Uchaguzi 2020 CHADEMA kutikisa Dar kwa siku tatu, Uchaguzi Mgombea Urais Tanzania na Zanzibar

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Sasa ni Rasmi.

Chama kikuu Cha upinzani nchini CHADEMA kitaanza vikao vyake kwa siku 3 mfululizo kuanzia Jumapili tarehe 2 mpaka Jumanne tarehe 4 katika ukumbi maarufu nchini wa Mlimani City.

Kikao Cha Kamati Kuu kitafanyika kesho Jumapili huku Baraza Kuu likiwa siku ya Jumatatu na Mkutano Mkuu utakuwa siku ya Jumanne.

Agenda Kuu ya vikao hivi ni kuchambua na hatimaye kupiga kura kumpitisha Rasmi mgombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA.

Tayari wajumbe wa vikao hivi wameshaanza kuwasili jijini Dar es Salaam wakiwa na shauku kubwa ya kutimiza takwa la kikatiba.

Mchuano mkali kwenye nafasi ya Urais ni Kati ya mafahali wawili Lazaro Nyalandu Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kanda ya Kati na Mjumbe wa Kamati Kuu akipambana na Tundu Lissu Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa na mwanasiasa mashuhuri zaidi kwa Afrika.

Ikumbukwe CHADEMA ilitikisa nchi siku ya Jumanne wiki hii wakati maelfu kwa maelfu ya watu walipojaa majiani kumlaki Tundu Lissu aliyerejea matibabuni huku kukiwa na maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea nchini kumsindikiza mwanasiasa huyo makao makuu ya Chama huku umati huu ukiimba 'Rais' Rais' Rais' kote alikopita ambapo Barabara ilifungwa kwa masaa manne kumsindikiza shujaa huyo.

Sisi wa Molemo Media Kama Sikuzote Tunatarajia kuwaletea matangazo ya moja kwa moja wasomaji wetu wa Jamii Forums ili Dunia kuweza kujua kinachoendelea ndani ya vikao hivyo muhimu.Tuna Imani hatukuwahi kuwaangusha wafuatiliaji wetu.

Wagombea wa CHADEMA ni;

Wakili Simba Neo

Lazaro Nyalandu

Tundu Lissu

Dk.Maryrose Majinge

Wakili Gaspar Mwanalyela

Isaya Mwita

Mchungaji Leonard Manyama

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatoa taarifa kwa Vyombo vya Habari na Umma wa Watanzania kuhusu ratiba ya vikao vya ndani ambavyo vitahitimisha uteuzi wa Mgombea wa Urais na Mgombea Mwenza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa Urais wa Zanzibar.

Vikao hivyo vya kitaifa ambavyo ni, Kamati Kuu ya Chama, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, vitaketi kwa siku tatu mfululizo na kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba ya Chama ya Mwaka 2006, Toleo la Mwaka 2019.
Kikao cha kwanza kitakuwa ni Kamati Kuu ya Chama itakayokutana Jumapili, Agosti 2, mwaka huu, itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kikatiba unaoelekezwa kwenye ibara ya 7.7.16(a) “Kufanya utafiti wa wagombea wa Urais na Mgombea Mwenza na kuwasilisha ripoti zake kwa Baraza Kuu.”

Tarehe 3, Agosti 2020, Baraza Kuu la Chama litakutana katika kikao chake, ambapo litajadili masuala mbalimbali ikiwemo “kufanya mapendekezo ya wagombea wa Urais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar na kuyawasilisha katika Mkutano Mkuu kwa uamuzi,” inavyoelekezwa kwenye ibara ya 7.7.12(a).
Aidha, kwa mujibu wa ibara ya 7.7.12 (n) Baraza Kuu litajadili rasimu ya Ilani (manifesto) ya Uchaguzi Mkuu na kuwasilisha mapendekezo yake kwa Mkutano Mkuu kwa maamuzi.

Tarehe 4, Agosti 2020, Mkutano Mkuu wa Chama utaketi na kutekeleza kazi zake, ikiwemo “kuteua mgombea wa Urais na mgombea mwenza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa Zanzibar,” inavyoelekezwa kwenye ibara ya 7.7.10 (c). Halikadhalika, Mkutano Mkuu wa Chama utainidhinisha Ilani (manifesto) ya Chama kwa Uchaguzi Mkuu, kwa mujibu wa ibara ya 7.7.10 (h).

Vikao vyote kuanzia Agosti 2 hadi 4, 2020, vitafanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Imetolewa leo Jumamosi, Agosti 1, 2020 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na MawasilianoView attachment 1523692
2473056_IMG_20200801_153107 (1).jpg
 
Dah umeandika kishabiki sana mkuu yaani maandamano ambyo hayajawahi kutokea tanzania? yepi hayo ?huyuhuyu lissu na ni siku hyo akirudi ? unachekesha kama hayo ndiyo maandamano ambayo hayajawahi kutokea utakua siyo mfuatiliaji wewe au akli yako inashida mahala kwenye medula oblangata
 
Hizo ndo habali watanzania hasa wapenda demokrasia haki na utawala bora ndo huwa wanapenda kuziskia achana na zile habali za kibaguzi
 
Lisu asipopita chadema mtakuwa mmejiangusha wenyewe. Wengine tunasubili jina la mgombea wa chadema ili tuanze kuzisaka kadi zetu za kupigia kura zilipo,

Nje ya hapo hatupigi kura, mimi nawakilisha wengi ambao tunasubili jina la lisu, kama tupo pamoja gonga likes za kutosha
 
h
Lisu asipopita chadema mtakuwa mmejiangusha wenyewe. Wengine tunasubili jina la mgombea wa chadema ili tuanze kuzisaka kadi zetu za kupigia kura zilipo,

Nje ya hapo hatupigi kura, mimi nawakilisha wengi ambao tunasubili jina la lisu, kama tupo pamoja gonga likes za kutosha
apo anapita nyalandu hivi unamjua mbowe wewe>? za awali tu kambwaga lissu vibaya unategemea nini ?
 
Back
Top Bottom