CHADEMA kutoa uamuzi wa maamuzi ya Mahakama Jumamosi NMC Arusha

"Huyu akimu naskia alichanjwa chale za matak.o.ni na Profesa Maji Marefu. Ukimuuliza karatasi za hukumu za kesi zina rangi gani? Anakutajia, kijaniiiiiiiiiiiiiii"

WATCH UR TONGUE, HUJUI ULISEMALO!
 
"Nasikia leo hii jaji aliyetoa hukumu ameitwa ikulu, kwasababu kwanini hakutekeleza kama alivyoambiwa? Kumpa adhabu mh Lema ya miaka mi5 ya kutojishughulisha na mambo ya siasa. Naona imekula kwa jaji, hata pata fungu alilohaidiwa."

UNA UHHAKIKA NA USEMAYO??? AU UMEROPOKA TU????
 
Baada ya ile mitusi ya Lusinde pale Arumeru nilisema laiti angekuwa ni jamaa yangu ningeukana ujamaa wetu siku hiyo hiyo, Jaji Gabriel Rwakibalila umenishawishi niukane ujamaa wetu leo! Kwa hukumu hii nashawishika kuukana udugu wetu na sasa nimeanza kuelewa kwa nini ulipoamia Dar ukitoka mahakama ya Shinyanga ukaanza kupanda ngazi za vyeo vya kimahakama kirahisi vile pale Kisutu mpaka Mahakama kuu Dar kabla hujaamishiwa Sumbawanga, au hukumu hii umeitoa kama fadhila kulipa mafanikio uliyoyapata katika ngazi ya mahakama maana hata uwezo wako twaujua?
 
Akimu ni nini? Halafu kwenye hiyo kesi ya Lema kulikuwa na Jaji sio hakimu.

Mkuu, kumbe wote japo ni wa-Tz, hamkijui kiswahili vizuri.
Mwenzio kaandika "akimu" na wewe ukaandika "Jaji sio Hakimu", unapoandika "sio hakimu", unamaanisha wangapi?
Ushauri wangu ni kwamba ni vema kujadili hoja kuliko kubezana kwa ubovu wa lugha na kuandika lugha chafu.
 
IMGP0816.JPG


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amesema kuwa hiki ni kipindi kigumu sana kwao na pia ni kipindi cha mpito. Amesema pamoja na kuweka jazba pembeni, chama hicho kinatakiwa kuonesha dunia jinsi haki inavyopatikana.

Mbowe alisema kuwa chama hicho hakiwezi kukataa ama kukuabali hukumu ya mahakama badala yake kinalenga kutafuta haki siku ya Jumamosi katika viwanja vya NMC jijini Arusha ambapo pia watashahuriana kabla ya kutoa tamko rasmi juu ya Lema kuvuliwa ubunge.

"Mimi naheshimu sana mahakama kwa kuwa ina taratibu zake za msingi na kwa hali hiyo nawasihi sana wananchi kuwa watulivu kwa siku hizi mbili mpaka jumamosi tutatoa tamko letu kama tutakata rufaa au laa na baada ya kushahuriana na viongozi na wanasheria wetu wa chama "aliongeza Bw Mbowe.

Akiongea jijini Dar Es Salaam, Katibu wa chama hicho Dr Wilbroad Slaa amesema kuwa chama chake kitatetea kiti cha ubunge Arusha kwa kumtumia au kutomtumia Lema. Dr Slaa amesema hata kama Lema atawekewa pingamizi watamsimamisha mgombea mwingine na atashinda.
 
Taratibu na intelejensia za kipolisi, hatutaki kuona raia wanapigwa bali tuone wakilindwa! Wataisoma, chadema ina kitu cha kujifunza though.
 
Ahsante sana our chairman Freeman, sisi tuna Mungu, wao wana pesa, mahakama, na vyombo vyote vya dola. Wacha uchaguzi urudiwe, Lema agombee tena if possible, halafu yeye kwenye mikutano ya kampeni atakuwa anasalimia na kuomba kura tu, na kisha kukaa chini. Siku ya kupiga kura ccm itatambua watz wanasemaje!
 
Hakuna haja ya kupeleka kesi ya gedere kwa nyani, mahakama zote na majaji wote wapo kwa maslahi ya CCM. Hawa tuwahukumu kwa kura.

Hadhi ya mahakama miongoni mwa watu makini Tanzania iliisha pale ilipokubali kutumiwa katika suala la kuruhusu mgombea binafsi. Tanzania hakuna mahakama huru tena (hata Jaji Mkuu kasema hilo) na heshima yake imekwenda na maji. Kila mtu anajua rushwa ilivyoota mizizi na kushamiri mahakamani na uhuru wake unavyoingiliwa na serikali. Hivyo pamoja na faida zote za kukata rufaa, kwa hili, hapana. Rufaa bora ni kwa wananchi.
 
Heshima kwenu wanabodi..nimekuwa nikijiuliza maswali bila majibu.....haya yote yanaoendelea Arachuga tatizo ni Lema kuwa Mbunge au Ni CDM bila majibu!Yamesemwa mengi na CCM hasa baada ya CDM kuchukua hili jimbo kuwa maendeleo ya jimbo yapo likizo,watalii wamepungua na hata la ukame wa Arusha na mipango mibovu,stendi ya mabasi na ufisadi wote ni sababu ya Lema.
Hali ilizidikuwa mbaya katika mchakato wa kuchagua meya pale ambapo CCM kupitia katibu wa Mkoa Bi. Marry Chatanda walihamua kwa makusudi kunyonga haki ya wanaarusha.
Hata pale CCD ilipo hamua kuwavua udiwani wake katika kata 4 kutokana na usaliti wao kwa chama CCM walikuwa wa kwanza kuwa support mpaka waziri husika naye Mkuchika naye akaingiza ushabiki wake.
Tuliona ni jinsi gani vyombo vya dola vilitumika na vinaendelea kutumika kuwa wapiga marungu na mabomu viongozi wa CDM katika matukio mbali mbali.
Ikumbukwe kuwa Lema alichaguliwa na wananchi kwa ridhaa yao kwa kura nyingi bila kuonga,kutoa rushwa wala kuchakachua.
Swali langu Tatizo Arusha ni Lema au CDM?
Nawasilisha
 
Hizo hela za rushwa alizopata zitamtokea puani. Muda unavyozidi kwenda ndio ban inaninyemelea nitatukana muda si mrefu!!!!!
 
siasa za tz ni uharo mtupu.
Hakuna uhuru wa mahakama, uhuru wa raia haupo na watu wanauwawa live na wengine kukatwa mapanga tena wabunge mbele ya polisi. Lema alishapigwa na polisi mpaka kulazwa hii sio njema. Coz what goes around comes around hope ccm watakuwa wastahimilivu zali
 
We jaji, kumbuka kuwa what goes arround comes back arround. Kwa jinsi Mungu aliivyotuumba, tukionea nafsi huwa zinatusuta. Sisi tutasahau, lakini wewe hili unalo kwa maisha yako yote. Najua one utatelekezwa kama Sioi wa Arumeru mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa ubunge kutangazwa
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom