CHADEMA - Mlima Mrefu Wenye Watu Wengi

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Amani iwe nanyi wanajamvi!

Nimelazimika kuja na hoja yenye lengo la kuwasaidia wale wote wanaoona wanachama wa CHADEMA wakiwa kimya licha ya kusikia na kushuhudia maneno, vurugu, rafu na propaganda kadhaa zenye lengo la kukidhoofisha chama hicho.

Nipende kuwajuza wote wenye kutekeleza jukumu la kuidhoofisha CHADEMA kwa kutumwa au kwa kujitafutia fursa na umaarufu wajue kwamba CHADEMA ni MLIMA MREFU WENYE WATU WENGI.

CHADEMA NI MLIMA MREFU WENYE WATU WENGI: wengine wanapanda mlima; wengine wanashuka.
Toka siku CHADEMA imesajiliwa wapo watu waaminifu wanaopanda mlima kwa mateso mengi, wakiweka mikakati kila siku namna ya kufika kileleni (kuwaletea watanzania ukombozi wa kweli) Hawa wameendelea kwa uaminifu kujituma bila kujali kwamba wao wanakosa fursa, kwamba wanaonewa sana na mfumo wa utawala uliopo madarakani na pengine kunyanyapaliwa na jamii na familia

kwa upande mwingine wapo walioingia CHADEMA pengine wakiwa na nia nzuri mwanzoni lakini baadaye kusudi la kwanza liliondoka na kubakia wakiigiza utume. Walipiga mwendo vizuri mwanzoni lakini baadaye wameshindwa kuendelea na safari ya ukombozi. Sasa hawa wameanza safari ya kushuka mlima. wakati wanashuka bila kujali walikuwa wamefika juu kiasi gani wao wanapishana na wengine wanaopanda.

La hatari zaidi ni pale ambapo watu hao wanaoshuka mlima wanapotumiwa kudhoofisha harakati za CHADEMA. Hawa wanaungana na wengine walioingia CHADEMA ili kufanya kazi moja tu ya kukidhoofisha chama. Kwa pamoja washuka mlima hawa wanasababisha chokochoko nyingi ili kuvuruga safari ya wenzao ya kupanda mlima kuleta ukombozi kwa watanzania. Wanaweka vigingi njiani wapandaji washindwa kuvuka. Wanaharibu malengo kwa kuwachonganisha wapandaji wakiwa waanzilishi wakuu wa mijadala isiyo na tija kwa ukombozi na yenye lengo la kuwakatisha tamaa wenye nia thabiti ya kufika kileleni.

Ninapenda kuwahakikishia wale wote wanaoshuka mlima wa CHADEMA kwamba "bila kujali idadi yao, umaarufu wao, utajiri wao, fursa zao, kulindwa kwao na watawala na dola na mbinu zao; kila wanaposhuka wajue wengi pia wako njiani wakiendelea na safari ya kupanda". Washuke waishie hadi usalitini, wapandaji wataendelea kupanda hata kama ni kwa mateso na dhiki nyingi.

ndugu yangu jipime. Je wewe unapanda ama unashuka mlima?

Mimi nilianza kupanda, sijawahi kufikiria kushuka, sitashuka kamwe, nitaendelea kupanda, nitawasaidia wengine waamue na waendelee kupanda.
Wakichoka njiani nitawatia nguvu,
Wakichubuka nitawaganga vidonda vyao,
Wakipata kiu nitawapa maji wanywe,
Wakivunjwa moyo nitawaimarisha,
Wakikosa mpango nitawapa mkakati.

tutakwenda pamoja bila kurudi nyuma wala kuchoka na "Hakuna kulala Mpka Kieleweke"
 
amani iwe nanyi wanajamvi!

Nimelazimika kuja na hoja yenye lengo la kuwasaidia wale wote wanaoona wanachama wa chadema wakiwa kimya licha ya kusikia na kushuhudia maneno, vurugu, rafu na propaganda kadhaa zenye lengo la kukidhoofisha chama hicho.

Nipende kuwajuza wote wenye kutekeleza jukumu la kuidhoofisha chadema kwa kutumwa au kwa kujitafutia fursa na umaarufu wajue kwamba chadema ni mlima mrefu wenye watu wengi.

Chadema ni mlima mrefu wenye watu wengi: Wengine wanapanda mlima; wengine wanashuka.
Toka siku chadema imesajiliwa wapo watu waaminifu wanaopanda mlima kwa mateso mengi, wakiweka mikakati kila siku namna ya kufika kileleni (kuwaletea watanzania ukombozi wa kweli) hawa wameendelea kwa uaminifu kujituma bila kujali kwamba wao wanakosa fursa, kwamba wanaonewa sana na mfumo wa utawala uliopo madarakani na pengine kunyanyapaliwa na jamii na familia

kwa upande mwingine wapo walioingia chadema pengine wakiwa na nia nzuri mwanzoni lakini baadaye kusudi la kwanza liliondoka na kubakia wakiigiza utume. Walipiga mwendo vizuri mwanzoni lakini baadaye wameshindwa kuendelea na safari ya ukombozi. Sasa hawa wameanza safari ya kushuka mlima. Wakati wanashuka bila kujali walikuwa wamefika juu kiasi gani wao wanapishana na wengine wanaopanda.

La hatari zaidi ni pale ambapo watu hao wanaoshuka mlima wanapotumiwa kudhoofisha harakati za chadema. Hawa wanaungana na wengine walioingia chadema ili kufanya kazi moja tu ya kukidhoofisha chama. Kwa pamoja washuka mlima hawa wanasababisha chokochoko nyingi ili kuvuruga safari ya wenzao ya kupanda mlima kuleta ukombozi kwa watanzania. Wanaweka vigingi njiani wapandaji washindwa kuvuka. Wanaharibu malengo kwa kuwachonganisha wapandaji wakiwa waanzilishi wakuu wa mijadala isiyo na tija kwa ukombozi na yenye lengo la kuwakatisha tamaa wenye nia thabiti ya kufika kileleni.

Ninapenda kuwahakikishia wale wote wanaoshuka mlima wa chadema kwamba "bila kujali idadi yao, umaarufu wao, utajiri wao, fursa zao, kulindwa kwao na watawala na dola na mbinu zao; kila wanaposhuka wajue wengi pia wako njiani wakiendelea na safari ya kupanda". Washuke waishie hadi usalitini, wapandaji wataendelea kupanda hata kama ni kwa mateso na dhiki nyingi.

Ndugu yangu jipime. Je wewe unapanda ama unashuka mlima?

Mimi nilianza kupanda, sijawahi kufikiria kushuka, sitashuka kamwe, nitaendelea kupanda, nitawasaidia wengine waamue na waendelee kupanda.
Wakichoka njiani nitawatia nguvu,
wakichubuka nitawaganga vidonda vyao,
wakipata kiu nitawapa maji wanywe,
wakivunjwa moyo nitawaimarisha,
wakikosa mpango nitawapa mkakati.

tutakwenda pamoja bila kurudi nyuma wala kuchoka na "hakuna kulala mpka kieleweke"

mimi napanda juu na najitahidi kupanda na wengi na pia sifikirii kushuka sina uhakika na vichuguu,......hata cdm ikiwa kikundi cha wafagia barabara nitakuwamo ndani yake..............mungu ibariki cdm.....viva m4c
 
Mimi namnukuu mjumbe mmoja hapa ukumbini; "hata CHADEMA ikibaki kuwa klabu ya taarabu nitabaki kuwa mwanachama wake kuliko kujiunga na ccm au chama kingine".

Kauli yangu ya dhati: CHADEMA nitajitolea kwa moyo wangu wote kwa maisha yangu yote kukilinda, kukipigania na kukijenga.
 
Najua kwamba moyo wa kulitumikia taifa utanifanya nisichoke kupanda mlima huu!
Enyi watanzania wenzangu twendeni tupande.

napenda kuuliza je hakuna anayeweza kupanda kwa kupitia CCM?
Kama wapo wako wapi na wanapanda kivipi?
Na kama hawako kwa nini?
 
Mie mwenyewe Tangu nianze kupanda mlima wa ukombozi kupitia Chadema 2004 hadi leo sijawaza na kamwe sitawaza kushuka na endapo nitaona nimebaki peke yangu kileleni basi nitashuka na kuamua kuwa Raia Mwema.
 
Kitu gani kitanitenga na Chadema?
Mabomu,
Propaganda,hela za Ccm,vyote hivyo haviwezi kunitenganisha nayo.
Hata ZITTO hawezi kunitenga na Cdm!
 
Amani iwe nanyi wanajamvi!

