Lord Diplock MR
JF-Expert Member
- Mar 16, 2015
- 1,393
- 3,234
Ndugu wanajamvi nimesikitishwa sana kitendo cha CHADEMA kufanya uchaguzi kimya kimya kulikoni?
Kwanini hili zoezi la mwaka huu la uchaguzi wa CHADEMA limekuwa likifanywa chinichini na kwa kificho hivi? Haiwezekani chama kinafanya uchaguzi kwa mfano CHADEMA Mwanza wapo ngazi ya mkoa lakini ni kama hakuna kinachoendelea. Inamaana wameanza msingi, tawi, kata, wilaya jimbo na sasa wapo mkoani hata chombo cha habari kuripoti hata kwa bahati mbaya hamna?
Haiwezekani uchaguzi wa chama kikuu cha upinzani kama CHADEMA kinafanya uchaguzi mpaka ngazi ya mkoa bila uwazi kwa kujifichaficha namna hivi kuna ajenda gani huko ndani?
Hivi mnataka mpaka ikifika zamu ya kumchagua Mbowe ndiyo tuwe taken by surprise? Mpaka mfike ngazi ya taifa? Kwanini zoezi lisiwe shirikishi hasa kwa vyombo vya habari kuanzia mapema?
Uchaguzi wa kisiri siri CHADEMA una maana gani na ni kwa maslahi ya nani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanini hili zoezi la mwaka huu la uchaguzi wa CHADEMA limekuwa likifanywa chinichini na kwa kificho hivi? Haiwezekani chama kinafanya uchaguzi kwa mfano CHADEMA Mwanza wapo ngazi ya mkoa lakini ni kama hakuna kinachoendelea. Inamaana wameanza msingi, tawi, kata, wilaya jimbo na sasa wapo mkoani hata chombo cha habari kuripoti hata kwa bahati mbaya hamna?
Haiwezekani uchaguzi wa chama kikuu cha upinzani kama CHADEMA kinafanya uchaguzi mpaka ngazi ya mkoa bila uwazi kwa kujifichaficha namna hivi kuna ajenda gani huko ndani?
Hivi mnataka mpaka ikifika zamu ya kumchagua Mbowe ndiyo tuwe taken by surprise? Mpaka mfike ngazi ya taifa? Kwanini zoezi lisiwe shirikishi hasa kwa vyombo vya habari kuanzia mapema?
Uchaguzi wa kisiri siri CHADEMA una maana gani na ni kwa maslahi ya nani?
Sent using Jamii Forums mobile app