CHADEMA mlipopeleka mboga ndiyo mfuate chakula. Watanzania siyo mazwazwa...

JOYOPAPASI

JF-Expert Member
Jan 10, 2016
250
408
*CHADEMA MLIPOPELEKA MBOGA NDIYO MFUATE CHAKULA*

Nimeona Malalamiko ya CHADEMA wakiitaka Serikali iwaeleze kwanini hawakupewa nafasi ya kuingia ndani ya Uwanja wa Uhurru kuungana na Watanzania wengine kumuenzi kipenzi chao *Rais Mstaafu Benjamini Mkapa.*

Mwalimu Nyerere alishawahi kusema kiongozi mzuri ni yule anayeheshimu mamlaka iliyopo madarakani, hakuna asiyefahamu hata mtoto wa darasa la 3 anayefundishwa somo la Uraia anaambiwa kiongozi Mkuu wa Nchi ni Rais na si mwingine.

Kuna sababu bilioni za kuamini, CHADEMA hawakuwa na nia dhati ya kushiriki maombolezo ya Rais Mstaafu Mkapa kama *wanavyojishaua* sasa hivi bali lengo lao lilikuwa ni kupata huruma ya kisiasa.

Taratibu, muongozo na maadili ya viongozi wa Umma, sehemu ambayo Mkuu wa Nchi anakuwepo kiitifaki yeye ndiye mtu wa mwisho kufika kwenye eneo hilo na baada ya kufika yeye tukio ndiyo linaanza, wanaokuja baada yake wanaruhusiwa kuingia kwenye eneo la tukio kama raia wa Kawaida, haijalishi nafasi yake ndani ya Serikali au nje ya Serikali, CHADEMA hawalijui hili ndiyo maana walifika baada ya Mkuu wa Nchi, Waligoma kukaguliwa, walisababisha fujo wakati kulikuwa na viongozi wa Mataifa mengine.

Kituko hiki cha CHADEMA leo kimeonesha *Ombwe kubwa la kiuongozi* lililopo ndani ya chama hicho, walitaka kulitumia tukio la huzuni kujinufaisha kisiasa, baada ya kuona jana Watanzania waliwagomea Uwanja wa Ndege na wakaji kuta wao wanachama wao Uchwara.

CHADEMA wameumbuka sana na watanzania wameshawajua kama hawa watu wanashindwa kuheshimu Mamlaka ya viongozi wa Umma wataweza kuwaongoza Watanzania ambao watawapigia kura Oktoba 28, unagundua hawana uwezo wa kuwatumikia Watanzania, *chaguo pekee lililobaki ni John Pombe Magufuli.*

Waswahili wanasema *kurukaruka kwa Maharage ndiyo kuiva kwake,* CHADEMA wamekosa sera na ajenda za kuwaambia wananchi kwenye Uchaguzi ujao, hivyo wameanza visanga na vitimbwi kama watoto wa kambo, niwaambie mtakula mlipopeleka mboga tukutane kwenye box.
 
Mbona sioni mtu mwenye hekima ya kuliunganisha taifa na kujali maslahi ya Watanzania katika CCM zaidi ya Mwenyekiti ambaye amethibitisha uzalendo wake na uhanga kwa taifa?

Hizi siasa za chuki na kuzomea, ubaguzi bila kujali hali halisi na ubindamu, zinaongeza tija gani katika ustawi wa Tanzania?
Mbona sikuoni hata kama unaelewa tofauti kati ya serikali, wananchi, vyama vya siasa na uongozi?

Ninakuona mtu wa chini tena aliyenje kabisa ya matazamio ya Rais wetu na watu kama wewe ndio mmekuwa mzigo kwa Raisi kila wakati anafanya teuzi na kubadilisha watu.

Wewe una sera gani unayowaambia watu hapa zaidi ya kujihami kiharamia?

Unaowatukana Chadema Mazwazwa, huoni unamdhalilisha rais wetu ambaye amepata viongozi makini sana kwa teuzi za waliopikwa na kuivishwa CHaDEMA? Ni asilimia ngapi ya hao amewatumbua? Asilimia ngapi ya wateule waliotoka cccm amelalamikia na kuwatumbua?

Tumechoka na siasa dhaifu. Matusi safari hii watanzania hatutaki. Tunataka facts. Usirudia kuwaita Watanzania Mazwazwa. Zwazwa ni wewe mwenyewe.
 
[SUP]Sasa na huyu kweli analipwa pesa zetu aiseee..Mh.Pole Pole naomba ulifanyie kazi ili[/SUP]
 
  • Kicheko
Reactions: Cyb
Huyu mzee sasa hivi story zake zimeisha baada tu ya kufujikwa lile zege.
Msiba umekwisha na habati zake zimeisha, sasa hiv lete story zingine tu Yona.
 
Huyu mwenyekiti wenu anaesema ninakupa mshahara, gari na mafuta alafu umtangaze mpinzani amepita ndiye anaejua demokrasia?
 
Chadema kiukweli Si wakutawala nchi bado wana mambo ya kitoto sana
Na kujiona wao maalumu nchi hii
Huu wako ndio utoto, na ili kuthibitisha huwezi hata ukaandika sentensi moja inayojitosheleza kuelezea 'mambo ya kitoto ya Chadema ni yapi'!
 
Chadema mnamambo ya kitoto sana, jaribuni kujipanga kimkakati. Najua nia yenu mlitaka mkiingia mpate attantion kwa watu mwisho mvuruge msiba. Nasema mikakati yenu bado ya kitoto sana.
Kwahiyo hiyo ndio sababu ya wao kuzuiliwa kuhudhuria msiba?
 
Kwahiyo hiyo ndio sababu ya wao kuzuiliwa kuhudhuria msiba?
Wewe unaona ilkua sawa walichotaka kukifanya. Sizan km wangewahi na kuingia bila ya kuandamana wangezuiliwa. Jamn upinzani unamanufaa ndani ya nchi lakini upinzani wa Chadema sijui km utatusaidia lolote. Hata kupangilia matukio yao hawajui kabisa na wanachotegemea ni ili wafanyiwe mabaya waonewe huruma na wananchi.
 
Mapumbavu na malofa wakubwa, Mzee Mkapa 2015 Jangwani

Sasa nakubaliana naye moja Kwa moja
Kama unaona utaifa unadumishwa kwenye hafla ya kuaga "maiti" ya rais mstaafu pekee ndiyo ukomavu ni bure.Usifanye watu wakamsema vibaya marehemu!
 
Wewe unaona ilkua sawa walichotaka kukifanya. Sizan km wangewahi na kuingia bila ya kuandamana wangezuiliwa. Jamn upinzani unamanufaa ndani ya nchi lakini upinzani wa Chadema sijui km utatusaidia lolote. Hata kupangilia matukio yao hawajui kabisa na wanachotegemea ni ili wafanyiwe mabaya waonewe huruma na wananchi.
Sasa mbona umeacha kujibu swali halafu unajipa kiwango cha kuni lecture? Anyway, nini ilikuwa busara kwa polisi kushughulika na watu waliochelewa msibani?
 
Back
Top Bottom