Chadema kumfikisha mahakamani Nape Nnauye

Mahakama ipi atakayokwenda? Nina wasiwasi wa kesi ya nyani kuhukumiwa na ngedere.

Tusife moyo. Kuna watendaji wazuri tu katika mahakama zetu. Mifano ipo kama wabunge wa CDM kushida kesi za uchaguzi kupitia vyombo vyetu vya mahakama. Mungu yupo atawainua wenye kutetea haki katika nchi yetu inayoelekea kubaya.
 
Mkuu, Katika siasa, ukweli na uongo vyote hutumika, ili mradi kuvuta hisia za jamii ambao ndio mtaji wa chama kisiasa. Hata chama chenu, si yote wasemayo ambayo ni kweli. wamekuwa wakitumia madhaifu machache ya kiutendaji ili kuvuna wanachama wengi, ambayo hata kama leo wangeingia madarakani, si rahisi kutimiza matazamio wanayowatazamisha jamii. Hii ndiyo maana tunaita kuwa siasa ni gamba gumu, kwa kuwa ni lazima uvumilie kusikia maneno mazito. Hii ndiyo inayo weza kutofautisha mwanasiasa aliyekomaa na mwanasiasa anayejifunza. Kisiasa, mahakamani huwa hatuendi ila tunaenda kwa wananchi. anayekimbilia mahakamani ni mwanasiasa uchwara. hivyo usikimbilie kuona kama mwenzenu karopoka, ila hiyo ndiyo siasa

Ndio siasa mufilisi ya CCM.

Siasa ya majitaka inapozidi ni lazima hatua zichukuliwe.

Uongo umekuwa ni mtaji wa CCM kisiasa, na uongo ndio utakaoiangusha CCM kisiasa.

Mwanasiasa aliyekomaa ni yule anayepima vema matokeo ya maneno yake! Ni yule ambaye si mwoga kukabiliana na matokeo ya kauli zake.

Mwanasiasa mahiri anajua kuutumia vema udhaifu wa mpinzani wake kwa faida yake. Udhaifu wa kuropoka na uongo, sasa utakula kwenu.

Mwanasiasa mwadilifu na raia mwema kamwe haogopi mahakama!
 
Hii hatua inawafurahisha sana wale wote wanaojali mustakabli wa nchi yetu. Hakika CDM mnaonyesha njia kwamba mnajitahidi kukarabati jamii yetu kurudi kwenye ukweli katika mfumo wa kistaarabu. Nape hana hamu
 
Tusife moyo. Kuna watendaji wazuri tu katika mahakama zetu. Mifano ipo kama wabunge wa CDM kushida kesi za uchaguzi kupitia vyombo vyetu vya mahakama. Mungu yupo atawainua wenye kutetea haki katika nchi yetu inayoelekea kubaya.

Kwa vyoyote Nape ana wakati mgumu. Kutoa ushahidi mahakamani kuwa Chadema watauza nchi ni kitu ambacho ni vigumu sana kuithibitishia mahakama 'beyond any shadow of doubt.'
 
na nyie chadema bwana, mnahangaika na domo kaya lile? hebu asiwapotezee muda wa kufanya mambo ya msingi achaneni naye aendelee kugombana na EL wake
 
Ningeshauri muachane na nape, mtaaibika bure. Mnyika my brother huenda hii issue ndani ya chama chako huijui ndo maana unakurupuka. Nakuhakikishia kwa hili nepi atawaaibisha. Dili nzimz anaifahamu mbowe na lema nyie wengine bendera tu. Kama unabisha, komaa na nape mwiho wake zigo utabaki nalo peke yako.
 
mimi nataka kusikia ameshafikishwa mahakamani basi hizi taarifa zingine hatuhitaji CDM tufanye mambo kwa vitendo tuache maneno mengi!!
 
Ningeshauri muachane na nape, mtaaibika bure. Mnyika my brother huenda hii issue ndani ya chama chako huijui ndo maana unakurupuka. Nakuhakikishia kwa hili nepi atawaaibisha. Dili nzimz anaifahamu mbowe na lema nyie wengine bendera tu. Kama unabisha, komaa na nape mwiho wake zigo utabaki nalo peke yako.
Nafikiri CHADEMA kupitia mheshiwa mnyika wako sawa kwenye hili. Nape alikataa kutoa ushahidi akisema anakumbuka muda muafaka ufike ndo amwage data nakumbuka aliyasema haya wakati akihojiwa na Fina Mango. Nafikiri wakienda mahakamni ukweli ndo utajulikana,,,, so usiwatishe CHADEMA kutumia haki yao ya kikatiba mkuu
 
Siyo mara ya kwanza Nape kuropoka wakati wa kesi ya ubunge Arusha aliwaambia wajiandae kwa ajili ya uchaguzi mwingine alipoitwa mahakamani ili afafnue kauli yake alisingizia anaumwa kama mwenzake Magufuli mwenzake Mwigulu Nchemba huwa analopokea bungeni akijua analindwa na kanuni za bunge tumechoka na siasa za mipasho waende mahakamani ili iwe fundisho
 
na nyie chadema bwana, mnahangaika na domo kaya lile? hebu asiwapotezee muda wa kufanya mambo ya msingi achaneni naye aendelee kugombana na EL wake

Hapa Issue sio kuhangaika nae koz alishaongea saana... Ila impact ya alichoongea ndo inahuiska sana...So inabidi aombe radhi au athibitishe.
 
CHADEMA kimemtaka katibu mwenezi wa CCM Nape Nnauye kukiomba radhi chama hicho ndani ya siku saba na kulipa fidia ya shilingi bilioni tatu baada ya kudai kuwa chama hicho kinawahadaa watanzania kwa kuchangisha fedha huku kikiwa na mabilioni ya fedha kutoka nje ya nchi.


video kwa hisani ya ITV TANZANIA ya youtube
 
Last edited by a moderator:
cdm ni chama makini. hizi tuhuma za nepi mahala pa kwenda kuzidhibitisha ni kwa jaji tu pale high crt. hii itakuwa ni fundisho kwa wote wanaoropoka hovyo km walivofanywa kina magufuli,alshabaab rage,mkapa na mukamb kule igunga.
 
[/SIZE][/COLOR]TUMBIRI (PhD - In Progress at HULL, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(UDSM), PCM(Mzumbe High School - 2[SUP]nd[/SUP] Overall Best Student in Form six National Exams).
tumbiri@jamiiforums.com[/QUOTE]

Unataka kuwa kama prof.luhanga!
Ngoja na mimi niweke ya kwangu,st.kanumba secondary ( HGE),BCOM(UDSM), CPA(T).Historia inaonyesha majiri wengi dunian hawana elimu kubwa na wengi walikatisha masomo mfn.bill gates, founder wa facebook etc.sijua ni kwa nini wasomi wakubwa (wenye masterz, phd, prof) hawapo kwenye list ya matajiri wakubwa dunia
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom