Ndachuwa
JF-Expert Member
- Mar 8, 2006
- 6,271
- 4,544
Pamoja na mafanikio ambayo Chadema imeyapata katika uchaguzi wa mwaka huu 2010, bado CHADEMA kama ilivyo CUF kinakubalika sehemu moja ya upande wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kukubalika huku upande mmoja wa Muungano pekee kutawafanya washindwe kuunda serikali inayoshirikisha pande zote za Muungano hata kama watashinda uchaguzi mkuu. Tofauti na ilivyo nchi jirani ya Kenya, hakuna uzoefu wa kuunganisha vyama ili kufikia malengo ya kutwaa dola haraka.
Kwa mwenendo wa kukubalika kwa vyama vya CUF na CHADEMA kimoja visiwani na kingine bara, endapo vyama hivi vingeungana chama ambacho kingezaliwa kingekuwa na ushawishi mkubwa visiwani na bara na hivyo kuwa chama mbadala.
Ni bahati mbaya kwa CHADEMA kwamba CCM visiwani wameshachukua hiyo fursa na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na CUF kule visiwani. Hii inaifanya CHADEMA kukosa chama makini kinachokubalika visiwani ambacho ingeweza kuungana nacho ili kuweza kupenya kwenye siasa za visiwani. Hata hivyo kwa kuwa uchaguzi wa 2010 umekwisha, CHADEMA kama chama inabidi kitafakari sana kura ilizoambulia visiwani na mikoa ya pwani na kuchukua hatua madhubuti kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa 2015.
Mojawapo ya hatua inayoweza kuchukua ni pamoja na kuunganisha nguvu na moja ya vyama vilivyoshiriki uchaguzi chenye ushawishi katika siasa za visiwani hata kama hakikuambulia jimbo lolote.
Chama kama Jahazi Asilia tayari kina mtandao wao visiwani wakiungana na CHADEMA na kupata uzoefu wa huku bara wanaweza kutoa upinzani visiwani na kuifanya CHADEMA kuweza kuingia visiwani na hivyo kuonea Tanzania nzima tofauti na hivi sasa ambapo kipo tu huku bara.
Kukubalika huku upande mmoja wa Muungano pekee kutawafanya washindwe kuunda serikali inayoshirikisha pande zote za Muungano hata kama watashinda uchaguzi mkuu. Tofauti na ilivyo nchi jirani ya Kenya, hakuna uzoefu wa kuunganisha vyama ili kufikia malengo ya kutwaa dola haraka.
Kwa mwenendo wa kukubalika kwa vyama vya CUF na CHADEMA kimoja visiwani na kingine bara, endapo vyama hivi vingeungana chama ambacho kingezaliwa kingekuwa na ushawishi mkubwa visiwani na bara na hivyo kuwa chama mbadala.
Ni bahati mbaya kwa CHADEMA kwamba CCM visiwani wameshachukua hiyo fursa na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na CUF kule visiwani. Hii inaifanya CHADEMA kukosa chama makini kinachokubalika visiwani ambacho ingeweza kuungana nacho ili kuweza kupenya kwenye siasa za visiwani. Hata hivyo kwa kuwa uchaguzi wa 2010 umekwisha, CHADEMA kama chama inabidi kitafakari sana kura ilizoambulia visiwani na mikoa ya pwani na kuchukua hatua madhubuti kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa 2015.
Mojawapo ya hatua inayoweza kuchukua ni pamoja na kuunganisha nguvu na moja ya vyama vilivyoshiriki uchaguzi chenye ushawishi katika siasa za visiwani hata kama hakikuambulia jimbo lolote.
Chama kama Jahazi Asilia tayari kina mtandao wao visiwani wakiungana na CHADEMA na kupata uzoefu wa huku bara wanaweza kutoa upinzani visiwani na kuifanya CHADEMA kuweza kuingia visiwani na hivyo kuonea Tanzania nzima tofauti na hivi sasa ambapo kipo tu huku bara.