CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

Status
Not open for further replies.

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
HEHEEEE, CHADEMA KWAWAKA MOTO, KILA MTU ANA LAKE LA KUSEMA ! JISOMEEEE MWENYEWE !!

Kamati Kuu Chadema kujadili uteuzi wa Zitto
*Mbowe akatisha masomo kuhudhuria kikao
*Mtei asema maslahi ya taifa hayana chama
*Zitto asema hajitoi labda Rais amfukuze
*Mnyika: Mkono wa CCM umepenyezwa


Waandishi Wetu

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inakutana Jumamosi wiki hii kujadili pamoja na mambo mengine uteuzi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kwenye Kamati ya kupitia upya mikataba ya madini nchini.

Zitto ni miongoni mwa wajumbe 11 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupitia upya mikataba ya madini na Sheria za Madini kwa lengo la kuwanufaisha Watanzania.

Habari kutoka ndani ya Chadema zinasema kwamba kutokana na mjadala wa uteuzi wa Zitto kuibuka ndani ya chama hicho, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa kushirikiana na viongozi wa juu ameitisha Kamati Kuu ya dharura kujadili hali hiyo. Kwa sasa Mbowe yuko masomoni nchini Uingereza.

"Hali imekuwa ngumu, inaonekana kuna watu wameingiza mkono katika huu uteuzi wa Zitto, hivyo chama kimeamua kuitisha Kamati Kuu ya dharura kujadili suala hili. Kikao kitafanyika Jumamosi jijini Dar es Salaam," alisema kiongozi mmoja katika Makao Makuu ya chama hicho ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Mwananchi iliwasiliana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kujua ukweli wa kuwepo kwa mkutano wa Kamati Kuu, ambaye akiri na kusema kuwa wameamua (viongozi) kuitisha mkutano wa dharura kutokana na kujitokeza kwa kauli tofauti kutoka kwa baadhi ya wananchama na viongozi kuhusiana na uteuzi huo wa Zitto kwenye kamati ya madini .

"Ni kweli tumeamua kuitisha Kikao cha Kamati Kuu ambacho kina maamuzi katika chama, ili kujadili kauli hizo za viongozi wa chama ambazo zimejitokeza sasa. Chadema haizui watu kuwa na mawazo tofauti, lakini lengo la kikao cha Jumamosi ni kutoa tamko la chama kuhusiana na suala hilo," alisema.

Alisema katika kikao cha Jumamosi, Chadema itatoa msimamo wa chama kuhusiana na Kamati ya Madini iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete na uteuzi wa Zitto katika Kamati hiyo ya kupitia mikataba ya madini.

Wakati Kamati Kuu ya Chadema ikipanga kukutana, Zitto amesema hawezi kujitoa katika kamati hiyo kama baadhi ya watu wanavyoshauri kwa kuwa suala la kupitia upya mikataba hiyo, limo katika sera za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambayo yeye ni mwanachama wake.

Sera ya Chadema ya madini, pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa: "Mikataba yote ya uchimbaji madini, itapitiwa upya na kuwekwa wazi kwa wananchi na kwamba kuanzia asilimia thelathini ya mapato yatokanayo na madini yatabaki nchini".

Akizungumza na Mwananchi jana, Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema alisema kutokana na sera hiyo ya chama chake, anaamini kuwa madini ni moja ya rasilimali zinazowanufaisha Watanzania kiuchumi kwa hiyo amejiandaa vema kutekeleza majukumu yake kwenye kamati kwa niaba ya chama chake na Watanzania, hivyo hawezi kujitoa kwenye kamati hiyo, labda Rais Kikwete amfukuze.

"Sitajitoa kwenye kamati, kwa kuwa kupitia mikataba ya madini ni sera ya Chadema, CCM (Chama Cha Mapinduzi) hawana sera ya aina hii. Hivyo, nitaendelea kushikilia msimamo huo labda rais anifukuze," alisema Zitto.

Alisema hayuko tayari kuipoteza fursa aliyoipata kwa kuwa hafahamu namna wananchi watakavyopokea iwapo ataamua kujitoa katika kamati hiyo, kama baadhi ya watu wanavyoshauri.

Akitoa maoni yake Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei alisema anaunga mkono uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo kwa kuwa ana sifa na pia tatizo la madini linapaswa kushughulikiwa na kila Mtanzania.

"Hata Chadema walimteua Zitto kuwa Naibu Katibu Mkuu kwa sababu ya misimamo yake na pia inapofika suala la madini, Mtanzania yeyote anatakiwa kuchangia," alisema Mtei.

Hata hivyo, Mtei alisema watu kuwa na mitazamo tofauti katika mambo ni jambo la kawaida, lakini linapojitokeza suala linalogusa maslahi ya taifa, wazalendo wa kweli wanatakiwa kuunga mkono na si kupinga.

"Watu wote wanatakiwa waunge mkono, sababu suala la madini ni rasilimali za nchi ambayo inawanufaisha Watanzania. Kazi ya upinzani si kupinga tu. Hivyo, sioni sababu yoyote ya Zitto kujitoa kwenye kamati," alisema Mtei.

Naye Mkurugenzi wa Vijana wa Chadema, John Mnyika alisema ana mashaka kwamba baadhi ya watu kutoka CCM wameshaanza kutumia hali ya sasa ya viongozi kuwa na kauli za kutofautiana kufanya propaganda kuwa kuna mgogoro ndani ya Chadema na kwamba chama hicho kinatanguliza maslahi ya kisiasa ya upinzani badala ya maslahi ya Taifa.

Wakati huo huo, UMOJA wa Vijana wa CCM umesema kuwa umeshangazwa na kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema Dk Wilibroad Slaa kuwa chama hicho hakina imani na kamati ya kupitia upya mikataba ya madini iliyoteuliwa na Rais Kikwete hivi karibuni.

Akitoa taarifa jana Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo Amos Makalla, alisema kauli hiyo inashangaza na akamtaka kiongozi huyo atulie na aiachie kamati hiyo ifanye kazi zake kwa uhuru.

Hata hivyo, wakati Zitto na Mtei wakisema hayo, Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Victor Kimesera alisema jana kuwa chama chake kinaitaka serikali iwe imezipatia ufumbuzi hoja za chama hicho za kupinga kuundwa kwa kamati hiyo ifikapo Novemba 25, mwaka huu.

Kimesera ambaye alizungumza na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana alisema, Chadema inapinga kamati hiyo kwa kuwa wajumbe wake wengi wanatoka kwenye chama kimoja (CCM).

Alisema hali hiyo inainyima kamati hiyo uhalali wa kisheria kudai nyaraka au chochote kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake.

"Bunge ndilo lililopaswa kuunda kamati hiyo kwa kuwa ingepata nguvu ya kisheria. Hizo ni' blabla' tu na Zitto atajikuta ameingizwa kwenye kitu ambacho hakitazaa matunda," alisema Kimesera.

Hata hivyo, alisema tangu kuundwa kwa kamati hiyo, hakuna lolote lililobadilika katika chama na kwamba, umoja na mshikamano ndani ya chama bado upo kinyume na inavyotangazwa na baadhi ya watu.

Alisema wanachokikataa wao na ambacho kinaonekana kuwa ni mgogoro ni chama kuendeshwa na fikra za mtu mmoja.

"Kila mtu afikiri anavyoona na ni haki yake, lakini tunachokikataa ni ile dhana ya 'zidumu fikra za mtu mmoja'," alisema Kimesera.

Kamati hiyo yenye wajumbe 11, iliundwa na Rais Jakaya Kikwete wiki iliyopita na iko chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Jaji Mark Bomani.

