Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Wadau wa JF nawasalimu na habari za siku kadhaa.
Nimekuwa busy kidogo tunapoelekea mwisho wa mwaka lakini harakati za kukijenga chama chetu pendwa, tumaini la watanzania zinaendelea kama kawaida kadri nafasi inavyopatikana.
Kesho tunatarajia kuwa na mkutano wa hadhara katika mtaa wa Mongolandege Kata ya Ukonga kuanzia saa nane kamili mchana (8:00).
Agenda kuu ya mkutano huo itakuwa ni kuwafahamisha wananchi wa Ukonga juu ya ufisadi mkubwa sana uliofanywa na wenyeviti wa serikali za mitaa ya Mongolandege na Mazizini, ambapo wote wawili wanatuhumiwa kuuza maeneo ya wazi yanayomilikiwa na serikali za mitaa husika.
Uuuzwaji wa eneo la serikali ya mtaa wa Mongolandege uliwahusisha Mwenyekiti wa mtaa(ccm), wajumbe watano wa serikali ya mtaa(ccm)na mtendaji wa serikali ya mtaa. Hadi wakati huu tulipoitisha mkutano wa hadhara tumeshazitia mkononi documents zote zinazoonyesha uuzwaji wa kiwanja hicho na aliyeuziw ameshajenga nyumba ya kuishi. Mwenyekiti wa mtaa tayari ameshajiuzulu baada ya kashfa hiyo lakini wajumbe wamegoma kujiuulu na wanalindwa na Mkuu wa wilaya ya Ilala akimtumia katibu tarafa.
Katika mtaa wa Mazizini napo mwenyekiti wa mtaa(ccm) ameuza eneo la kiwanja cha ofisi ya serikali ya mtaa na wananchi wamekwisha mkataa japokuwa ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ilala kupitia kwa katibu tarafa anaendelea kumlinda, kama anavyowalinda wajumbe watano wa mongolandege.
Wadau wote wa maeneo ya jirani na Ukonga mnakaribishwa sana katika mkutano huo ambapo mgeni rasmi atakuwa mwenyekiti wa Vijana Chadema Taifa kamanda John Heche Suguta.
NB:
Diwani wa kata ya Gongolamboto ambaye pia ni meya wa manispaa ya Ilala akae mkao wa kulia kwakuwa baada ya hawa wenyeviti wa mitaa ni zamu yake, tunamalizia ku compile mafaili ya ufisadi wake katika manispaa ya Ilala, hasa kuhusiana na ardhi.
Wasalaaam Mwita Maranya, nimerudi tena kuwashika.
Nimekuwa busy kidogo tunapoelekea mwisho wa mwaka lakini harakati za kukijenga chama chetu pendwa, tumaini la watanzania zinaendelea kama kawaida kadri nafasi inavyopatikana.
Kesho tunatarajia kuwa na mkutano wa hadhara katika mtaa wa Mongolandege Kata ya Ukonga kuanzia saa nane kamili mchana (8:00).
Agenda kuu ya mkutano huo itakuwa ni kuwafahamisha wananchi wa Ukonga juu ya ufisadi mkubwa sana uliofanywa na wenyeviti wa serikali za mitaa ya Mongolandege na Mazizini, ambapo wote wawili wanatuhumiwa kuuza maeneo ya wazi yanayomilikiwa na serikali za mitaa husika.
Uuuzwaji wa eneo la serikali ya mtaa wa Mongolandege uliwahusisha Mwenyekiti wa mtaa(ccm), wajumbe watano wa serikali ya mtaa(ccm)na mtendaji wa serikali ya mtaa. Hadi wakati huu tulipoitisha mkutano wa hadhara tumeshazitia mkononi documents zote zinazoonyesha uuzwaji wa kiwanja hicho na aliyeuziw ameshajenga nyumba ya kuishi. Mwenyekiti wa mtaa tayari ameshajiuzulu baada ya kashfa hiyo lakini wajumbe wamegoma kujiuulu na wanalindwa na Mkuu wa wilaya ya Ilala akimtumia katibu tarafa.
Katika mtaa wa Mazizini napo mwenyekiti wa mtaa(ccm) ameuza eneo la kiwanja cha ofisi ya serikali ya mtaa na wananchi wamekwisha mkataa japokuwa ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ilala kupitia kwa katibu tarafa anaendelea kumlinda, kama anavyowalinda wajumbe watano wa mongolandege.
Wadau wote wa maeneo ya jirani na Ukonga mnakaribishwa sana katika mkutano huo ambapo mgeni rasmi atakuwa mwenyekiti wa Vijana Chadema Taifa kamanda John Heche Suguta.
NB:
Diwani wa kata ya Gongolamboto ambaye pia ni meya wa manispaa ya Ilala akae mkao wa kulia kwakuwa baada ya hawa wenyeviti wa mitaa ni zamu yake, tunamalizia ku compile mafaili ya ufisadi wake katika manispaa ya Ilala, hasa kuhusiana na ardhi.
Wasalaaam Mwita Maranya, nimerudi tena kuwashika.