Uchaguzi 2020 CHADEMA kutobandika picha za Tundu Lissu ni kosa la kiufundi

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,211
22,266
Leo tena natumia haki yangu ya kikatiba kutoa maoni kuhusu uchaguzi huu. Hii pia imechangiwa na wengi wenu kunitumia PM kuniomba nitoe maoni yangu kuhusu mwenendo wa uchaguzi huu. Nimekubali kufanyia kazi maombi ya wengi.

Niseme kwamba kampeni hizi za mwaka huu ni za kipekee. Ziko tofauti sana. Wapiga kura wengi kwa sasa wana akili nyingi sana na hawasikilizi blah blah. Ilishazoeleka wagombea kutamka uongo ulio wazi na ahadi nyingi hewa ila kwa mwaka huu inaonekana kabla mgombea hajatamka kitu inabidi ajifikirie mara nyingi sana. Watu wanataka maelezo ya kina. Kwahiyo hakuna Chama chenye wakati mrahisi tunapoiendea tar 28 Octoba.

CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kimeonyesha kuleta changamoto kwenye uchaguzi huu hasa baada ya kupata mgombea jasiri na ambaye inaonekana wazi hakuna anachohofia. Chama hicho kina mtaji mkubwa wa kura za huruma kutoka kwa watu wanaoamini kuwa Lisu alitendewa ubaya na CCM. Bahati nyingine ya hivi karibuni ambayo inaweza kuwaongezea kura za huruma ni hiki kitendo cha NEC kumsimamisha Lisu kufanya kampeni kwa siku 7. Tukiachana na kura za huruma ni wazi CHADEMA watapata kura chache kutoka makundi mengine ya wananchi.

Kosa la kiufundi ambalo CHADEMA wamelifanya na litawagharimu kwenye sanduku la kura tar 28 ni kutobandika picha za mgombea wao kama walivyofanya vyama vingine. Ikumbukwe Lissu amekaa nje ya nchi kwa miaka kadhaa na alikuwa adimu machoni mwa wapiga kura. Au chama kimesahau kwenye karatasi ya kupigia kura kuna picha za wagombea? Mabango kwa watu wa marketing watakubaliana nami ni nyenzo kubwa sana kwenye kuitangaza bidhaa. Mtu asiyejua kusoma itamsaidia sana kwenye kupiga kura. Watu kama wahadzabe mngekuwa mmewarahisishia sana.

Mimi nionavyo ndani ya CHADEMA kuna ambao kwa makusudi waliamua kumhujumu Lisu kwa kutoweka mabango. Au pia watu hao wameona tu Rais Magufuli anatosha kwahiyo wamsaidie kinamna. Ombi langu kwa Rais JPM asimsahau Mh Tundu Lissu kwenye teuzi za serikali yake ijayo.
 
Uelewa wako ni mdogo hakuna anayetaka kumhujumu Lissu ndani ya CDM ya kweli inajulikana hali ya kifedha mbaya hata Lissu alisema hilo.

Mabango hayasaidii kitu hasa siku hizi za mitandao na media nyingi. Pamoja na mabango kona zote magufuli anapiga magoti kuomba kura ni ajabu!
 
Uelewa wako ni mdogo hakuna anayetaka kumhujumu Lissu ndani ya CDM ya kweli inajulikana hali ya kifedha mbaya hata Lissu alisema hilo.

Mabango hayasaidii kitu hasa siku hizi za mitandao na media nyingi. Pamoja na mabango kona zote magufuli anapiga magoti kuomba kura ni ajabu!
Ukata umesababishwa na nini? Jibu ni matumizi mabaya ya ruzuku na michango ya wanachama hasa wabunge.
 
Uelewa wako ni mdogo hakuna anayetaka kumhujumu Lissu ndani ya CDM ya kweli inajulikana hali ya kifedha mbaya hata Lissu alisema hilo.

Mabango hayasaidii kitu hasa siku hizi za mitandao na media nyingi. Pamoja na mabango kona zote magufuli anapiga magoti kuomba kura ni ajabu!
Anavuna matunda ya kazi aliyoifanya.
 
Ngoja nimueleweshe mleta mada hapa.
Kwanza Sio kweli kuwa Lissu hana mabango au CHADEMA hawajatengeneza mabango, mabango yapo lakini yanaonekana kwa uchache kwa sababu zifuatazo:

(i)Gharama za kutengeneza mabango ni kubwa sana, kiasi ambacho Chama hakiwezi kugharamia mabango mengi kama walivyo CCM. Ikitokea CADEMA kikisaidiwa na watu/wafanyabiashara wasiotaka kujulikana wazi ili kutengeneza mabango, Chama kitaambiwa kinatumika kinatakatisha Pesa. (Kumbuka kisa cha msaidizi wa Membe kilichompata)

(ii)Kwa sasa (katika uchaguzi huu wa 2020) Kuchapisha na kubandika bango sehemu rasmi unapaswa kulipia kodi. Ukijaribu kufanya kienyeji, utaambiwa unakwepa kodi, hivyo chama kipo mtegoni. (Kumbuka kisa cha Kubenea kukamatwa akitokea Kenya).

(iii)Uchunguzi uliofanyika katika mikoa mingi ambapo mabango ya Lissu yalibandikwa, ndani ya masaa 24 tu toka yabandikwe zaidi ya 80% yalikutwa yamechanwa au kung'olewa huku ikielezwa zoezi hilo kufanywa na vijana wa CCM chini ya usimamizi wa jeshi la Polisi.

(iv)CCM imesambaza mabango ya Magufuli kila kona ya nchi (mpaka kwenye vyoo vya bar, stendi na guest house) kwa sababu wanazo means zote (pesa, serikali, mamlaka), hivyo uwepo wa mabango ya Lissu na CHADEMA itabidi yawe sambamba katika mwelekeo huo huo ili kuonekana, Otherwise mabango ya Lissu na CHADEMA hayataonekana.
 
Uelewa wako ni mdogo hakuna anayetaka kumhujumu Lissu ndani ya CDM ya kweli inajulikana hali ya kifedha mbaya hata Lissu alisema hilo.

Mabango hayasaidii kitu hasa siku hizi za mitandao na media nyingi. Pamoja na mabango kona zote magufuli anapiga magoti kuomba kura ni ajabu!
Hali ya kifedha mbaya?. Zimeenda wapi ruzuku, na michango ya wadau?. Chama saccos kimejaa ubadhilifu wa kutisha, huku mwenyekiti wenu akichekacheka tu. Watanzania wanawatazama mnavyojikanyaga.
 
Hali ya kifedha mbaya?. Zimeenda wapi ruzuku, na michango ya wadau?. Chama saccos kimejaa ubadhilifu wa kutisha, huku mwenyekiti wenu akichekacheka tu. Watanzania wanawatazama mnavyojikanyaga.
Zimeenda wapi trilion 1.5 walizotoa wahisani kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la Bukoba? CCM mmezipeleka wapi? Magu amezipeleka wapi?
 
Leo tena natumia haki yangu ya kikatiba kutoa maoni kuhusu uchaguzi huu. Hii pia imechangiwa na wengi wenu kunitumia PM kuniomba nitoe maoni yangu kuhusu mwenendo wa uchaguzi huu. Nimekubali kufanyia kazi maombi ya wengi.

Niseme kwamba kampeni hizi za mwaka huu ni za kipekee. Ziko tofauti sana. Wapiga kura wengi kwa sasa wana akili nyingi sana na hawasikilizi blah blah. Ilishazoeleka wagombea kutamka uongo ulio wazi na ahadi nyingi hewa ila kwa mwaka huu inaonekana kabla mgombea hajatamka kitu inabidi ajifikirie mara nyingi sana. Watu wanataka maelezo ya kina. Kwahiyo hakuna Chama chenye wakati mrahisi tunapoiendea tar 28 Octoba.

CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kimeonyesha kuleta changamoto kwenye uchaguzi huu hasa baada ya kupata mgombea jasiri na ambaye inaonekana wazi hakuna anachohofia. Chama hicho kina mtaji mkubwa wa kura za huruma kutoka kwa watu wanaoamini kuwa Lisu alitendewa ubaya na CCM. Bahati nyingine ya hivi karibuni ambayo inaweza kuwaongezea kura za huruma ni hiki kitendo cha NEC kumsimamisha Lisu kufanya kampeni kwa siku 7. Tukiachana na kura za huruma ni wazi CHADEMA watapata kura chache kutoka makundi mengine ya wananchi.

Kosa la kiufundi ambalo CHADEMA wamelifanya na litawagharimu kwenye sanduku la kura tar 28 ni kutobandika picha za mgombea wao kama walivyofanya vyama vingine. Ikumbukwe Lissu amekaa nje ya nchi kwa miaka kadhaa na alikuwa adimu machoni mwa wapiga kura. Au chama kimesahau kwenye karatasi ya kupigia kura kuna picha za wagombea? Mabango kwa watu wa marketing watakubaliana nami ni nyenzo kubwa sana kwenye kuitangaza bidhaa. Mtu asiyejua kusoma itamsaidia sana kwenye kupiga kura. Watu kama wahadzabe mngekuwa mmewarahisishia sana.

Mimi nionavyo ndani ya CHADEMA kuna ambao kwa makusudi waliamua kumhujumu Lisu kwa kutoweka mabango. Au pia watu hao wameona tu Rais Magufuli anatosha kwahiyo wamsaidie kinamna. Ombi langu kwa Rais JPM asimsahau Mh Tundu Lissu kwenye teuzi za serikali yake ijayo.
Mgombea wetu wa CCM akiwa Zanzibar anawaeleza Wazanzibar kuwa wasiondoke uwanjani hapo maana akimaliza hotuba bado Kuna show kabambe kutoka kwa wasanii na watamuona nae akicheza.... Wazenji nao viburi wakaondoka wakati anazungumza. Aisee!
 
Rais Magufuli amteue kwenye nyadhifa itakayomfaa. Lissu kazungukwa na watu wenye uwezo mdogo mno kwenye kufikiria. Uchaguzi ukiisha ajiunge CCM kwa wasomi wenzake.
Mgombea wetu wa CCM akiwa Zanzibar anawaeleza Wazanzibar kuwa wasiondoke uwanjani hapo maana akimaliza hotuba bado Kuna show kabambe kutoka kwa wasanii na watamuona nae akicheza.... Wazenji nao viburi wakaondoka wakati anazungumza. Aisee!
 
Back
Top Bottom