mgeni wenu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 3,664
- 1,730
Apeleke maji na barabara huko kwake naskia hawamtaki
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Mahusiano Stephen Wassira amesema chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kitakumbwa na mgogoro mkubwa ndani ya kipindi kifupi kijacho.Wassira amesema mgogoro huo ndio utakaopelekea kusambaratika vibaya chama hicho na kubaki historia hapa nchini.Amesema mgogoro huo utahusiana na Uongozi na kuwaomba wananchi wavumilie kidogo ili washuhudie anachokisema.
Wassira amesema CDM ni chama cha hovyo na cha ajabu kilichojaa ubinafsi wa hali ya juu.Amesema CDM kimekuwa kikipinga kila kinachofanywa na serikali ya CCM na kwao CDM hakuna zuri la CCM tangu uhuru wa Taifa hili.
Source:Majira Jumapili.
Kumbe ni huyu tahira kasema simwamini hata kidogo labda angesema makufuli ndio ningeamini
Bado yuko usingizini na ndotoni angelipewa wizara ya usingizi na vyandarua vya kuzuia malaria
View attachment 54225
Hivi yule waziri wa maliasili na utalii hajaanza kazi rasmi!!? Mbona harudishi wanyama waliotoroshwa mbugani na kupelekwa ikulu eti wazungu wasipate tabu ya kwenda maporini!!?
ukisoma zile stages za mtu anaekaribia kufa mojawapo kati ya zile signs inaonyesha kitu kinachoitwa DENIAL yaani unakataaa na hutaki kukubali kwamba sasa unakufa, unaamini kwamba utapona tu na utarudi na kuendelea na majukumu yako, ndio utaskia mgonjwa anasema nikipona tu ntamalizia ile nyumba yangu, kisha hali inafikia mahali unaingia kwenye ACCEPTANCE, sasa naona huyu DINGI yeye yuko kwene stage ya DENIAL anaamini kuwa CCM inapitia ugonjwa flani na itapona na kuendelea kutawala ila nashukuru pia baadhi yao wamekubali (ACCEPTANCE) kuwa sasa CCM inakufa ndio maana wanataka RECONCILIATION (SP) na wananchi, ntaendelea baadae ngoja nipate komunio kwanza
Kauli kama hizi ni kero kwetu wanachama hai wa NCCR, sisi hatujabaki historia tupo na tunaendelea kuwepo. Maneno yenu mengine yanatukosea adabuHuenda alishatega timing bomb huko CDM na anaona linakaribia kulipuka! Haya mambo ya siasa magumu kweli. Watu hatukuamini kama NCCR ingesamabaratika na kubaki historia. Nikikumbuka NCCR ya 1993 ikaja ile ya Mrema ya 1995 na kisha ukaja ule msambaratiko wa Tanga naogopa. Nikikumbuka akina Marando, Selasini na Komu kuwa walikuwepo Tanga siwezi kusema kitu hadi tufike 2015 na kuipita CDM ikiwa salama.
like,,,,,,,mkizungo like dis:spy:Huenda alishatega timing bomb huko CDM na anaona linakaribia kulipuka! Haya mambo ya siasa magumu kweli. Watu hatukuamini kama NCCR ingesamabaratika na kubaki historia. Nikikumbuka NCCR ya 1993 ikaja ile ya Mrema ya 1995 na kisha ukaja ule msambaratiko wa Tanga naogopa. Nikikumbuka akina Marando, Selasini na Komu kuwa walikuwepo Tanga siwezi kusema kitu hadi tufike 2015 na kuipita CDM ikiwa salama.
wewe na wasira mnashabihiana sanaWasira ni mtu makini sana kwa kiasi kikubwa ndio aliofanikisha ziara ya Chadema Ikulu kwenda kuonana na Rais Kikwete, anachosema siwezi kukataa ni suala muda tu...kuna mitengo yake kaitenga ndani ya Chadema, hata kule Mwanza ni mkono wake.