CHADEMA leo wana nafasi ya kuweka historia ya kusimamia maadili ya chama kwa kuwafukuza Wanachama wake 19 kwa mpigo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,991
144,327
Ni imani yangu viongozi wa CHADEMA leo wataweka mbele heshima ya chama kwa kulinda katiba ya chama hicho pale watapowafukuza wasaliti 19 kwa mpigo na kuweka historia ya kufukuza Wanachama Waandamizi 19 kwa mpigo ili kulinda Katiba ya chama.

Hakika leo itakuwa ni siku ya historia kwa CHADEMA na pigo kwa watu wa chama fulani na mamluki wao pamoja na taasisi zote zilizohusika katika hujuma hii iwapo CHADEMA watafanya maamuzi hayo ya kuwafukuza wasaliti hawa katika kikao chao cha leo tarehe 27/11/2020.

Tarehe 27/11/2020, itakuwa ni siku ya kukumbukwa. Kazi kwenu CHADEMA.
 
Ni imani yangu viongozi wa CHADEMA leo wataweka mbele heshima ya chama kwa kulinda katiba ya chama hicho pale watapowafukuza wasaliti 19 kwa mpigo na kuweka historia ya kufukuza wanachama waandamizi 19 kwa mpigo ili kulinda katiba ya chama.

Hakika leo itakuwa ni siku ya historia kwa CHADEMA na pigo kwa watu wa chama fulani na mamluki wao na taasisi zote zilizohusika katika hujuma hii.

Kazi kwenu CHADEMA.

Kwamba leo ni washirika wa wale wanaojulikana wasiojulikana?

Kwamba si madhila ya Ben, Lissu au yeyote aliyeumia, kujeruhiwa, kufa au kupotezwa waliyo na kumbukumbu nayo?

Kwamba si wizi wa uchaguzi wala madhila ya wizi huo waliyo na kumbukumbu nayo?

Kuwa bado wanajitutumua na hata kujimwambafy kuwa wanapopanga haki?

Haki ipi wanayoipigania hawa ndani ya CDM?

Na waende huko wanakotakikana labda nao ni weupe!
 
Ni imani yangu viongozi wa CHADEMA leo wataweka mbele heshima ya chama kwa kulinda katiba ya chama hicho pale watapowafukuza wasaliti 19 kwa mpigo na kuweka historia ya kufukuza wanachama waandamizi 19 kwa mpigo ili kulinda katiba ya chama.

Hakika leo itakuwa ni siku ya historia kwa CHADEMA na pigo kwa watu wa chama fulani na mamluki wao pamoja na taasisi zote zilizohusika katika hujuma hii iwapo CHADEMA watafanya maamuzi hayo ya kuwafukuza wasaliti hawa leo hii.

Kazi kwenu CHADEMA.
Jiandae kisaikolojia bwashee.

Mzee Mtei ameagiza asifukuzwe mbunge yoyote kati ya hao 19!
 
Ah ah mnatapatapa sana....sasa mtamfukuza hadi mwenyekiti..maana ye ndo aliyesaini
 
Ni imani yangu viongozi wa CHADEMA leo wataweka mbele heshima ya chama kwa kulinda katiba ya chama hicho pale watapowafukuza wasaliti 19 kwa mpigo na kuweka historia ya kufukuza Wanachama Waandamizi 19 kwa mpigo ili kulinda Katiba ya chama...
Unafuruahisha jukwaa tu
 
CHADEMA kwa historia yake wakati wa matukio kama haya hawajawahi kuniangusha, naamini na leo wataendelea na msimamo wao wa kawaida.

Chama imara lazima kiwe na maamuzi imara siku zote.
 
Mtafukuza wangapi?
Msitazame mnapoangukia, tazameni mnapojikwaa!

Msijione Vichwa kwa kufukuza wanaowasaliti, jiulizeni kwanini mnasalitiwa? Kwanini Viongozi wenu wanathamini vyeo na fursa kuliko Itikadi? Mtakabiliana vipi na usaliti

Hao kina Catherine Magige kama Halima angewaweka kwny orodha ya 'covid 19' wasingechomoa sema baada ya kutoswa lazima waigize uzalendo

Kuna Mtu aliaminiwa kuwa kaiva kiitikadi Chadema kama Dr Slaa, lakin kiko wapi leo?

Hata Halima Mdee alikuwa akiwacheka na kuwakebehi sana wanaosaliti kama Mashinji lakin leo kiko wapi?

Msishangae Mnyika akiahidiwa Ubunge wa kuteuliwa na Rais nae akabwaga manyanga maana Kibamba alikimbia baada ya kuona hana nafasi sio kuwa alitosheka na Ubunge
 
HAFUKUZWI mtu. Mtarudi tu humu na U turn kutetea na kujustify maamuzi halali ya Chama
 
Then wewe unapata faida gani?
Watu wengine sijui uwa mnawaza kitu gani

Michango na mapambano ya Hao wadada kwa chadema unaijua?

Unajua mambo waliopitia Mpaka chama kimefika hapo?

Hata mkiwavua bado wanakuwa wabunge Sasa chama kinakuwa kimepata nn kama sio ujinga?
 
Back
Top Bottom