CHADEMA Kuitikisa Nyanda za Juu Kusini; Safari Kuanza kesho

Wana JF.

Heshima kwa wote.

Ile Ziara ya Maandamano ya Nyanda za Juu Kusini imewadia.Maandalizi yanaendelea vizuri na kesho ndio msafara unaoondoka kwa Convoy kuelekea Mkoani Mbeya.

Maandamano yenyewe yatazinduliwa Mbeya Mjini Siku ya Ijumaa tarehe 6 Mei, tunatarajia kufanya Ziara kwenye Mikoa ya Mbeya,Rukwa,Ruvuma na Iringa respectively.

Mkoa wa Morogoro tumeuondoa kwa sasa kwa kuwa kuna mvua nyingi na sehemu nyingine kuna mafuriko hivyo hatutaweza kufika maeneo yote, Morogoro tutakwenda baada ya Bunge la Bajeti.

Maandamano hayo kuongozwa na Viongozi Wakuu wa Chama. Makamanda Mbowe, Dr Slaa, Zitto na Arfi tukifuatiwa na Wabunge, Watendaji Makao Makuu, Viongozi wa Mikoa, Wilaya na Majimbo.

Ziara inatarajiwa kuwa ya Siku 12 kila Mkoa ni siku tatu.

Kama kawaida nitajitahidi kuwahabarisha kila kitakachojiri kadiri ya uwezo wangu.
Nitaanza na Msafara wa kesho.

Aluta Continua

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Nina wasiwasi na Maandamano kama ndio njia sahihi ya Kujenga Chama. CCM wana Ofisi kila kata na kijiji, pamoja na daftari la wanachama, na mabalozi wa nyumba kumi. Mzingatie hayo kwanza, na mabadiliko ya Katiba yatakayotupa Tume Huru ya Uchaguzi. Vinginevyo, mtajachakachuliwa tena 2015...
 
Tunawatakia kila la kheri katika safari ya kukijenga chama. ila naomba msisahau kufungua matawi kote kote, alikeni wanachama wapya. natumai habari kubwhuko itakuwa ni kutueleza wanachama wapya kwa maelfu wamejiunga. chooonde chonde...........
 
Usisahau kutuwekea picha. Kule Mwanza tulikudai picha sana hukutuwekea inawezekana hukuwa na kamera. Picha pia huzungumza sana wakati fulani hata kuzidi maneno. Kabla hamjaondoka tayarisha kabisa kamera.

Hakika mama Regia kila la kheri , wakati wanajivua gamba nyinyi kamueni
 
Try to act like an MP...jaribu kujenga hoja na kutetea hoja kama mh.Lissu,Zitto,Lema n.k maana nimekuwa nikisoma majibu yako mengi umekuwa haukosoleki..may b bado mchanga kisiasa na ndo kwanza unapata exposure ya siasa za kitaifa..sio kila anayekosoa haipendi Cdm..fanyia kazi.

Hoja hujibiwa kwa hoja, ikiwa ww hukutoa hoja ulitegemea kupata hoja gani.
Labda ungeonyesha kwanini style wanaitumia CDM haina matokeo kwa uchunguzi ulioufanya pia ungependekeza njia au style nyingine ambayo unaona yafaa lakini ukisema kijuuju hapo hakuna hoja my bro.
 
Kila la kheri, jitahidini kusisitizia mambo yote ya msingi esp tatizo la mfumuko wa bei, mishahara midogo ya watumishi wa umama etc. Pamoja sana
 
Kila la kheri wapiganaji! Mimi ningeyachukulia haya maandamano na mikutano yake kama mikutano ya injili. Kila baada ya mahubiri watu hupewa nafasi ya kutubu na kuja kwa Yesu. Hamwezi kufanya kitu kama hiki na hata baada ya hapo viongozi wa maeneo hayo wawafatilie hao wananchama wapya na kuendelea kuwaelimisha zaidi? Tunahitaji kupata watu huko vijini ili waanze kuenenza habari hii njema kwa kila kaya. Viongozi wa kitaifa hamtaweza kufika hadi kijijini

Kwa mara nyingine kila la kheri na Mungu awatangulie na iponye safari yenu !
.
 
Regia & cdm co,
Nawatakia kila la heri katika msafara wenu Nyanda za juu kusini.
Nisalimieni Bwana Shitambala Sambwee huko, sijui atajibeba na Mbeleko gani!
Kuweni makini na kijana huyu...si mtu mzuri hata kidogo, na najua atajaribu kuwakwamisha!
 
Wana JF.

Heshima kwa wote.

Ile Ziara ya Maandamano ya Nyanda za Juu Kusini imewadia.Maandalizi yanaendelea vizuri na kesho ndio msafara unaoondoka kwa Convoy kuelekea Mkoani Mbeya.

Maandamano yenyewe yatazinduliwa Mbeya Mjini Siku ya Ijumaa tarehe 6 Mei, tunatarajia kufanya Ziara kwenye Mikoa ya Mbeya,Rukwa,Ruvuma na Iringa respectively.

Mkoa wa Morogoro tumeuondoa kwa sasa kwa kuwa kuna mvua nyingi na sehemu nyingine kuna mafuriko hivyo hatutaweza kufika maeneo yote, Morogoro tutakwenda baada ya Bunge la Bajeti.

Maandamano hayo kuongozwa na Viongozi Wakuu wa Chama. Makamanda Mbowe, Dr Slaa, Zitto na Arfi tukifuatiwa na Wabunge, Watendaji Makao Makuu, Viongozi wa Mikoa, Wilaya na Majimbo.

Ziara inatarajiwa kuwa ya Siku 12 kila Mkoa ni siku tatu.

Kama kawaida nitajitahidi kuwahabarisha kila kitakachojiri kadiri ya uwezo wangu.
Nitaanza na Msafara wa kesho.

Aluta Continua

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

.
Msiache kuchukua tahadhari zote za kiusalama hasa wakati wa kusafiri. Mafisadi mliowataja ndani ya chama cha magamba kimsingi wameshathibitishwa kufa, hivyo watajaribu kutumia kila nafasi itakayopatikana kushuka kuzimu na ninyi wahasimu wao wa kisiasa.
KUNYANGANYWA TONGE MDOMONI AMBALO TEZI ZIMESHALITENGENEZEA MATE YA KULIMEZA SII MCHEZO!!
.
 
.
Msiache kuchukua tahadhari zote za kiusalama hasa wakati wa kusafiri. Mafisadi mliowataja ndani ya chama cha magamba kimsingi wameshathibitishwa kufa, hivyo watajaribu kutumia kila nafasi itakayopatikana kushuka kuzimu na ninyi wahasimu wao wa kisiasa.
KUNYANGANYWA TONGE MDOMONI AMBALO TEZI ZIMESHALITENGENEZEA MATE YA KULIMEZA SII MCHEZO!!
.

Kweli jamani muwe na tahadhari katika kusafiri. Ulinzi na usalama ni muhimu
 
Mh Regia Tunasubiri kwa ham kubwa sana, hii ziara ya nyanda za juu
 
Kila la heri Cdm! Acha watalii na kuzurura nje ya nchi sie tunatwanga kotekote!
 
...........Nadhani baada ya hawa jamaa wa kujivua gamba kuzunguka nchi nzima kuwadanganya watanzania juu wa falsafa yao,sasa tunaingia watu makini wenye uchungu na nchi hii kuwaeleza watanzania ukweli wa mambo...Naomba hawa jamaa na watu wa intelejensia wawe makini waone watanzania tulivyo makini kwasasa..hatudanganyiki ng'o....Bravo CHADEMA..
 
Mhe.Regia,tunashukuru sana kwa taarifa njema.Karibuni sana makamanda katika mkoa wetu wa Njombe.
Sisi makamanda wa Njombe tumejipanga kuwapokea kwa shangwe kubwa.Hapa Njombe ni jimboni kwa bibi mkora hivyo kazi itakuwa nyepesi sana.kila mtu amechoka.hapa Njombe pia ni mahala ambapo kuna mbunge ambaye amevunja rekodi ya kuingia bungeni kwa kuto kujua kusoma na kuandika.Wizi mtupu.
karibuni sana makamanda mje mtukomboe wenzenu vanyalukolo.
Huko ndiko kuliko na makamanda maarufu kama Thomas Nyimbo,Nyagawa,Lulandala na makamanda wengi wenye uchu mkubwa wa kuhakikisha CCM inafutika katika ramani ya nchi ya wabena,wakinga na wapangwa.
Mtapata mapokezi makubwa kuliko wakati mwingine wowote mliowahi kufika Njombe.:bange:
Ukweli mtupu Kamanda Lutondwe. Tutahakikisha CCM inafutika Njombe watake wasitake
 
Siasa za kitaifa unamaanisha nini?MP wakoje?Siwezi kupretend kufanya kama unavyotaka wewe.I like the way iam and am proud to be the way iam.Kwa kweli nimeyafurahia sana majibu
yangu yaleo kwa wote mliokatisha mbele yangu.Unajingine?
<br />


Una mme?Pengine angekuwa akikupoza na kukupa busara za kisiasa.Nitakutafuta,maake naona kama unanifaa.
 
Hongera dada Regia mtema na CDM yote kwa moto huu munaoupeleka nyanda za juu kusini. Ila musisahau kwenda wilaya ya Tunduru,pale ccm ilishajifia siku nyingi sana ila huwa wanashinda kiti cha ubunge kwa wizi tu. Tunduru ilikuwa ngome ya CUF,ila baada ya kufa mpiganaji wao Mazee....inaonekana wananchi hawajajua wahamie chama gani, So kama mtaenda huko Tunduru am sure mtapokelewa vizuri sana na mtapata wanachama wengi sana....Nawatakieni safari njema na yenye mafanikio mema
 
Karibuni sana Mbeya Mh Regia na makamanda wetu wote. Asanteni sana kwa kuendelea na kazi ngumu ya kutufumbua macho watanzania. Tunawahitaji sana. All the best.
 
We wish you the best. Your success is our success. The future of Tanzania depends on CHADEMA succeeding in its efforts to awaken the masses of our people from the deep slumber that has been induced on them by many years of misrule by CCM.

Mheshimiwa Regia lazima nikuulize swali moja: Wewe ni Waziri Kivuli? Hii maana yake ni photocopy ya waziri! Unapashwa kuitwa Waziri Mbadala wa Kazi na Ajira (yaani Alternate Minister for Labour and Employment), na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom