Chadema msiba wa Salome hawahusu?

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
sijaona salam za rambi rambi za chama makini juu ya huu msiba kama chama, jee ndio hauwahusu? ndio mafisadi hawastahiki kupewa mkono wa pole?

...Lipumba, Makamba wamlilia

Na Mwandishi Wetu

MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, amemtumia Rais Jakaya Kikwete, salamu za rambirambi kutokana na kifo cha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bibi Salome Mbatia.

Katika salamu hizo alizozituma jana, Profesa Lipumba alisema amepokea
kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Bibi Mbatia, kilichotokea juzi kwa ajali ya gari lake kugongana na lori aina ya Mitsubishi Fuso katika wilaya ya Njombe, mkoani Iringa.

"Nilimfahamu marehemu Mbatia tangu tukiwa wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1973/76. Tangu akiwa mwanafunzi, alikuwa mchapa kazi, mwenye bidii na nia ya kijiendeleza na kushirikiana na wenzake.

"Kama kiongozi mwanamke, alikuwa mfano mzuri kwa wanawake wengine katika nchi yetu. Na kwa kweli Watanzania tulikuwa bado hatujautumia kikamilifu uwezo wa marehemu Salome Mbatia," alisema Profesa Lipumba.

Alisema Watanzania ni waumini wa dini mbali mbali na wao CUF wanaamini kifo ni jambo la lazima kwa kila binadamu.

"Lakini pia Mwenyezi Mungu ametupa uwezo wa kujiendeleza na kuepukana na ajali. Mheshimiwa Rais tumepoteza Watanzania wengi kwa ajali za magari barabarani. Pamoja na kauli za Serikali na jitihada mbali mbali ikiwa ni pamoja na kampeni maalumu, bado ajali ni nyingi mno," alisema.

Alisema ajali nyingi zinasababishwa na kutofuata sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani na kwamba kifo cha Bibi Mbatia na wenzake, hakina budi kutoa changamoto mpya ya mjadala wa kitaifa, kuhusu kuzuia ajali za magari barabarani na kuchukua hatua madhubuti ya kufanya hivyo.

"Tunawapa pole familia ya marehemu Mbatia. Tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira na uvumilivu wakati huu mgumu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amin," alisema Profesa Mbatia.

Naye Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusufu Makamba, katika salamu zake za rambirambi kwa Rais Kikwete, alisema kifo hicho kimeacha pengo kubwa kwa Serikali, CCM na jamii kwa ujumla.

"Marehemu atakumbukwa kwa ucheshi, uhodari wa kazi na upendo wake kwa watu...alikuwa amana ya Mwenyezi Mungu, kwa chama na Serikali na sasa Mungu amechukua amana yake," alisema.

Bw. Makamba aliwataka wana CCM, ndugu, jamaa na marafiki na wananchi kwa ujumla, kulitaza tukio hio kuwa ni mapenzi ya Mungu na kutambua kuwa ingawa wengi walimpenda na walikuwa bado wanamhitaji, lakini Mungu alimpenda zaidi.

Marehemu Mbatia pamoja na kuwa Mbunge wa Viti Maalumu, na Naibu Waziri, aliwahi kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM wa Uchumi na Fedha na mjumbe wa Kamati Kuu na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) tangu mwaka 2002 hadi mwaka jana.

Hadi anafariki dunia, alikuwa mjumbe wa NEC na akiwa mgombea wa NEC kundi la wanawake.

Aliwahi pia kuwa Meneja Mkuu wa kampuni ya Biashara Consumers Services Ltd kwa miaka 10, Mwenyekiti wa Bodi ya VETA kanda ya Dar es Salaam na mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).

Pia aliwahi kuwa mjumbe wa bodi za TBS, Uhuru na Mzalendo, Bahati Nasibu ya Taifa na Privatization Trust.

Wakati huo huo, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM inatarajiwa kukutana leo Dar es Salaam, kwa ajili ya kikao cha siku moja chini ya uenyekiti wa Rais Kikwete.

Kikao hicho kitajadili taarifa ya hali ya siasa nchini na mapendekezo ya wana CCM wanaoomba uongozi wa CCM mkoa wa Arusha na maendeleo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Nane wa CCM na ushiriki wa CCM katika uchaguzi mdogo wa udiwani.

http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=4313
 
Bi. Kiwelu (MB) alikuwepo nyumbani kwa marehemu na alituma salamu za rambirambi, kama hukuangalia channel 10 bahati mbaya. Hata hivyo hadi hivi sasa sijaona salamu za TEC, CCT, BAKWATA n.k hivi wote hawa msiba hauwahusu?

asante.
 
Unapofikia kufa watu wote ni sawa. Mbona huwa hamuuliza salamu za rambirambi wanapokufa raia wengine tena kwa uzembe unaosababishwa na viongozi fisadi? Au hawo roho zao ni cheap sana. Acheni unafiki nyie
 
ni swali la kitoto, halina uzuri wowote! yaani wote waliotoa rambirambi wawekewe mabango?

thanks again.
 
Taifa lamlilia Mbatia

na Happiness Katabazi na Godfrey God

VIONGOZI wakuu wa kitaifa serikalini, wanasiasa kutoka vyama mbalimbali vya siasa na wananchi wa kawaida wameshikamana kuomboleza kifo cha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Joseph Mbatia, aliyefariki dunia juzi wilayani Njombe kwa ajali ya gari.

Vilio vya kwikwi na hali ya simanzi jana vilianikiza nyumbani kwa marehemu jijini Dar es Salaam na eneo zima la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam (Terminal One), kabla, wakati na baada ya mapokezi ya mwili wa aliyekuwa naibu waziri huyo.

Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyewaongoza viongozi wakuu wote watatu wa kitaifa na mamia ya waombolezaji wengine wakiwamo makada wanawake wa Chama Cha Mapinduzi waliokuwa wamevalia mavazi rasmi ya chama hicho katika kuupokea mwili wa Mbatia.
Mwili wa kiongozi huyo aliyepata kuwa Mweka Hazina wa Taifa wa CCM, ulifikishwa uwanjani hapo majira ya saa 7:59 kwa ndege ya serikali aina ya Fokker 50, yenye namba za usajili 5H-TGH ambayo pia ilibeba mwili wa dereva wa naibu waziri huyo, Anakleti Mogella, ambaye naye alipoteza maisha katika ajali hiyo hiyo.
Ilipotua na kusimama, wahudumu walifungua mlango na aliyetangulia kushuka alikuwa ni mume wa marehemu, Dk. Joseph Mbatia, aliyekuwa ameongozana na Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Celina Kombani, ambao waliondoka Dar es Salaam jana asubuhi na ndege hiyo kuufuata mwili huo.

Baadaye Naibu Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja, alikabidhiwa bendera ya taifa, ambayo aliingia nayo ndani ya ndege na kuitumia kufunika sanduku lililokuwa na mwili wa Mbatia kabla halijateremshwa.

Sanduku hilo lilipitishwa mbele ya Rais Kikwete, Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, John Samwel Malecela na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambao waliweka mikono yao juu ya jeneza hilo kama ishara ya kumwomboleza.

Aidha, baada ya kumalizika kwa tukio hilo mwili wa Mbatia uliingizwa kwenye gari maalumu la kubebea wagonjwa aina ya Land Rover Defender, lenye namba za usajili 1776 JW04, na maiti ya dereva nayo ilipakiwa kwenye gari la kubebea wagonjwa aina ya Land Rover Defender lenye namba 1744 JW04, mali ya Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam, ambapo zilipelekwa kuhifadhiwa kwenye hospitali hiyo.

Muda mfupi baada ya msafara wa magari ya maiti kuondoka uwanjani hapo, viongozi wote wakuu wa kitaifa walikwenda kuwapa pole watoto wa marehemu; Philip, Yolanda, Junior na Charles, ambao walikuwa wanalia kwa uchungu kwa kuondokewa na mama yao.
Viongozi wengine waliojitokeza kuupokea mwili wa marehemu ni mawaziri na naibu mawaziri, Mnadhimu Mkuu wa (JWTZ) Meja Jenerali Abdulaman Shimbo, makatibu wakuu wa wizara mbalimbali, viongozi wa vyama, wabunge na wananchi wa kawaida.

Mara baada ya mwili kuwasili uwanjani hapo, Rais Kikwete aliwaongoza viongozi mbalimbali katika kuwashika mikono na kuwakumbatia watoto, mume na ndugu wengine wa marehemu ambao walikuwa na huzuni kubwa.

Muda wote akiwa uwanjani hapo, Yolanda, mtoto pekee wa kike wa marehemu, alikuwa akilia kwa kwikwi, huku akiwa amekumbatiwa na mtu mmoja aliyetajwa kuwa ndugu wa karibu wa familia ya Mbatia.
Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya mwili wa marehemu kuwasili, Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, alisema kuwa mwili wa marehemu ungehifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo na jana jioni maombolezo yangeendelea nyumbani kwa marehemu, Oysterbay, Mtaa wa Uganda, nyumba namba 120.

Waziri Chenge alisema mwili wa marehemu utatolewa Lugalo leo saa moja asubuhi na kupelekwa nyumbani. Hata hivyo, alisema bado haijafahamika iwapo ibada ya kumwombea marehemu itafanyika kanisani au nyumbani kwa marehemu na kuongeza kuwa baada ya ibada, saa nane mchana mwili huo utapelekwa uwanja wa ndege kwa ajili ya kusafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro ambako mazishi yatafanyika.

Naye Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye jana asubuhi alikwenda nyumbani kwa marehemu kabla ya kwenda kuulaki mwili wa mbunge huyo wa Viti Maalumu, alisema Ofisi ya Bunge imepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa, kwa kuwa marehemu alikuwa ni kiongozi mchapakazi na hivyo kifo hicho ni pigo.

Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Augustine Mrema, ambaye naye alifika nyumbani kwa marehemu kutoa pole, alisema marehemu ni mmoja wa viongozi wanawake waadilifu na kutoa pole kwa familia kwa niaba ya chama chake.

Wakati huo huo, Mweyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amemtumia Rais Kikwete salamu za rambirambi kutokana na kifo hicho.

Katika salamu hizo, Profesa Lipumba alisema alipokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mbatia.
“Nilimfahamu marehemu tangu tulipokuwa wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1973-76. Toka akiwa mwanafunzi, marehemu alikuwa mchapakazi, mwenye bidii na nia ya kujiendeleza na kushirikiana na wenzake. Kama kiongozi mwanamke, alikuwa mfano mzuri kwa wanawake wengine katika nchi yetu. Na kwa kweli Watanzania tulikuwa bado hatujautumia kikamilifu uwezo wa Mbatia,” alisema.

Nao wanawake wa CHADEMA, katika taarifa yao kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Ofisa Mwandamizi Taifa Kurugenzi yya Wanawake wa chama hicho, Mary Jumbe, wamesema wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mbatia.

Wamesema taifa limepoteza mmoja wa viongozi katika harakati za maendeleo ya jamii, jinsia na watoto na kuwa wanatoa pole kwa familia ya Mbatia na marehemu wote waliofariki kwenye ajali hiyo.

Aidha, wanawake hao wa CHADEMA wamesema wanafadhaishwa na wimbi la ajali za barabarani zinzoendelea kutokea hapa nchini.
“Wakati umefika kwa serikali kutangaza hali hii kama sehemu ya majanga yanayolikabili taifa ili mikakati madhubuti iwekwe kuzuia ongezeko la ajali ambazo zinachangia katika kuacha wanawake wengi kuwa wajane na watoto kuwa yatima,” ilisema taarifa hiyo ya CHADEMA.


Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba, kwa niaba ya chama hicho, naye alituma salamu za rambirambi kwa Rais Kikwete na kuwataka watu kufahamu kuwa kuondokewa na Mbatia ni mapenzi ya Mungu.
Katibu Mkuu huyo wa CCM amekielezea kifo hicho kuwa kimeacha pengo kubwa kwa serikali, CCM na jamii kwa ujumla. Alisema marehemu atakumbukwa kwa ucheshi, uhodari wa kazi na upendo wake kwa watu.

“Mbatia alikuwa amana ya Mwenyezi Mungu, kwa chama na serikali yetu. Mungu ameichukua amana yake kutoka kwetu ili akaitumie kwa kazi nyingine. Hatuna uwezo wa kumzuia zaidi ya kumshukuru,” alisema Makamba.

Kutoka Iringa, inaripotiwa kuwa maelfu ya wananchi mkoani humo jana walijitokeza kuuaga mwili wa Mbatia, kabla ya kusafirishwa kwa ndege hadi Dar es Salaam.

Hata hivyo, wananchi hao hawakupata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa naibu waziri huyo na akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Bernard Nzungu, aliwaambia wananchi waliokuwa nje ya chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa kuwa jambo hilo haliwezi kufanyika kutokana na ufinyu wa muda.

Mwili wa Mbatia pamoja na wa dereva wake, Anakleti Mogella, ambaye naye alifariki katika ajali hiyo, ilisafirishwa kwa ndege iliyoondoka kuelekea Dar es Salaam jana majira ya saa 6:30 mchana.

Baadhi ya viongozi waliokuwa katika msafara huo ukiongozwa na Naibu Waziri wa Tamisemi, Celina Kombanya ni pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Lawrance Masha na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk. Emmanuel Nchimbi.
Wengine waliokuwa katika msafara huo ni mume wa marehemu, Dk. Mbatia, mtoto wa kiume wa marehemu na baadhi ya wanafamilia. Mwakilishi wa Jeshi la Polisi Tanzania, aliyemuwakilisha Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema, Kamishna wa Polisi Paul Chagonja, alisema ajali zinazoendelea kutokea sehemu mbalimbali nchini zinaendelea kuwakumbusha watumia barabara kuzingatia sheria za barabarani.

Katika ajali hiyo, gari la waziri huyo aina ya Nissan Safari lenye namba za usajili T 724 AGZ, liligongana uso kwa uso na gari lenye namba T 299 AFJ aina ya Mitsubishi Fuso mali ya Jackson Kilagwa wa Rujewa, Mbeya.

Kamishna Chagonja alisema pamoja na Naibu Waziri na dereva wake kufariki papohapo, msaidizi wa dereva wa roli hilo, Castory Kilangwa, naye alifariki papo hapo.

Dereva wa lori hilo, Peter Mangula, mkazi wa Makambako, wilayani Njombe, aliyenusurika katika ajali hiyo, alitoroka baada ya ajali hiyo na Jeshi la Polisi limeahidi kumsaka mpaka apatikane.
Nicholaus Lubava na Dastun Gonze, waliokuwemo kwenye lori hilo lililokuwa limebea mbao, walijeruhiwa vibaya kwa kuvunjika miguu na mikono ambapo walipelekwa katika Hospitali ya Kibena, Njombe.

Source: Tanzania Daima

Au mpaka salaam zitolewe na Cheamani ndo zinaonekana ni salaam za Chama?
 
si mpaka wasome.. na unadhani atakuja na kuomba radhi au kujisahahihisha? wangekuwa na ujasiri wa mwanakjj kuombaga radhi wangejijengea heshima kidogo.

asante.
 
Shalom you will have to live with it, ndo unafiki wetu sisi watanzania wakujifanya unamthamini mtu pale anapokuwa na cheo! Na I can tell you wengi humu wakati huyu maza anateuliwa walimponda na wengi walikuwa hata kumjua hawamjui, lakini kapatwa na mauti wanajifanya wako soooclose to her and her family!!!!

Yaani, no wonder tutaendelea kuwa maskini tuu, maana tuna umaskini wa FIKRA! We jiulize what is the connection of CHADEMA na mama Mbatia(RIP) au inabidi akifa kila kiongozi/waziri vyama na taasisi mbali mbali vitoe matamko? how about us wananchi because we are non issues? au kwa vile hatuna vyeo serikalini? its so disguisting with this level of hypocricy, hii siyo siasa sasa ni unafiki wa hali ya juu!!! Lakini ndo tunaambiwa ndo demokrasia yenyewe!!
 
By the way thats FD for you, he is always willing to look the other side of the coin! and I always salute him for that!
 
Kifo kinampata kila mtu, kifo hakina chama wala fisadi wala kabila wala rangi, sasa mambo ya nani katoa salam za rambirambi, nani hajatoa, huo ni ulimbukeni wa hali ya juu. Katika masuala ya misiba, hakuna umaarufu, wala siasa, ukifa umekufa, na wengi watafuata, yeye kashatangulia kupumzika, nasi tutamfuata, eti Chadema hawajatoa salam za rambirambi? Duh, hivi hatuna kazi ya kufanya enh? Tanzania itaendelea kuwa maskini milele, kama hawa ndio viongozi wa kesho, no way.

Mtu wa Pwani, nadhani wewe ni muumini mzuri tu, muogope Mwenyezi Mungu, vitu vingine si vya kujadili hapa, usije ukapate laana bure.
 
Lakini hata kama tukizungumzia vyama vya Siasa, Mtu wa Pwani ina maana chama alichoona hakijatoa salam za rambirambi ni CHADEMA tu? Mbona hajahoji kuhusu CHAUSTA, SAU, NLD, DP na vinginevyo?
 
Lakini hata kama tukizungumzia vyama vya Siasa, Mtu wa Pwani ina maana chama alichoona hakijatoa salam za rambirambi ni CHADEMA tu? Mbona hajahoji kuhusu CHAUSTA, SAU, NLD, DP na vinginevyo?

Labda kwa vile chadema ndicho tishio kwake,maana tuna vyama nyomi lakini yeye kachagua chadema tu.
 
ndicho kinachoitw makini hapa, hivyo vyengine sio makini, au simvyo msemavyo?
 
Huyu jamaa wa Pwani yeye anadhani Chadema ni Mbowe kama ilivyo kwa CCM kwamba lazima aseme JK .Chadema imeshiriki sana huu msiba mkubwa kuliko hata CCM. Kumbuka Zitto was first kuwa katika aneo la ajali na alisomba majeruhi .Sasa ulitaka Chadema ifanye nini ama una uoga wa kusikia na kuona kwamba kweli Chadema ni makini ?
 
Huyu jamaa wa Pwani yeye anadhani Chadema ni Mbowe kama ilivyo kwa CCM kwamba lazima aseme JK .Chadema imeshiriki sana huu msiba mkubwa kuliko hata CCM. Kumbuka Zitto was first kuwa katika aneo la ajali na alisomba majeruhi .Sasa ulitaka Chadema ifanye nini ama una uoga wa kusikia na kuona kwamba kweli Chadema ni makini ?


lunyungu....

KWANI NA WW CHADEMA?



mtu wwa pwani...

hapo umekosea mzee mwenzangu,zitto nasikia alisaidia kuitoa maiti ndani ya gari.sema hatujasikia mwenyekiti mbowe na mnyika wakitoa rambirambi.
 
Asante bwana Keil kumletea habari ndefu zaidi ya aliyoileta Mtu wa pwani (ambayo hata waandishi wake hawataki kujulikana, mwandishi wetu).

By the way hata zito alikuwepo sehemu ya ajali, na huenda ni miongoni mwa watu wa awali kutoa pole na kutoa taarifa pia.
 
KWA NINI DEREVA WA MAREHEMU MHE. SALOME MBATIA HAZUNGUMZIWI.

Kuna habari za kuaminika kuwa Dereva aliyempeleka Mhe. Mbatia kwenye ziara ya kikazi huko njombe alikuwa 'House Boy'(shangaa).

Taarifa hizo zimenedelea kusema kwamba miezi michache iliyopita dereva wa Mhe. Mbatia aliachishwa kazi na Mhe. waziri huyu ambaye kwa sasa ni marehemu. Baada ya kumwachishwa kazi aliomba apewe dereva mwingine, na akapewa. Sasa hapa sijui ni Mungu mwenyewe au vipi, dereva huyu mpya aliarifiwa kuhusu safari hiyo ya Iringa, kwa bahati mbaya, lakini nzuri kwa dereva huyo, siku ya safari alifika na gari la kazini akiwa amechelewa na kukuta Mhe. kisha ondoka kuelekea Iringa akiwa na huyo House boy ambaye naye pia ni dereva kwani amekuwa akiendesha magari ya nyumbani kama kupeleka watoto school na kumpeleka Mhe. kwenye shughuli binafsi.

Dereva huyo baada ya kuambiwa kwamba Mhe. kisha ondoka, alimpigia simu kutaka kujua kulikoni. Mhe. alimwambia kuwa baada ya kuona amechelewa kufika(yaani dereva) aliamua kutumia gari lake binafsi(ambayo imepata ajali) ili awahi shughuli za serikali huko Iringa.

Hata hivyo habari zinaendelea kusema kuwa, Mhe. waziri ilibidi atoe maelekezo kwa dereva huyo kwa njia ya simu, kuendelea kufanya kazi za pale nyumbani ambazo kimsingi alikuwa akizifanya huyo House Boy. Mawasiliano kati ya Dereva aliyebaki na Mhe. yamekuwa yakifanyika karibu siku nzima,kwa maana ya marehemu kutoa maelekezo ni kipi afanye hapo nyumbani. Dereva huyo amewasiliana na Mhe. karibu siku nzima. Mawasiliano kati yao yalikatizwa na ajali hiyo.

Nyeti zinasema, House Boy huyo ambaye ni mkazi wa kinondoni, alikuwa na mke na watoto, pia alikuwa ni kipenzi cha Marehemu. Chanzo cha habari hizi kinasema kuwa kuna wakati House Boy huyo alitaka kuacha kazi lakini mama kwa mapenzi dhidi ya house boy huyo alimuongezea dau kubwa na kumfanya abakie hapo.Safari za mara kwa mara kati ya house boy huyo na marehemu kilikuwa ni kitu cha kawaida kwao.

Habari hizi yawezekana kuwa ni kweli, maana hakuna taarifa ni wapi dereva aliyekuwa na marehemu amepelekwa. Kwa wale wanaofahamu tujulisheni. Dereva wake aliyepewa na serikali inasemekana yupo hai na anamshukuru God kwa kuchelewa kufika hapo kwa Mhe. kwa ajili ya safari, vinginevyo naye angekufa.

Naomba kuwasilisha, na mwenye habari zaidi achangie au tufuatilie kujua kulikoni.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi 'Amen'
 
Back
Top Bottom