Tangu Rais Kikwete aunde kamati hiyo na kumteua Zitto kuwa mmoja wa wajumbe wake (kamati hiyo), baadhi ya watu, wakiwamo wafuasi wa chama hicho wakiongozwa na Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe, wamekuwa wakipinga uteuzi huo wa Zitto kwa madai kwamba, unadhoofisha hoja za wapinzani na kujenga usaliti baina yao kuhusiana na suala la madini nchini.

Novemba 13, Mwaka huu Rais Kikwete alitangaza kuundwa kwa Kamati ya kupitia mikataba na sheria za madini na kuwateua wajumbe wa kamati hiyo iliyojumuisha wajumbe kutoka kambi ya upinzani akiwemo Zitto wa Chadema.

Mbali na Zitto, wengine wanaunda Kamati hiyo, ni Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo, Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Wajumbe wengine, ni Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, Price Water Coopers, David Tarimo ambaye ni mtaalamu wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.


Imeandaliwa na Muhibu Said, Elizabeth Suleyman na Salim Said wa MUM
 
Last edited by a moderator:
haya sasa, utamu upo hapa ! bwa mdogo mnyika na uswahili wake anasema kuna mkono wa serikali (ana-apply hii theory yake katika kila kitu) wakati bwana zitto anasema hatoki humo unless rais amfukuze (which wont happen) ! mtei kaonekana hajabase kwenye chama bali maslahi ya taifa !

weweee, utamu upo hapa !!

napenda sana kunukuu haya maneno ya bwana zitto !
"Sitajitoa kwenye kamati, kwa kuwa kupitia mikataba ya madini ni sera ya Chadema, CCM (Chama Cha Mapinduzi) hawana sera ya aina hii. Hivyo, nitaendelea kushikilia msimamo huo labda rais anifukuze
 
Kukomaa kwa chama sio kutokuwa na migongano ya mawazo bali kuwa na njia za kuhakikisha migongano hiyo ya mawazo haigeuki kuwa migogoro.

Nawatakia mkutano mwema CHADEMA; watu hata kwenye familia hutofautiana ndio iwe kwenye siasa? Waangalie tu wasianze kufukuzana.
 
Kukomaa kwa chama sio kutokuwa na migongano ya mawazo bali kuwa na njia za kuhakikisha migongano hiyo ya mawazo haigeuki kuwa migogoro.

Nawatakia mkutano mwema CHADEMA; watu hata kwenye familia hutofautiana ndio iwe kwenye siasa? Waangalie tu wasianze kufukuzana.


That is, you said it all. Thanks
 
Kukomaa kwa chama sio kutokuwa na migongano ya mawazo bali kuwa na njia za kuhakikisha migongano hiyo ya mawazo haigeuki kuwa migogoro.

Nawatakia mkutano mwema CHADEMA; watu hata kwenye familia hutofautiana ndio iwe kwenye siasa? Waangalie tu wasianze kufukuzana.

maneno mazuri hayo ! lakini kila mtu ndani ya chadema anajifanya kichwa ngumu ukizingatia master wao aliyewaacha kondoo wa chama chake yupo masomoni, basi hao walioachwa huko wanapelekesha tu mambo wanavyoweza wao ! mara mnyika anasema hivi, slaa anasema vile, mtei yupo upande huu, zitto upande ule yaaani taabu tupu !

komaa zitto na usitoke kwenye hiyo kamati bana, hata wakisema wewe sio mtalaam kwani katika kila sector kuna watalaam ? jibu ni hapana. wee baki huko huko kwenye kamati mzee.
 
Tatizo liko wapi... Zito ameteuliwa na Rais wa Serikali ya Tanzania kuwa mjumbe wa hii kamati inayoshughulikia rasilimali za taifa; tusisahau pia, licha ya kusimamishwa, Zitto ni Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa ishu za kitaifa. Kama kuna sababu za yeye kujitoa kwenye hii kamati basi kwa sababu hizohizo ajitoe kwenye ubunge na kwa vigezo hivohivo wabunge wa upinzania wote ni haramu kuwa wabunge.
Kujitoa kwenye kamati itakuwa ni dalili ya uoga na umbumbu wa kisiasa
Tuamini kuwa Jk ana imani na uwezo wa Zitto katika kupambanua ishu. Inaweza kuwa ni dalili njema kuwa rais analo sikio la kusikia sauti za upinzani hata kama hatuna uhakika kama anafanyia kazi sauti hizi. Au mnataka hata ikulu ibinafsishwe iwe na bendera ya jembe na nyundo!
 
Tatizo liko wapi... Zito ameteuliwa na Rais wa Serikali ya Tanzania kuwa mjumbe wa hii kamati inayoshughulikia rasilimali za taifa; tusisahau pia, licha ya kusimamishwa, Zitto ni Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa ishu za kitaifa. Kama kuna sababu za yeye kujitoa kwenye hii kamati basi kwa sababu hizohizo ajitoe kwenye ubunge na kwa vigezo hivohivo wabunge wa upinzania wote ni haramu kuwa wabunge.
Kujitoa kwenye kamati itakuwa ni dalili ya uoga na umbumbu wa kisiasa.
Tuamini kuwa Jk ana imani na uwezo wa Zitto katika kupambanua ishu. Na pia ni dalili njema kuwa rais analo sikio la kusikia sauti za upinzani. Au mnataka hata ikulu ibinafsishwe iwe na bendera ya jembe na nyundo! Hakuna kujitoa mtu kwenye kamati.

lakini akili za wanachama wa CHADEMA tawi la JF, halitaki zitto awepo kwenye kamati na ndio maana hadi yule dogo mswahili mnyika anasema kuna mkono wa serikali ( yaani mwenyewe anapenda kweli kusema hivi hadi inakera ) sasa wewe unadhani mtu kama mnyika anayeleta hisia zake za kiswahili kwa kusema kuna mkono wa serikali katika kila jambo kweli ndio tutaendelea iwapo tutasema tunahitaji vijana wa vizazi vipya kutuletea maendeleo na mawazo yao yenyewe BOGUS kabisa ??
uzuri ni kwamba ndani ya chadema kama ilivyo kwenye vyama vingine ni kwamba kila mtu has a say, lakini mbaya kwao wao ni kwamba kila mmoja anajiona ni top ! msikie mnyika anavyosema, slaa anavyosema, mtei anavyosema utajua hawa watu wa chipukizi kweli na wanahitaji msaada !

ZITTO kaza buti babu, maana wachawi ni hao hao waliomo ndani ya chadema, mara walizusha sijui ulitaka kuuliwa, binafsi ukaja kukanusha na kusema yaliyo moyoni mwako, halafu watu hao hao leo wanasema utoke kwenye kamati, je wanakutakia mema hawa watu kweli ??
 
Source ya hii story ingawa aliyebandika hapa hajaiweka ila inaonekana kabisa ni gazeti la majira au moja ya magazeti ya Rostam Aziz. This guy kwake kila kitu ni kupigana na kupondea.

Chadema ambao sio kama wabunge wa ccm ambao wanakalishwa chini na Lowasa na kuambiwa cha kufanya, wao wanajadiliana na kutofautiana.

Poor Rostam, umechemsha tena katika hili kujaribu kuzua kitu out of nothing na kuacha makada wako waki-hang!
 
Source ya hii story ingawa aliyebandika hapa hajaiweka ila inaonekana kabisa ni gazeti la majira au moja ya magazeti ya Rostam Aziz. This guy kwake kila kitu ni kupigana na kupondea.

Chadema ambao sio kama wabunge wa ccm ambao wanakalishwa chini na Lowasa na kuambiwa cha kufanya, wao wanajadiliana na kutofautiana.

Poor Rostam, umechemsha tena katika hili kujaribu kuzua kitu out of nothing na kuacha makada wako waki-hang!

uzuri ni kwamba, zitto ni member wa JF hivyo sitoshangaa siku yoyote akija kusema kwamba ni kweli amesema hatotoka kwenye hiyo kamati kama pale alipokanusha mliposema alitaka kuuliwa !

je hayo madai ya kutaka kuuliwa kwa zitto mliyoanzisha wewe na mwanakijiji na habari hii ambayo ni ya UKWELI unataka kusema watu wanaospin habari ni nani ?? DEFINITELY YOU PEOPLE !!

endelea kuspin, cuz you live for that !
 
uzuri ni kwamba, zitto ni member wa JF hivyo sitoshangaa siku yoyote akija kusema kwamba ni kweli amesema hatotoka kwenye hiyo kamati kama pale alipokanusha mliposema alitaka kuuliwa !

je hayo madai ya kutaka kuuliwa kwa zitto mliyoanzisha wewe na mwanakijiji na habari hii ambayo ni ya UKWELI unataka kusema watu wanaospin habari ni nani ?? DEFINITELY YOU PEOPLE !!

endelea kuspin, cuz you live for that !

Kada,

Mimi ni free spirit na sio kwamba nafikiria kile viongozi au mtu yeyote anafikiria. Kama mimi nikifikiria kuwa Zitto hatakiwi kuwa katika hiyo kamati, hiyo haimfanyi zitto afikirie kama mimi.

Hii ndio tofauti hapa na ccm. Kinachoamriwa na Lowasa na Rostam Aziz ndicho wanaccm wote wanatakiwa kufuata. Hakuna mtu anaweza kufikiria tofauti. Zitto akiamua kuwa katika hiyo kamati huu ni uamuzi wake NA KAMA NILIVYOAHIDI HAPA SIKU ILE NI KUWA ZITTO ASITEGEMEE KABISA IZE RIDE. AKIKOSEA AU AKIFANYA YASIYO ATAPEWA DOZI LIKE EVERY BODY ELSE.

Nje ya ccm kuna demokrasia ambayo wanaccm huko ndani hamuipati kwa hiyo sikushangai ukizani kuwa ni big deal sana CHADEMA kuwa na mitizamo tofauti.
 
By The Way,

Bado naamini kuwa kuna something fishy kwenye ajali ya mama mbatia. na kwa sababu mimi ni independent and free spirit basi nina hakika kuwa sitakuwa nafikiria kile ambacho zitto anafikiria
 
Kada,

Mimi ni free spirit na sio kwamba nafikiria kile viongozi au mtu yeyote anafikiria. Kama mimi nikifikiria kuwa Zitto hatakiwi kuwa katika hiyo kamati, hiyo haimfanyi zitto afikirie kama mimi.

Hii ndio tofauti hapa na ccm. Kinachoamriwa na Lowasa na Rostam Aziz ndicho wanaccm wote wanatakiwa kufuata. Hakuna mtu anaweza kufikiria tofauti. Zitto akiamua kuwa katika hiyo kamati huu ni uamuzi wake NA KAMA NILIVYOAHIDI HAPA SIKU ILE NI KUWA ZITTO ASITEGEMEE KABISA IZE RIDE. AKIKOSEA AU AKIFANYA YASIYO ATAPEWA DOZI LIKE EVERY BODY ELSE.

Nje ya ccm kuna demokrasia ambayo wanaccm huko ndani hamuipati kwa hiyo sikushangai ukizani kuwa ni big deal sana CHADEMA kuwa na mitizamo tofauti.

