CHADEMA kutoa uamuzi wa maamuzi ya Mahakama Jumamosi NMC Arusha

Naamin uchaguzi ukirudiwa, jimbo linabaki chadema kila mtu anajua mpaka makada wa ccm wanajua hilo. Let us decide to learn and other nations learn what Tanzanian court is doing.
 
Mamlaka zilizowekwa zimewekwa na mungu. na sauti ya uma ni sauti ya mungu. haihitaji unabii kujua mustakabali wa taifa hili. kifupi tusubiri wanachi waweke mtu wamtakaye arusha wala si mahakama. kama sheria ni msumeno kuna ushaihidi wa kutosha wa kuwavua ubunge walw jamaa waliongea ovyo arumeru. Naomba CDM wakubali uchaguzi ndani ya siku hizo ili wadhihirishe ulimwengu kuwa nini maana ya Magamba.
 
Nimeeleza sababu kwenye post ikiwemo kusahihisha hukumu isiyo ya haki ili mahakama isigeuzwe kuwa kichaka cha wanasiasa na majaji walafi. Naamini viongozi wa Chadema watajadili hukumu hii na kukata rufaa kwa kuzingatia maelezo niliyoyatoa kwenye post.

Nadhani hayo yote CHADEMA na wananchi wanayaelewa ndio maana muelekeo sasa ni Uchaguzi, kwa kufanya uchaguzi watu watazidi kuelimika unlike kurudi kwenye system hiyohiyo ambayo iko rotten
 
Una hoja nzuri lakini context na mantiki mmh!

Mahakama kuu na yenye uwezo mkubwa kirufaa na kwa mazingira yalivyo sasa ni wananchi. Kwa vile magamba walilianzisha basi wacha CDM wapeleke rufaa yao kwa wenye nchi; maana sasa wanafuatilia nchi yao inaendeshwaje na wanataka kushiriki ktk maamuzi.
 
Rufaa! ya kazi gani kwa mahakama hizi za kifisadi! hivi huoni rufaa ya dowans! ha ha ha! kila siku mihela yaongezeka! Mwenye dowans, anayekata rufaa, Jaji ndiye huyo huyo! Rufaa haina maana kwa wanyonyaji hawa.
 
Kwa mabadiliko ya sasa katika nchi yetu, Godbless Lema/CHADEMA haiwezi kuzidiwa na yeyote katika wanachama hai, si Batilda wala Kinana (mafia wa meli). Kuna mmoja tu anayeizidi CHADEMA/Lema umaarufu naye ni Hayati Julius K. Nyerere (rip)
 
Kinacho tuuma wananchi wa ars ni iwapo Lema hotogombea! na kama itakuwa hivyo chama kifanye utani wa karne! unakumbuka issue ya ndizi na chungwa kenya basi cdm waweke jina jiwe! hafu tuanze kampeni wakitaka picha tunapeleka ya jiwe
 
I beg to differ. CDM must think big. Wakithubutu tu kukata rufaa kesi itaburuzwa hadi 2015 na ndicho wanachotaka Magamba kwani hata wao wanajua wazi kuwa CDA Arusha hata wakisimamisha punda watashinda. Pamoja na maamuzi mabovu ya mahakama CDM waihimize tume ya uchaguzi iitishe uchaguzi hata kesho, tena bila hata kampeni!
 
Hukumu iliyotolewa ya kumvua ubunge Mh. Lema haikutarajiwa kwa kuzingatia mwenendo wa kesi. Katika hali hii ni lazima Chadema kwa kushirikiana la Lema wakate rufaa kupinga hukumu hii. Sababu za kupinga hukumu ni kubwa kiasi kwamba Lema kwa kusaidiwa na Chadema lazima wakate rufaa

Haki haikutendeka

Hukumu ya kumvua Ubunge Lema siyo ya haki kwa kuzingatia mwenendo wa kesi. Hakuna ushahidi iliotolewa ambao haukuacha shaka yoyote kuwa Lema alitenda kosa la kumtukana Batilda. Na hata kama ushahidi usingeacha shaka yoyote hicho kinachoitwa tusi si kosa la kumvua ubunge Lema. Mwanasiasa yoyote anayegombea inabidi mwenendo wake wa maisha uhojiwe li kuona kama anaweza kushika madaraka ya kisiasa. Hata kama ushahidi mzito ungeonyesha kuwa Lema alidodosa maisha ya mgombea, hiyo haiwezi kuwa kosa la kumvua Ubunge. Wote tunatambua namna maisha ya wagombea wa Chadema yanavyohojiwa wakati wa chaguzi Mbalimbali, za ubunge na uraisi. Na hii ni haki kwa wananchi kujua, siyo kosa. Pamoja na mapungufu ya kutungwa kwa kosa, pia hakuna uthibitisho wa nguvu wa hicho kinachoitwa kosa kuwa Lema alikifanya. Ni ushahidi wa kutunga wa maneno, hakuna ushahidi wa maandishi wala sauti katika mkanda wala CD kuwa Lema alitoa matamshi yaliyotungiwa mashitaka

Kutekeleza M4C (Movement for change)- Vuguvugu la mabadiliko
Chadema lazima kielekeze vuguvugu la mabadiliko la M4C lililozinduliwa huko Arumeru katika maeneo yote. Kwa wananchi, kwa wabunge, kwa wana-CCM na katika mhimili wa Mahakama. Kwa sasa, Chadema kimpatie Lema kazi ya kutekeleza mikakati ya M4C wakati rufaa ya kupinga hukumu imekatwa. Lema hatakosa kazi ya kufanya katika chama wakati kesi ya rufaa inaendelea au wakati wa kusubiri kupangiwa kesi. Lema hana cha kupoteza kwa kukata rufaa kwa sababu tangu alipoamua kujiunga na Chadema alijiunga siyo kwa ajili ya kutafuta ufahari au mali bali kusaidia kuondoa ukandamizaji wa CCM. Ndiyo maana alikubali kukaa mahabusu ili kupinga ukandamizaji wa Polisi. Watanzania wote wanaojiunga na Chadema wanachagua kutetea wananchi, wanamapenzi na nchi yao na hawakimbiliii mali, wanaokimbilia mali za kifisadi hujiunga na CCM. Wanaojiunga na Chadema ni watu ambao wameweka rehani hata maisha yao wenyewe kwa ajili ya kuitetea na kuilinda nchi yao dhidi ya ufisadi na dhuluma ya CCM na serikali yake.

Kutathmini mhimili wa Mahakama
Kwa kukata rufaa Chadema kitaweza kutathmini mwenendo wa mhimili wa mahakama. Tunataka kujua kama jaji Gabriel Rwakibarila aliyetoa hukumu ametumiwa na CCM na serikali yake kama yeye binafsi au imehusisha mtandao wa majaji wengine katika mhimili wa mahakama. Tunajua kuwa kuna wanasheria ambao wamekuwa wakitumiwa na wanasiasa mafisadi kuhujumu uchumi wa nchi kwa kusaini mikataba ya kifisadi. Mikataba yote ya kifisadi imehusisha wanasheria wasiokuwa na uchungu na nchi yetu. Tumejua kwa mwenendo wa kesi ulivyokuwa kwamba jaji huyo ametumika na CCM kutekeleza azima yao. Tunajua jinsi Lema alivyokuwa mwiba bungeni kwa waziri wa mambo ya ndani na pia waziri mkuu pinda na jeshi la polisi. Siyo ajabu kwa CCM na Serikali yake kumtumia huyo jaji ili kumkomoa Lema na Chadema. Kwa Chadema kukata rufaa wananchi tutajiridhisha kama muhimili wa mahakama utalinda hadhi yake kwa kutengua hukumu hiyo isiyo ya haki. Kama itaibariki tutakuwa tumetambua tatizo kwa ujumla wake na kuwatambua kwa majina majaji wanaoshiriki katika kuua demokrasia na hivyo kuwa target ya M4C. Tunaamini kuwa mahakama ya rufaa italinda hadhi yake kwa kutengua humu hiyo isiyo ya haki ili mhimili wa mahakama na taaluma ya sheria visidhalilishwe.

Kutunga sheria zenye hadhi
Kwa kutata rufaa, Chadema na Lema watakuwa wamesaidia wananchi kukataa sheria dhalili. Maana kwa kuiacha hukumu hiyo kama ilivyo, itaingia kwenye kumbukumbu za sheria na hivyo kuwa sehemu ya nukuu katika taaluma ya sheria na katika muhumili wa mahakama. Tunataka Chadema ifanye kwa vitendo kukataa sheria za ovyoovyo na hasa tunapoelekea kutunga katiba mpya.

Yani wewe ni gamba 'live'.Kama mlitegemea rufaa ili mfanye ujanja wenu hapo mmeliwa hakuna haja ya rufaa, turudi kwenye uchaguzi maana ndo itayokuwa process isiyopoteza muda
 
Hayo ndiyo maombi ya magamba,kwamba akate rufaa,iende hadi 2014,halafu Lema anashnda kesi,ili Lema akose muda wa kuwatumikia wananchi!
 
CHADEMA wana mtaji wa kura 57,000, mpinzani wa karibu ana 37,000.takwimu zinaonyesha kuwa kura za CHADEMA zinaongezeka kwa kasi.so we have nothing to loose kama hawatakata rufaa kwa sababu baada ya siku chache tutampata Mbunge mwingine wa CHADEMA.Awe ni Lema au mwingine yeyote kulingana na uchaguzi wa mgombea ndani ya chama.Faida na hasara za kukata rufaa ni kama zilivyoainishwa hapo juu,
 
kwa mawazo yangu..hakuna haja ya kukata rufaa...hii ni fursa ya kujijenga kwa uchaguzi ujao...leo arusha..utasikia kinafuata ni ubungo...sina uhakika na segerea...kama chaguzi hizo zitarudiwa..ni muda wa kuungana na kusema sasa basi kupitia sanduku...
 
Hakuna haja ya kupeleka kesi ya gedere kwa nyani, mahakama zote na majaji wote wapo kwa maslahi ya CCM. Hawa tuwahukumu kwa kura.
 
Siasa za Arusha ni ngumu ka jiwe. Kwenye uchaguzi wa Arumeru tulishuhudia mengi. Kama Felix Mrema hajakata tamaa ataingiza timu na anaweza kutoa upinzani wa kutosha.
Uzoefu unaonyesha kwamba katika chaguzi za Arusha mjini CCM walihujumiana na hata huu wa Arumeru wamehujumiana.
 
Back
Top Bottom