CHADEMA Kususa Mwenge na sherehe za miaka 50 ya UHURU ni KUKOSA UZALENDO

Nchi haiendeshwi kwa kusubiri chenji kwa hiyo mnasubiri kosa lingine ili mpate chenji ya kujenga zahanati? hizo sherehe sherehekeni nyie na watoto wenu sisi ni job kama kawa.

Nawapongeza sana makamanda kwa kususia hawataki kuwa sehemu ya unafiki kwa sababu hata maana ya sherehe yenyewe inapotoshwa imekuwa ya kisiasa si ya kitaifa tena, kama leo tunasherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania ikifika mwaka 2014 itafikisha miaka mingapi 53?

Feedback,
Nakubaliana na wewe hapo juu na karibu kila kila comment zako huwa ni nzruri.
Ila nina swali footprint yako ( E L for ccm Chairman 2012) Matumaini yapo?
 
Waungana katika pitapita zangu nimegundua wana CDM hawafurahi TZ kusheherekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika.
Dalili zimejoinyesha;-

1. Viongozi wao katika ngazi zote kutoshiriki vikao vya maandalizi ya Mwenge wa Uhuru
2. Viongozi wao kushindwa kushiriki kuukimbiza mwenge ulipofika katika maeneo yao; mfano Ubungo (mhe.Mnyika) na Kawe (mhe. Mdee ).
3. Wabunge wao wameshindwa kushiriki katika vikao vya maandalizi ya miak 50 ya uhuru pasipo kutoa udhuru.


Watanzania inabidi tutumia akili ya mbaimbawi tuwahukumu CDM katika masanduku ya kura kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa 2012 na tuwape kichapo kikubwa uchaguzi mkuu 2015. Hawa wamekosa uzalendo, wamebaki kushabikia sera za Mfadhili wao David Cameroon.

Hukumu hiyo na kichapo hicho utakipata wewe na hao waliokutuma.
 
Hii ni fursa pekee kwa watz kujiuliza, kutafakari pale tulipojikwa na kupata mkakati wa kitaifa, TUZIDI kusonga mbele.

Mwaka 1961, graduate walikuwa 12, leo wapo mitaani hawana idadi wengine wanatumika pasipo kujitambua kushiriki maandamano ya CDM; tuwe waungwana tujitambue maendeleo yamepatikana.

Leo watoka Mwanza hadi DSM siku moja.

UDOM ni ishara ya maendeleo katika elimu

Powertillers kwa wakulima walioingia katika KILIMO KWANZA

Ndugu yangu una roho ngumu, du
 
Utaonekana mwenda wazimu iwapo utaangusha bonge la party kusheherekea anniversary ya ndoa ya jirani yako.
 
Kama nimewahi kukutana na thread kichefuchefu basi ndio hii. Hivi wewe, uhuru una maana gani kwako? Unapozungumzia uzalendo sijui unamaanisha nini! Kukosa uzalendo kunaweza kuthibitika kwa vitendo kwa tunayoyaona na wala sio haya unayotuambia. Kama kukataa kuwapigia makofi na kuwapongeza wanaotuibia mali za nchi ni kukosa uzalendo basi hata na mimi si mzalendo.

Unaonekana unaishi ktk primitive age ilhali mwili wako tunao hapa kwenye dunia mpya. Mwenge wa uhuru kwa Watanzania wengi umeshakosa maana kwa kuwa hawako huru. Kama mashamba ya vijiji yameporwa toka kwa wakulima wetu na kupewa wawekezaji wezi huo ndio uzalendo wa CCM?

Watu wanaiba fedha za umma na wanathibitika kuwa wameiba badala yake wanaambiwa wazirejeshe na hata baada ya kurejeshwa hazijulikani zilipo, huo ndio uzalendo? Kweli akili nzuri ukiwa nayo. Wewe ndio wale mnaotoka jasho la kwapa kwenye gari la kampeni za CCM mkikatika viuno kwa ujira wa sh 2000 kwa siku, T-shirt na khanga.

Nikukumbushe kuwa: Wakati Idara za Serikali na Taasisi zake zinatoa thsh 75,000 kununua pair moja ya sare za sherehe ya miaka 50 ya sijui kitu gani hicho mnakijua wenyewe, kuna wenzetu kule vijijini wanakufa kwa njaa japo mkuu wa wilaya yao alikanusha kwa kuwa hajawahi kufika huko. Tumia akili zako vizuri na usirudie tena kuita watu mbayu wayu, wewe ndio mbayu wayu hasa (kinega) usiye na akili ya kufikiri ukajua kuwa uhuru haujapatikana kwa wote zaidi ya wale waliopata bahati ya kuchaguliwa na watu wenye akili kama zako, waibe fedha za umma kwa ajili ya familia zao huku wewe ukiwapigia makofi.
 
Mashilili acha ushamba wewe wa kulinganisha takwimu mbovu na muda.hata wewe ulipozaliwa hukuwa na ndevu na sasa unazo.je hayo ni maendeleo?
 
Kwanza tuanze na mwenge wa uhuru.
Huu mwenge ni wa uhuru gani? Tanzania ina mataifa mawili tu katika katiba ya nchi,yaani Zanzibar na Tanzania ambayo ni muungano.Je mwenge wa uhuru ni mwenge unaohusu uhuru wa Zanzibar? au unahusu uhuru wa muungano?
muungano hauna uhuru,

Kwahio mwenge wa uhuru si wa Zanzibar wala muungano ambazo serikali mbili ndizo zilizomo katika katiba ya Tanzania, kwahivyo mwenge na sherehe za uhuru wa Tanganyika hauhusiani kabisa na shughuli za muungano wa Tanzania kwani hio nchi haipo wala haitambuliwi tena,
hawa jamaa wamekuwa wakiutembeza na kuishangilia siku ya uhuru wa Tanganyika kwa fedha za muungano tokea mwaka 1964,ambapo fedha hizo si halali kuziendeshea shughuli za Tanganyika isiyokuwepo ndani ya Tanzania aidha Zanzibar inabidi ilipwe zaidi ya dola billioni moja kwa makosa yote ya uhalifu na utumiaji fedha za muungano kwa shughuli za Tanganyika au Tanzania Bara ambazo hazipo katika katika ya nchi.


Sherehe za uhuru:

Kuna habari imetoka magazetini ambazo rais wa marekani ametuma salamu za hongera kwa rais kikwete kwa kutimiza miaka 50 ya uhuru wa Tanzania, (miaka 50 ya uhuru wa Tanzania?) uhuru wa Tanganyika 1961-2011 ni mika 50 na uhuru wa Zanzibar hapo ilikuwa ni mika 3 baadae yaani jan 12-1964. hapo inakuwa uhuru wa Zanzibar una miaka 47 sasa, na huo uhuru wa Tanzania wa kutimiza miaka 50 ulikujaje hapo wakati bado Zanzibar ilikuwa inatawaliwa na sultani?

Kwahio hawa jamaa wanautangazia uhuru wa Tanganyika au wanaitangazia Tanganyika au shughuli za Tanganyika kimataifa kama ni Tanzania hali ya kuwa ni Tanganyika ndani ya Tanzania na kuiba mamilioni ya fedha za Zanzibar hivihivi yaani.
Obama si mchawi kuwa anaweza kuamka tu agaagulia kuwa Tanzania inafanya uhuru wake miaka 50 dec 6,kwanza Tanzania sio nchi ya kufanya sherehe za uhuru kwani Tanzania haina uhuru bali sherehe za muungano badala ya sherehe za uhuru,hivyo viongozi wa Tanganyika ndio wanaopeleka habari nchi zote duniani kuwa Tanzania inafanya uhuru wake miaka 50 hali ya kuwa ni Tanganyika. hilo ni kosa kubwa sana kuishirikisha serikali ya Tanganyika katika shughuli za muungano wa Tanzania.
Hii hapa tena uhai tosha kua katika michuano ya kombe la CECAFA linaloendelea hivi sasa hapo dar,viongozi wa tff wa bara wanapeleka matokeo ya mechi zote za timu ya taifa ya Tanzania Bara kama wanavyoiita kilimanjaro stars kuwa ni kama matokeo ya timu ya taifa ya Tanzania,ambapo katika world ranking yataingizwa na matokeo yanakuwa ni timu ya taifa ya Tanzania ndio wanaocheza michuano hio na sio Tanzania Bara,hapo chini nimekutumia website ya fifa uiangalie ili uipeleke kwa wahusika kwavile Zanzibar pia inacheza hio michuano lakini matokeo yake hayawekwi katika fifa bali matokeo ya Tanzania Bara ambayo sio timu ya taifa ya Tanzania yanawekwa kama timu ya taifa ya Tanzania.
Je ni kigezo gani kinachopelekea wao waingizwe katika kuwa ni Tanzania hali ya kuwa ni bara? na hayo wamekuwa yakifanyika kila mwaka wakati timu ya taifa ya bara inapocheza katika mechi yoyote ile.mbali na kuwa timu hio ilikufa tokea muungano wa Tanzania ulipoanzishwa na wao hawakutakiwa kushiriki tena maisha yao,hio pia ni corruption kubwa sana ya katiba hivyo wanatakiwa wailipe zanziabr bilioni moja dola ambazo wamekuwa wakizitumia katika njia chafu tokea mwaka wa kwanza wa muungano.
Wao tff walipeleka habari kuwa Zanzibar ilikufa utaifa wake tokea muungano wa mwaka 1964, je wao tnganyika wanaweka matokeo yao ya taifa la Tanzania Bara linalocheza CECAFA na mpinzani wake wa kundi jingine ni nchi ya Zanzibar iweje wao taifa lao la tnanzania bara halikufa katika muungano wa mwaka 1964 na wetu sisi uwe ulikufa? iweje wao wanashiriki mara mbili kama timu ya taifa ya Tanzania ya muungano na pia timu ya Tanzania Bara pia kama muungano?
Utaifa gani wa Zanzibar wanaodai ulikufa mwaka 1964 baada ya muungano? Kama baada ya muungano tu Zanzibar walikuwa sio nchi tena mbona ni miaka ya hivi karibuni wabara bado walikuwa wanaingia Zanzibar na pasport za mchele.je kama Zanzibar ilikuwa sio nchi tena mwaka huo 1964 ilikuwaje waingie ndani ya nchi ya Zanzibar na pasport?lakini hata mwishowake walipoamua kuondoa pasport kwenda Zanzibar kwavile ni part ya muungano hakuna sheria njingine yoyote iliyotungwa inayosema kuanzia sasa kwenda Zanzibar itakuwa ni bila pasport na Zanzibar kuanzia sasa itakuwa sio nchi tena,hakuna hakuna hata kipenegele kimoja kilichowekwa hapo kuwa Zanzibar ilikufa utaifa wake baada ya kuondoa pasport iweje utaifa ulikuwa umekufa mwaka 1964 baada ya muungano?
Katika maoni ya katiba hivyo vyama vya akina chadema na vinginevyo wanadhani hio katiba inaweza kuibada Zanzibar kudai chake. hivyo vyama ni vyama vilivyozaliwa katika muungano tu,havihusiani katika masuala ya kuibana au kuiathiri Zanzibar katika masuala yake kama nchi,
ahsante.
 
Nilishtushwa na habari hizi ambazo nadhani wazanzibar walikuwa muda wote hawajaamka nazo.Kwakifupi kila mwaka hufanyika mashindano ya mpira wa miguu kwa timu za taifa za nchi za Africa mashariki na kati (aidha huwepo pia baadhi ya timu waalikwa kutoka nchi moja au mbili za upande mwingine wa Africa). Lakini muhimu timu za taifa za nchi mshiriki "kwa mujibu wa sheria ya CECAFA chama cha soka cha Africa Mashariki na kati ni kuwa nchi hizo ziwe huru ambazo hazitawaliwi tena na ziwe na nyimbo na bendera y waandaaji wa mashindano hayo ya mwaka jana na mwaka huu ni Tanzania Bara(ambao hio nchi ya Tanzania kwa bahati mbaya hawana bendera ila wanaitumia bendera yetu ya muungano na pia hawana nyimbo ya taifa pia wanaitumia tena kwa kosa jingine nyimbo yetu ya taifa ya Tanzania).
Hilo ni kosa kubwa sana muheshimiwa kufoji kitu kisichokuwepo katika sheria ya nchi,kuiingiza nchi ndani ya nchi pasipo kushirikishwa Zanzibar hilo ni kosa kubwa sana.Kila mwaka nchi wanachama zinatakiwa kulipia uwanachama wao wa nchi za CECAFA "tena kwa mara nyingine Tanzania Bara inalipiwa pesa hizo kutoka pesa za muungano bila Zanzibar kushirikishwa,aidha kunakuwa na kiasi fulani cha fedha ambacho nchi wanachama hupatiwa na CECAFA hapo kwa mara nyingine tena Tanzania Bara inapokea rushwa ikiwa kama ni nchi wakati nchi hio ni kivuli ndani ya Tanzania.
Mara nyingi kumekuwa na kawaida wahamiaji haramu kutoka ethiopia na somalia huwa wanakamatwa kutoka misituni walikojificha na kufikishwa mahakamani pamoja na watanzania ambao huwa wanawaingizwa nchini kwa njia za panya pia hufikishwa mahakani,
Ndugu muheshimiwa "nchi ya Tanzania Bara imeandaa mashindano ya CECAFA kwa mwaka wa pili mfululizo wanawaalika watu"nchi nyingine"kuja kucheza mipira"yaani kufanya kazi ya kulipwa pesa nyingi" kinyume na sheria za nchi) kama waandaaji wa mashindano hayo ni Tanzania Bara basi nchi hio haitambulikani kwa mujibu wa sheria ya Tanzania kwahivyo kuwaalika watu kuja nchini,tena kufanya kazi bila ya kibali cha muungano basi hilo ni kosa kubwa sana,huwezi kumualika mtu kama sio raia wa nchi,raia gani wa nchi ya Tanzania Bara waliowaalika hao watu kuja kucheza mipira?
Hawa watu wa bara wana nchi yao ya Tanzania Bara ndani ya Tanzania kwa muda wa miaka mingi sana,wamekuwa na timu nyingi za taifa za vijana wa marika mwalimbali wa Tanzania Bara ambao huwa wanakaa hoteli kwa muda kila mara,kusafiri,kupewa posho,kuzilipia timu zinazokuja kucheza nazo na viongozi pamoja na marefaree ,ambapo tokea Tanganyika ilipokuwa na kuunda Tanzania nchi ya Tanzania Bara imekuwa ikiingia katika mashindano hayo kwajina la Tanzania(taifa stars) mpaka miaka michache tu iliyopita waZanzibari walipopiga marufuku jina hilo lisitumiwe kwavile linawashirikisha wachezaji kutoka bara peke yao,kutokana na hali hio walibadilisha jina kutoka taifa stars na kuita timu ya soka ya Tanzania Bara "kilimanjaro stars".
Kutokana na wizi "corruption walizozitumia hawa jamaa wa bara kwa miaka mingi, serikali ya Zanzibar inabidi iwapige faini ya zaidi ya dola billioni moja za kimarekani kwa makosa yote hayo waliyokuwa wakiyafanya kwa miaka yote na wanaendelea kuyafanya hadi sasa,aidha muungano utakuwa hapo ndio umekwisha kutokana na wenzetu kufanya makosa za jinai kwa muda wa miaka mingi sana na kuiibia au kutumia mali za muungano ikiwemo zanzibar kwa muda mrefu sasa.
Ikiwezekana ndugu waheshimiwa wabunge wetu waliopo bungeni waje kwa haraka hapo nyumbani wakutua na wenzao wawakilishi ili suala hili hawa jamaa wasitufanya mabaradhuli kila siku.
Miungano hio yao sheria za mbio za mwenge tayari zimepitwa na wakati,miungano mingi ya kijanja janja imevunjika hao waaanzilishi wao russia ,yugoslavia,bosnia na sehemu nyingi imekwisha pitwa na wakati,hawa wenzetu wa bara wanadhani kuwa muungano kuwa labda kuna kipengele cha sheria kinachosema muungano ni lazima?
Hakuna kifungu chochote cha sheria za muungano kuwa ni lazima/kwanguvu na lazima iwe maisha huo muungano,wenzetu hawajui kuwa Zanzibar ni nchi kamili na inaheshimu tu muungano lakini inao uwezo wa kuamka siku moja na kutangaza rasmi kuwa Zanzibar imejitoa katika muungano wa Tanzania na kuwa ni nchi huru inayojitegemea na kuanzisha embassy zake nje na kuwaita wawekezaji kuja hapo nyumbani.
Pia kila mwezi wa Dec 09 wanasherehekea uhuru wa Tanganyika nchi ambayo haipo tena,na isitoshe wanatumia wimbo wa taifa na bendera ya taifa na kugharimu mamilioni ya fedha za muungano kwa sherehe hizo ambazo hio nchi wala haipo,kwahio wenetu bado wana nchi ya Tanganyika lakini pia hio Tanganyika inabadilika katika mpira wanaiita Tanzania Bara ,au kuna Tanzania Bara na Tanganyika pia ndani ya Tanzania? je pesa za kugharamia shughuli za kusherehekea uhuru wa Tanganyika kwa miaka yote hio sio hizi pesa zetu za muungano?
Tanganyika inapesa zozote zile ilizoziwacha kufanyia na kugharamia shughuli hilo ghali mno kila mwaka?au kunawafadhili wanao zifadhili sherehe hizo za Tanganyika?kutokana na hali kama hizi muungano tayari muda mrefu umekwisha hapa inabidi wazanzibar wakate huu mzizi wa fitna,hata wananchi wa Zanzibar wanaoishi bara hawachukuliwi na wenzao kama watanzania hadi leo wanawaita wapemba na kuwanyanyasa tu.
Kama ikiwezekana mwaka huu kwa mara ya kwanza Zanzibar zasimshirikishe mtu yoyote katika katika sherehe hizi,kwani kunaunguza mamilioni ya fedha ya nchi yetu kwa upande wa muungano,hizi sherehe za mwaka huu zitakuwa kubwa sana kwahio kutakuwa na majeshi na magari yao,watu kutoka mikoa yote ya nchi ambao watakuwa wakilala mahoteli ya kifahari na kula chakula kizuri kwa fedha zetu za muungano kwaajili ya nchi ambayo haipo.
Isitoshe kwa upande wao nchi yao ya Tanzania Bara haipo nchini lakini inashirikiki mashindano ya mpira kwa timu za taifa,pia vilabu vyao kila mwaka vinashiriki mashindano ya vilabu vya soka kwa nchi za Africa mashariki na kati ambapo kwahivi sasa yanga ya Tanzania Bara ndio mabingwa wao.
Lakini kama wao wanaitambua Tanzania Bara na kuingiza mashindanoni suala kwanini wao wanashindidwa kufanya hisani kwa wenzao wazanzibar timu yao ya taifa ikashiriki katika mashindano ya Africa na pia kuwania kushiriki kombe la dunia?kama nchi ya Tanzania Bara ipo ndani ya Tanzania,basi Kikwete ni lazima aandike barua kwa fifa kuwa nchi ya Zanzibar ipo na inajitegemea kama nchi kamili ili ishiriki mashindano kivyake vyake.
Vinginevyo Kikwete inabidi asimamishe mashindano ya mpira yanayoendelea hivi sasa dar ambao Tanzania Bara ndio waandaaji kwa fedha za muungano,na pia uhuru wa Tanganyika usifanyike pia mwaka huu kwavile nchi hio haipo ambapo pia ni fedha za muungano ndio zinazouungua hapo na kuwaua wanzaniabar njaa.
Coach Salum
 
Hivi dk 90 mpira zikiisha,na man u akapigwa 6-1 na man city,kuna haja fergason na watoto wake wakajipongeza kwa mbwembwe zote hizi eti angalau tumepata goli moja au warudi wakajipange kwa mechi ijayo,mtoa mada ana lake jambo na tumemshutukia!!!!!
 
Katika hili swala la Mwenge na Maadhimisho ya miaka 50 ya UHuru wa Tanganyika kusema kweli mimi sintakubaliana na Chadema na kwa sababu zangu maana mimi ni Mhafidhina na Utaifa wangu unatangulia kwanza hata kama kesho Afrika itaungana na kuwa nchi moja.

Tafisri ya neno UHURU itabakl palepale kama siku wananchi wa nchi fulani wamepoata UHURU wao, ikiwa na maana hoja ni WATU waliokuwa huru ktk mipaka ya NCHI hiyo. Na UHURU huu unaweza weka mipaka ama kupunguza mipaka lakini kitu muhimu ni raia wananchi wake kuondokana na kutawaliwa..Na kama nilivyosema, kila nchi ina WATU na MZINGIRA tofauti hivyo hatuwezi kuiga nchi kama Mareakani ambayo inasherehekkea Uhuru wake July 4, kwa sababu ndiyo siku nchi hiyo ime declare Uhuru kutoka kwa koloni la Muingereza na zikiwemo nchi 13 tu, leo hii zimefikia 50 na zaidi na bado wanaweza kuongeza nchi nyingine wakiendelea kutumia jina la USA..

Tofauti na wao, sisi tumebadilisha jina baada ya kuunganisha nchi zetu mbili bila kufikiria mbele maana ni asili yetu kufikiria kwa marefu ya mkono. Kesho tukiungana na Kenya au Uganda lazima tutabadilsiha jina na vivyo hivyo maana Muungano wetu bado una tabaka za kijamii ambazo tumeshindwa kuzivunja. Zanzibar wana/taendelea kusherehekea siku ya Mapinduzi na halali kwao lakini haramu kwa Bara kusherehekea Uhuru wao. Kwa nini tunajaribu sana kujidanganya? ukweli unabakia kwamba Bara ipo ni nchi ambayo kisiasa tu tunaindoa ktk ramani lakini hatuwezi kufuta historia kwa siasa vile vile, Mungu apitishie mbali kesho Muungano ukifa tutarudi kwa nani?

Na kwa nini watu waseme tusherehekee miaka 50 ya Tanzania ifikapo April 2014 ikiwa hizo zitakuwa sherehe za Muungano wa nchi ambazo tayari zilikwisha kuwa HURU.. Je kweli tunakubali kupoteza historia ya UHURU wetu kwa siasa na majivuno ambayo ndiyo yalipelekea tukasahau hata kuweka kumbukumbu za vita ya Maji Maji, ukweli kamili wa biashara za Utumwa, tukawasahau wazee walioshiriki kuupata Uhuru wetu ambao kesho ktk sherehe hizi tunatakiwa kuwatunukia tunu za Ushujaa..

Jamani Watanzania wenzangu, kwa mara ya kwanza tuwe na roho ya kitajiri maana umaskini huja na mengi. Leo hii hata Mwenge umepoteza maana yake kabisa kwa sababu wananchi wameshindwa kuikubali hali halisi na hivyo mwenge unawakumbusha machungu tu. Wanafikiria gharama ya kuutembeza Mwenge lakini hawataki kupunguza posho zao wala kuacha mashangingi yao. Wanafikiria gharama za Mwenge lakini watazame ktk maharusi wakinunua pete za mamillioni zenye vito vinavyopatikana ndani ya ardhi yao. Wasifikirie haya na jinsi leo tunavyotawaliwa ktk mazingira ya ajabu ajabu lakini haramu kujikumbusha tulikotoka na tunataka kwenda wapi.


Mimi kusema kweli siku hiyo nitasimama na kufanya kitu kama Yoga, yaani nita meditate na kukumbuka nili/tulikotota, kumshukuru Mungu tumefika hapa tulipo japokuwa maskini na tuna matatizo yetu ya ndani... kumbukumbu hii ya Uhuru itanipa ari zaidi kuendelea kudai Haki na UHURU walopigania wazee wangu hata kama umeporwa na jamaa zetu.
Unahoja nzito lakini mjumbe jaribu kufupisha unakumbuka enzi zile za kuandikiana barua na kutuma kwa posta
 
Isitoshe kwa upande wao nchi yao ya Tanzania Bara haipo nchini lakini inashirikiki mashindano ya mpira kwa timu za taifa,pia vilabu vyao kila mwaka vinashiriki mashindano ya vilabu vya soka kwa nchi za Africa mashariki na kati ambapo kwahivi sasa yanga ya Tanzania Bara ndio mabingwa wao.
Coach Salum
Mjumbe kwa taarifa hakuna nchi ya Tanzania Bara inayotambuliwa na FIFA na CAF na kuruhusiwa kushiriki michuano ya kimataifa. Tafadhali acha upotoshaji
 
Waungana katika pitapita zangu nimegundua wana CDM hawafurahi TZ kusheherekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika.
Dalili zimejoinyesha;-

1. Viongozi wao katika ngazi zote kutoshiriki vikao vya maandalizi ya Mwenge wa Uhuru
2. Viongozi wao kushindwa kushiriki kuukimbiza mwenge ulipofika katika maeneo yao; mfano Ubungo (mhe.Mnyika) na Kawe (mhe. Mdee ).
3. Wabunge wao wameshindwa kushiriki katika vikao vya maandalizi ya miak 50 ya uhuru pasipo kutoa udhuru.


Watanzania inabidi tutumia akili ya mbaimbawi tuwahukumu CDM katika masanduku ya kura kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa 2012 na tuwape kichapo kikubwa uchaguzi mkuu 2015. Hawa wamekosa uzalendo, wamebaki kushabikia sera za Mfadhili wao David Cameroon.

Bob Marley alishawahi kusema huko nyuma kuwa "You can fool some people some sometime, but u cant fool all people all the time"
Ingawa si mfurukutwa wa chama chochote, ukweli am still Mtanzania mzalendo. Napenda kukuuliza mtoa mada kwamba:
1. Uhuru wa Tanganyika ipi?
Kwani hakuna serikali yetu ya Tanganyika kwa sababu hatuna wimbo wa taifa wa Tanganyika, hatuna bendera ya Taifa, hatuna Bunge letu. Hii yote nikwa sababu yakuongozwa ni viongozi wanaojua kujilimbikizia mali na si ustawi wa taifa letu. Zanzibar ktk hivyo nilivyotaja vyote vipo sasa huu uhuru wa Tanganyika ni sawa na kufanya birthday party ya marehemu. Hii haingii akilini hata kidogo kwani wanatumia kodi zetu katika mambo yasiyo na msingi wala manufaa kwetu wananchi.
 
TOKA NIONE HEADING YA THREAD HII NILISITA KUIFUNGUA lkn baada ya kuona port zimekua nyingi nikashawishika kuifungua SASA NAJUTA KUIFUNGUA
 
Ni vijana wangapi leo hawajui hatima ya elimu yao baada ya kukosa mkopo na wamechaguliwa tayari na TCU kujiunga na vyuo mbalimbali hapa nchini?
Ni nini hatima ya vijana wanaolandalanda mitaani na kuishia kumaliza sory za viatu wakati hakuna ajira na serikali haina sera za kuwapatia ajira ili kuwawezesha kujipatia mkate wao wa kila siku ila badala yake inafurahi kuwaona wakizidi kuwa ombaomba
Tunasherehekea miaka 50 ya kunyang'anywa rasilimali zetu na wachache wa nchi hii? Ni asilimia ngapi ya watz leo inafaidika na madini pamoja na ardhi ya watz kiwango cha kujisifia.

OMG! rescue us from this calamity called CCM
 
Maneno yako unaonyesha aidha ni mrundi ama una hasira za kukosa kuingia jumba la magogoni mwaka jana. Wewe kama ni mtz, utatembea kifua mbele kutokana na mafanikio ya miaka 50, sikulaumu sana kwa vile umri wako ni mdogo yaliyotokea baada uhuru huoni ni ya kujivunia.

Jaribu kukaa kitako na mama yako muulize kabla ya uhuru wao walizalishwa maeneo gani. Wewe hauna shukrani, UMEZALIWA zahanati, umeshoma shule ya msingi na sekondari bora.

Tujipongeze watz, TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA
 
Unahoja nzito lakini mjumbe jaribu kufupisha unakumbuka enzi zile za kuandikiana barua na kutuma kwa posta
Ni Uvivu huu wa kusoma ndio maana sisi bado maskini na unaskini huo unatokana na uzembe wa kutosoma maelezo marefu. Hivi kweli mnasoma vitabu vyenye kurasa 200 au, sema kweli?.. Nani kati yenu mwenye mazoea ya kusoma kitabu kila siku... sidhani!..hata hivyo, turudi kwenye mada.

Katika kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika (sio Kusherehekea kama mnavyodhania), kwa nini wale woote wanaosema hawatashiriki wasichukue nafasi ya siku hii KUANDAMANA kupinga utawala uliopo? at least fanyeni la maana kuonyesha hisia zenu siku hiyo, lakini kugoma tu kushiriki kuadhimisha siku hiyo hakuwezi kuwaletea sifa yoyote zaidi ya kuwadhalilisha zaidi..

Desember 9 iwe siku ya maandamano nchi nzima mkipinga yoote mnayoyalaaani na ndio iwe siku ya kudai huo UHURU muutakao..
 
alama za taifa la tanzania ni;
1.mwenge wa uhuru
2.wimbo wa taifa
3............
4............
5...............

kwa hiyo kuwa mpinzani siiiiiii kupinga kila kitu.tuheshimu misingi ya utaifa iliyoasisiwa na baba wa taifa hili.

Acha kukariri ndugu' hakuna kisichobadirishwa' ukiwaza vizuri utangundua kuwa Mwenge unatumia pesa nyingi za walalahoi huku ukiwa hauna faida yoyote!
 
Back
Top Bottom