Mwafrika wa Kike,
kwanza pongezi sana kwa ku-act mature kidogo tofauti na post nyingine ambazo kwa kweli utoto ulikuwa umeuweka mbele sana na ilikuwa too much !IWAPO UTAENDELEA KUWA HIVYO BASI FORUM ITAKUWA ON ANOTHER LEVEL IT HAS NEVER BEEN ON BEFORE, TRUST ME! so congratulations on that !

secondly, mwngi uliyosema humo sio kweli na ni maneno ambayo hayana ukweli, unaposema EL na RA wakiongea ndio wanaccm wafuate una maana gani ? inawezekana wakawa wanalazimisha watu wafanye wanayotaka wao lakini not that i know of, which makes it easy for me to know kwamba haupo ndani ya kamati ya ccm kujua nini kinachoendelea huko, sasa hayo maneno umeyatoa wapi ?
unaposema EL, RA wakisema kitu kinafuatwa napenda kurudia tena kwamba hilo suala sio la ukweli, ukitaka kujua ni kwamba, angalia katika upigaji kura, kama EL angekuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya mkoa au wilaya, ungemuona jinsi angekuwa anachakarika kuomba kura kama akina kapuya na wengineo na kama kweli angekuwa na nguvu kiasi hicho, basi nadhani tokea '95 lowassa angekuwa tishio hadi hivi sasa !

lakini nyie mshamzoea lowassa yule wa kwenye habari, the exaggerated lowassa anayemjua mwanakijiji !!
 
Mwafrika wa Kike,
kwanza pongezi sana kwa ku-act mature kidogo tofauti na post nyingine ambazo kwa kweli utoto ulikuwa umeuweka mbele sana na ilikuwa too much !IWAPO UTAENDELEA KUWA HIVYO BASI FORUM ITAKUWA ON ANOTHER LEVEL IT HAS NEVER BEEN ON BEFORE, TRUST ME! so congratulations on that !

secondly, mwngi uliyosema humo sio kweli na ni maneno ambayo hayana ukweli, unaposema EL na RA wakiongea ndio wanaccm wafuate una maana gani ? inawezekana wakawa wanalazimisha watu wafanye wanayotaka wao lakini not that i know of, which makes it easy for me to know kwamba haupo ndani ya kamati ya ccm kujua nini kinachoendelea huko, sasa hayo maneno umeyatoa wapi ?
unaposema EL, RA wakisema kitu kinafuatwa napenda kurudia tena kwamba hilo suala sio la ukweli, ukitaka kujua ni kwamba, angalia katika upigaji kura, kama EL angekuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya mkoa au wilaya, ungemuona jinsi angekuwa anachakarika kuomba kura kama akina kapuya na wengineo na kama kweli angekuwa na nguvu kiasi hicho, basi nadhani tokea '95 lowassa angekuwa tishio hadi hivi sasa !

lakini nyie mshamzoea lowassa yule wa kwenye habari, the exaggerated lowassa anayemjua mwanakijiji !!

Ukitaka kuniita mtoto au chochote unaweza tu ila ukiangalia sana inawezekana hata wewe unafanya exactly hicho unachokiita utoto kwa upande wangu.

Nguvu ya Lowasa kwenye vikao vya wabunge wanaccm cha kuamua nini kipigiwe kura na nini kiachwe imethibitishwa mara nyingi sana hapa.

Otherwise, unakarabishwa kwenye free world ambayo unaweza pia kutofautiana na viongozi wako wa chama!
 
uzuri ni kwamba, zitto ni member wa JF hivyo sitoshangaa siku yoyote akija kusema kwamba ni kweli amesema hatotoka kwenye hiyo kamati kama pale alipokanusha mliposema alitaka kuuliwa !

je hayo madai ya kutaka kuuliwa kwa zitto mliyoanzisha wewe na mwanakijiji na habari hii ambayo ni ya UKWELI unataka kusema watu wanaospin habari ni nani ?? DEFINITELY YOU PEOPLE !!

endelea kuspin, cuz you live for that !

Kada acha kunichulia nilikuambi nenda kaangalie mada yako uliyoanzisha kuhusu kumuuliza Zitto na utaona jibu langu lilikuwa nini. Una wiki karibu mbili hujaweza kufanya hivyo. Ila unazidi kurudia uongo ule ule. Hakuna mahali hata pamoja ambapo nilidai au kuashiria kudai kuwa ajali ya Mbatia ilikuwa imemlenga Zitto. Period.
 
Ukitaka kuniita mtoto au chochote unaweza tu ila ukiangalia sana inawezekana hata wewe unafanya exactly hicho unachokiita utoto kwa upande wangu.

Nguvu ya Lowasa kwenye vikao vya wabunge wanaccm cha kuamua nini kipigiwe kura na nini kiachwe imethibitishwa mara nyingi sana hapa.

Otherwise, unakarabishwa kwenye free world ambayo unaweza pia kutofautiana na viongozi wako wa chama!

BOGUS !!!!!!!!!!!!! ushaanza kulitia maji ....
 
Kada acha kunichulia nilikuambi nenda kaangalie mada yako uliyoanzisha kuhusu kumuuliza Zitto na utaona jibu langu lilikuwa nini. Una wiki karibu mbili hujaweza kufanya hivyo. Ila unazidi kurudia uongo ule ule. Hakuna mahali hata pamoja ambapo nilidai au kuashiria kudai kuwa ajali ya Mbatia ilikuwa imemlenga Zitto. Period.

pick a show boy, MAURY, JERRY SPRINGER or esle ..... ukawaambie huko kwamba zitto alilengwa kwenye ajali na ccm, wakati mwenyewe kakanusha KULIKO. binafsi hapa JF am not ready to hear that nonsense ! zitto alishakanusha ! wewe unang'ang'ania tu kama ulikuwepo, au mganga gani alikwambia hayo unayosema ??
 
By The Way,

Bado naamini kuwa kuna something fishy kwenye ajali ya mama mbatia. na kwa sababu mimi ni independent and free spirit basi nina hakika kuwa sitakuwa nafikiria kile ambacho zitto anafikiria

ahhh, kumbe haya ni mawazo yako nilifikiri unasema FACTS, hahahaaaaaa !! endelea na mawazo uchwara hayo ! pick a show ukawaeleze watu spirits zako, maybe DR.PHIL !!
 
Mwafrika wa Kike,
kwanza pongezi sana kwa ku-act mature kidogo tofauti na post nyingine ambazo kwa kweli utoto ulikuwa umeuweka mbele sana na ilikuwa too much !IWAPO UTAENDELEA KUWA HIVYO BASI FORUM ITAKUWA ON ANOTHER LEVEL IT HAS NEVER BEEN ON BEFORE, TRUST ME! so congratulations on that !

secondly, mwngi uliyosema humo sio kweli na ni maneno ambayo hayana ukweli, unaposema EL na RA wakiongea ndio wanaccm wafuate una maana gani ? inawezekana wakawa wanalazimisha watu wafanye wanayotaka wao lakini not that i know of, which makes it easy for me to know kwamba haupo ndani ya kamati ya ccm kujua nini kinachoendelea huko, sasa hayo maneno umeyatoa wapi ?
unaposema EL, RA wakisema kitu kinafuatwa napenda kurudia tena kwamba hilo suala sio la ukweli, ukitaka kujua ni kwamba, angalia katika upigaji kura, kama EL angekuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya mkoa au wilaya, ungemuona jinsi angekuwa anachakarika kuomba kura kama akina kapuya na wengineo na kama kweli angekuwa na nguvu kiasi hicho, basi nadhani tokea '95 lowassa angekuwa tishio hadi hivi sasa !

lakini nyie mshamzoea lowassa yule wa kwenye habari, the exaggerated lowassa anayemjua mwanakijiji !!

wala siyo mimi tu na watu wengi wanaomfahamu... kwani ni mimi niliyeanzisha msemo wa "richmonduli"?
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom