISI. HOJA YA "WALKOUT" NI JAMBO LA KAWAIDA KUONESHA MSIMAMAMO WA KILE CHAMA KINAAMINI KWA NIABA YA WANANCHI ILI MAKOSA KAMA HAYO YASITOKEE TENA. ANGALIZO: "UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU"-KISINGIZIO CHA MAONI BINAFSI KATIKA DEMOKRASIA KISIPEWE NAFASI TUKAJIMONG'ONYOA SISI WENYEWE NA KUWAFURAHISHA WABAYA/WAPINZANI WETU. TUSISAHU YALIYOWAFIKA NCCR MAGEUZI BAADA YA 1995-TUSIJE TUKALITIA MAJI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! PEOPLES!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Zitto ana kauli za utata sana sijui kwa nini, yeye sidhani kama ni msemaji wa chama, na hata kama ni msemaji wa chama hakutakiwa azungumzie vile. Anyway kwa mazingira yaliyotokea nawapongeza wabunge wa chadema ambao wameonyesha kwa vitendo kuwa hawakubaliani na matokeo ya urais kama ambavyo mimi sikubaliani na matokeo hayo.

Dawa ni kukomaa mpaka kieleweke, na kudai katiba mpya ndiyo suluhu ya haya yote, vinginevyo wataendelea kudhulumu hivihivi!


Ninaamini CHADEMA hakuna mgawanyiko, ila mafisadi wanataka kupenyeza hisia zao zipate nafasi ndani ya chadema, na hawatapata nafasi hata kidogo. CHADEMA ni chama makini ambacho hakiwezi yumbishwa na chochote.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom