Gangongine
JF-Expert Member
- Dec 31, 2015
- 3,854
- 1,776
Jana nilimsikia Mwandishi mmoja wa Habari ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo moja la Dar es Salaam kuwa yeye hawezi kununuliwa na CCM kwa kuwa anajua thamani yake. Alisema hivyo baada ya uvumi kuwa anajiandaa kuhamia CCM.
Nimetafakari sana manaeno yake nikajiuliza swali la "kijinga" kuwa Nyalandu aliyehamia CHADEMA hivi majuzi naye amenunuliwa? Au wanaonunuliwa ni wale wanaohamia CCM pekee? Ni busara CHADEMA na UKIWA kwa ujumla wakatafakari kwa nini kuna wimbi la watu kuhamia CCM kipindi hiki. Pia wajiulize kama Nyalandu aliachia Ubunge na Marupurupu yake akahamia CHADEMA ina maana amepewa pesa? Nasema hivyo kwa kuwa Mtulia kaachia Ubunge sawa na alivyofanya Nyalandu.
Acheni fikra potofu za kuwaona wanaokwenda CCM wamenunuliwa ila wanaokwenda CHADEMA na UKIWA ni Wazalendo. Muda si mrefu tutawaona Viongozi wengi wanakuja CCM kwa hiyari na utashi wao na siyo kwamba wamenunuliwa. Muhimu ni CHADEMA na UKIWA kujitafakari WAMEKOSEA WAPI?
Nimetafakari sana manaeno yake nikajiuliza swali la "kijinga" kuwa Nyalandu aliyehamia CHADEMA hivi majuzi naye amenunuliwa? Au wanaonunuliwa ni wale wanaohamia CCM pekee? Ni busara CHADEMA na UKIWA kwa ujumla wakatafakari kwa nini kuna wimbi la watu kuhamia CCM kipindi hiki. Pia wajiulize kama Nyalandu aliachia Ubunge na Marupurupu yake akahamia CHADEMA ina maana amepewa pesa? Nasema hivyo kwa kuwa Mtulia kaachia Ubunge sawa na alivyofanya Nyalandu.
Acheni fikra potofu za kuwaona wanaokwenda CCM wamenunuliwa ila wanaokwenda CHADEMA na UKIWA ni Wazalendo. Muda si mrefu tutawaona Viongozi wengi wanakuja CCM kwa hiyari na utashi wao na siyo kwamba wamenunuliwa. Muhimu ni CHADEMA na UKIWA kujitafakari WAMEKOSEA WAPI?