Nimelazimika kuja na hoja yenye lengo la kuwasaidia wale wote wanaoona wanachama wa CHADEMA wakiwa kimya licha ya kusikia na kushuhudia maneno, vurugu, rafu na propaganda kadhaa zenye lengo la kukidhoofisha chama hicho.

Nipende kuwajuza wote wenye kutekeleza jukumu la kuidhoofisha CHADEMA kwa kutumwa au kwa kujitafutia fursa na umaarufu wajue kwamba CHADEMA ni MLIMA MREFU WENYE WATU WENGI.

CHADEMA NI MLIMA MREFU WENYE WATU WENGI: wengine wanapanda mlima; wengine wanashuka.
Toka siku CHADEMA imesajiliwa wapo watu waaminifu wanaopanda mlima kwa mateso mengi, wakiweka mikakati kila siku namna ya kufika kileleni (kuwaletea watanzania ukombozi wa kweli) Hawa wameendelea kwa uaminifu kujituma bila kujali kwamba wao wanakosa fursa, kwamba wanaonewa sana na mfumo wa utawala uliopo madarakani na pengine kunyanyapaliwa na jamii na familia

kwa upande mwingine wapo walioingia CHADEMA pengine wakiwa na nia nzuri mwanzoni lakini baadaye kusudi la kwanza liliondoka na kubakia wakiigiza utume. Walipiga mwendo vizuri mwanzoni lakini baadaye wameshindwa kuendelea na safari ya ukombozi. Sasa hawa wameanza safari ya kushuka mlima. wakati wanashuka bila kujali walikuwa wamefika juu kiasi gani wao wanapishana na wengine wanaopanda.

La hatari zaidi ni pale ambapo watu hao wanaoshuka mlima wanapotumiwa kudhoofisha harakati za CHADEMA. Hawa wanaungana na wengine walioingia CHADEMA ili kufanya kazi moja tu ya kukidhoofisha chama. Kwa pamoja washuka mlima hawa wanasababisha chokochoko nyingi ili kuvuruga safari ya wenzao ya kupanda mlima kuleta ukombozi kwa watanzania. Wanaweka vigingi njiani wapandaji washindwa kuvuka. Wanaharibu malengo kwa kuwachonganisha wapandaji wakiwa waanzilishi wakuu wa mijadala isiyo na tija kwa ukombozi na yenye lengo la kuwakatisha tamaa wenye nia thabiti ya kufika kileleni.

Ninapenda kuwahakikishia wale wote wanaoshuka mlima wa CHADEMA kwamba "bila kujali idadi yao, umaarufu wao, utajiri wao, fursa zao, kulindwa kwao na watawala na dola na mbinu zao; kila wanaposhuka wajue wengi pia wako njiani wakiendelea na safari ya kupanda". Washuke waishie hadi usalitini, wapandaji wataendelea kupanda hata kama ni kwa mateso na dhiki nyingi.

ndugu yangu jipime. Je wewe unapanda ama unashuka mlima?

Mimi nilianza kupanda, sijawahi kufikiria kushuka, sitashuka kamwe, nitaendelea kupanda, nitawasaidia wengine waamue na waendelee kupanda.
Wakichoka njiani nitawatia nguvu,
Wakichubuka nitawaganga vidonda vyao,
Wakipata kiu nitawapa maji wanywe,
Wakivunjwa moyo nitawaimarisha,
Wakikosa mpango nitawapa mkakati.

tutakwenda pamoja bila kurudi nyuma wala kuchoka na "Hakuna kulala Mpka Kieleweke"

mie bado nakaza mwendo nifike kileleni!
 
Najua kwamba moyo wa kulitumikia taifa utanifanya nisichoke kupanda mlima huu!
Enyi watanzania wenzangu twendeni tupande.

napenda kuuliza je hakuna anayeweza kupanda kwa kupitia CCM?
Kama wapo wako wapi na wanapanda kivipi?
Na kama hawako kwa nini?


Huko wapo wengi tu, ila huwaoni kwa kuwa wanapanda wakiwa wamefunika nyuso zao, na wanaongea kwa kunong`ona ili wasitambulike, nao wanazo nyenzo muhimu za kutusaidia kufika kileleni - Amini hivyo.
 
Miti isingeweza kuteketezwa na shoka tupu, ndipo ikabidi kushirikisha mti kwa kazi hiyo, yaani 'Mpini'. Hali kadhalika huwezi kushinda vita bila kukamata mateka kadhaa na kuwatumia ipasavyo.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom