CHADEMA mmejifunza nini maana ya demokrasia?

fasiliteta

JF-Expert Member
Jul 2, 2014
2,165
3,655
Habari za muda huu wakuu.

Bila kuwachosha niende moja kwa moja katika maudhui ya uzi huu.

Hivi karibuni tumeshuhudia na tunaendelea kushuhudia kwa kinachoitwa democracy katika chama kikuu cha upinzani Tanzania (CHADEMA) kupitia chaguzi zake mbalimbali hasa hizi nafasi za uenyekiti.

Kiukweli ni hatua nzuri sana katika ustawi wa democracy nchini pale chama kinapojali maoni/mapendekezo/Machaguo ya wanachama na wananchi wao.

Nipende kutoa pongezi kwa dhati kabisa kwa chama hiki huku nikitazama nafasi ya mwenyekiti wa chama ngazi ya Taifa ambapo Mh. Mbowe anagombea kwa awamu ya nne katika historia ya chama hicho.

Huku mtaani watu wamekuwa na maoni tofauti katika hii nafasi nyeti kwa chama huku wakiendelea kujiuliza sana hili suala linawezekanaje kwa mwenyekiti kugombea tena licha ya kuhodhi madaraka ya uenyekiti muda mrefu?

Majibu ya wanachama husika yamekuwa ni mengi sana huku wakijitapa kuwa Mh.mbowe ndiye mtu sahihi na aendelee kuwavusha daraja kutokana na kukitendea haki kiti chake kwa muda aliokaa hivyo hawaoni haja ya kutafuta mbadala zaidi ya yeye kuendelea kukitumikia chama kwa nafasi hiyo.

Sisi kama wananchi hatuna shaka na hilo kutokana na baadhi ya sababu hizo. Zaidi tumejifunza kitu kumbe uwezekano wa democracy kutumika pindi tu mtu anapofanya vizuri na hivyo kupewa nafasi ya kuongoza mihula zaidi ya miwili kama wengine tulivyojiaminisha ndio mihula ya kiuongozi kidemokrasia inawezekana.

Swali kwenu wana CHADEMA je wale walioona mazuri ya Rais wao mchapakazi Mh.Dr John Pombe Magufuli walikuwa sahihi kudai aongezewe muda wa kukaa madarakani kwa kutumia democracy hiyo hiyo mnayoifanya kwa sasa ndani ya Chama?

Je, kuna ubaya tukamuomba Mheshimiwa Rais naye aendelee kuchapa kazi kwa vipindi vingi zaidi baada ya kuona matunda yake kwa muda mfupi?

Je! CHADEMA sasa wamegundua Democracy inaishi na si ya kubezwa?Maana kumbe yawezekana kama alivyoweza na anavyoendelea kuweza Mh. Mbowe.

Mwisho niwaombe CHADEMA na wanachama wake, kuna kipengele katika democracy kinaelezea nguvu ya POLITICAL TOLERANCE au kiswahili UVUMILIVU KATIKA NYANJA ZA SIASA.

Nyinyi mmeweza sasa na bila shaka mnaenda kumsimika Mh. Mbowe kwa muhula wa nne.

Muda ukifika kwa wengine basi mnyamaze kimya na muache DEMOCRACY iendelee kuishi.

Msumeno hukata pote pote, ni zamu yenu sasa na zamu yao ikifika basi ndio Democracy hiyo wajomba.
 
Kwani Katiba yao inasema mwenyekiti agombee mihula mingapi? Tuanzie hapo, maana demokrasia ni pamoja na kufuata katiba.
 
Kwani Katiba yao inasema mwenyekiti agombee mihula mingapi? Tuanzie hapo, maana demokrasia ni pamoja na kufuata katiba.
Katiba inabadilishwa kama walivyowahi badilisha CHADEMA
So yote ni Democracy tu usiwe na wasi na hilo.
Tumejifunza toka Chadema na tupo mbioni kumuomba jemedari wetu aendelee kuwatumikia waTZ
 
Katiba inabadilishwa kama walivyowahi badilisha CHADEMA
So yote ni Democracy tu usiwe na wasi na hilo.
Tumejifunza toka Chadema na tupo mbioni kumuomba jemedari wetu aendelee kuwatumikia waTZ
Sasa shida yako ni nini?
 
CCM muwekeni JPM awe mwenyekiti wenu wa maisha,hatutowaingilia!Ila mkisema Rais wa nchi,hapo ndio mnapoleta utani,hii ni nchi ya watu wote bila kujali itikadi za vyama!Sasa wanaCCM hamuwezi kutuamulia jambo nyeti kama hilo
 
Katiba inabadilishwa kama walivyowahi badilisha CHADEMA
So yote ni Democracy tu usiwe na wasi na hilo.
Tumejifunza toka Chadema na tupo mbioni kumuomba jemedari wetu aendelee kuwatumikia waTZ
Aendelee kuitumikia CCM na si Tz!Kama mnatafuta machafuko nchi hii,jaribuni hilo
 
Aendelee kuitumikia CCM na si Tz!Kama mnatafuta machafuko nchi hii,jaribuni hilo
Punguza munkari babaaa, hiyo ndio democracy. Wananchi wenzetu wametuonyesha mwanga pasipo machafuko yoyote.
Ni Democracy ya wengi wape ndio itatumika tu.
 
Katiba ya Tanzania unasemaje kuhusu ukomo wa Raisi? Si mihula miwili tu? Katiba imeweka ukomo. Hata hivyo huyu hajamaliza hat mihula wa Kwanza, wasiwasi wenu ni nini, si muache amalize mihula wa kwanza, aingie ulingini achaguliwe halafu tuone atafanyaje huo muhula wapili ambao katiba inamruhusu kuhudumu? Akimaliza muhula wapili, ikiwa atakuwa amekidhi vigezo hivyo, then hoja hii ikiletwa hapa itakuwa na mntiki. Kwasasa nikupotezeana muda Tu.

Pili mbowe ni mwenyekiti wa chama. Hahusiani na uraisi wajamuhuru ya muungano wa Tanzania. Yeye anawahusu Wana Chadema peke yao. Maswala Yao chama waachieni bwanachama waamue wenyewe. Kama katiba yao inaruhusu, Hilo linawahusu nini?

Raisi wa jamuhuru anatuhusu Sisi site, si swala la CCM wala Chadema au chama kingine cha siasa, ni swala la watanzania wote. Hivyo halipaswi kuchezewa nawala CCM hawana mamlaka yakuwalazimisha watanzania wote waongozwe na huyo. Ni swala la wote na niswala la katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Usiyalinganishe haya mawili. Chama na Serikali. Kuhusu uwenyekiti wa CCM hakuna shida, badilisheni mnavyotaka. fasiliteta,
 
nzotangai,
Mkuu mi si mwanachama,ila ni miongoni mwa wananchi wengi walioona kasi ya Rais na kuguswa na ayafanyayo kwa muda mfupi.

Tupaze sauti jembe letu liendelee kupiga kazi.Kumpata kama huyu itatuchukua miaka mingi sana.

Katiba ya TZ inabadilika tu muhimu ni wengi wape
 
CCM muwekeni JPM awe mwenyekiti wenu wa maisha,hatutowaingilia!Ila mkisema Rais wa nchi,hapo ndio mnapoleta utani,hii ni nchi ya watu wote bila kujali itikadi za vyama!Sasa wanaCCM hamuwezi kutuamulia jambo nyeti kama hilo
sawa. ila kumbuka sisi mwenyekiti wetu ndiye kiongozi wa nchi. Nashukuru kwa kuelewa
 
Chadema mmeniangusha sana, mbowe umeiua chadema. Nami sio mwanachadema tena. Mm nabaki tu kua mwananchi huru, sio ccm mafisadi, wala chadema masultan, wala act ya yule muha ambae nae ni kama mbowe.
Upinzani tz ni miradi ya watu.
 
Ni Mbowe Mbowe VIBARAKA wa Lumumba riziki yao ya buku7 anatembea nayo Mbowe. Wasipo mtaja Mbowe hamna kula. Mbowe asubuhi, Mbowe mchana, Mbowe jioni na Mbowe usiku. Lumumba kazi moja tu Mbowe Mbowe Mbowe Mbowe.
Namuelewa Magufuli anavyoita WAPUMBAVU WAKE.
 
sawa. ila kumbuka sisi mwenyekiti wetu ndiye kiongozi wa nchi. Nashukuru kwa kuelewa
Sio lazima mwenyekiti wa CCM kuwa Rais!!Anaweza kuacha urais baada ya muda wake kikatiba kuisha ila akaendelea kuwa mwenyekiti wa CCM kama mtampenda zaidi!
 
Katiba ya CHADEMA ilikuwa na ukomo wa mwenyekiti ila ineyeyushwa...

Dont you worry tutapiga kura kubadilisha kipengele cha kubadili ukomo wa Raisi.. tukishinda ataendelea zaidi ya awamu 2.

Suala la ukomo wa uongozi ama mwenyekiti ama Raisi linazingatia umahiri na umuhimu wa kiongozi kama ilivyo mfano wa Mbowe ndani ya chadema...

Katiba sio biblia tutarekebisha.

Na demokrasia itatumika kufanya maanuzi sahihi nzotangai,
 
Back
Top Bottom