VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Kujaza makada mashuhuri na waandamizi wa CCM jijini Arusha ni mbinu za kisiasa. Hii itazifanya sehemu nyinginezo ambazo nazo zitafanya uchaguzi Jumapili ya tarehe 16/6/2013 kutokufatiliwa na hivyo kusahaulika. Iko wazi kuwa mpambano wa Arusha ni wa kupigiwa mfano. Ni mpambano wa kisiasa kweli!
Huu utakuwa ni mwanya kwa chama chetu,CCM, kujitwalia ushindi kwenye kata zisizo Arusha kama 'kumsukuma mlevi' vile. CHADEMA lazima iwe makini na mbinu hii. Isijisahau kwingineko. Ipambane kila Kata ya kila mkoa. Nina uhakika mnaweza kuleta ushindani popote.Napenda siasa za ushindani.Siasa huleta maendeleo.Ndiyo maana natoa angalizo hili.
Kila la kheri CCM,CHADEMA,CUF,TLP,NCCR-Mageuzi na wengineo katika uchaguzi wa Jumapili!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
Huu utakuwa ni mwanya kwa chama chetu,CCM, kujitwalia ushindi kwenye kata zisizo Arusha kama 'kumsukuma mlevi' vile. CHADEMA lazima iwe makini na mbinu hii. Isijisahau kwingineko. Ipambane kila Kata ya kila mkoa. Nina uhakika mnaweza kuleta ushindani popote.Napenda siasa za ushindani.Siasa huleta maendeleo.Ndiyo maana natoa angalizo hili.
Kila la kheri CCM,CHADEMA,CUF,TLP,NCCR-Mageuzi na wengineo katika uchaguzi wa Jumapili!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.