CHADEMA kufanya Maadhimisho Makubwa ya Miaka 20 ya Kusajiliwa Kwake

Mtanke

JF-Expert Member
Nov 19, 2011
712
1,771
Wenyeviti na Makatibu wa Mikoa wa CHADEMA Tanzania wameadhimia kwa kauli moja kuwa Chama kifanye maadhimisho makubwa ya kusajiliwa kwake. Viongozi hao waliokuwa Wilayani Karagwe Mkoani Kagera kwa ajili ya semina ya kuwajengea uwezo pamoja na Operesheni M4C katika Wilaya ya Karagwe na Bukoba walitoa maazimio hayo wakati wa majumuisho ya semina yao.

CHADEMA iliasajiliwa rasmi tarehe 19 July 1993 hivyo kutakuwa na mwezi au wiki ya CHADEMA ambapo Chama kitafanya shughuli mbalimbali za kijamii na za kujitolea ikiwa ni pamoja na mashindano ya kitaaluma kwa wanafunzi wa Sekondari na vyuo mbalimbali, usajili wa wanachama wa wapya, Makongamano n.k. Kilele cha sherehe hizo kitakuwa ni tarehe 19 July 2013.
 
maadhimisho sio sera ya UFISADI ya CCM?

Yes, rejea adhimisho la miaka 50 ya uhuru na kashifa ya matumizi makubwa ya fedha za walipa kodi. Ila CDM wanakuja na stayle mpya yenye ubunifu mkubwa kwa faida ya watanzania-ni siku ya kujitolea, kuibua vipaji kupitia nashibdano ya shule and the like. Mambo haya yanaigika-ccm wanaweza kufanya hivyo pia.
 
ijapokuwa CCM hawasemi hadharani ila moyoni wanatamani kuwa CDM,hii nayo wataiga,heko makamanda ...constructive mission!
 
Hapo ndipo unapooneka ubunifu wa makamanda siyo kuwa bendera fuata upepo.kama wale wa upande wa pili.
 
Wiki 2 za mwanzo toka Jula1 hadi Julai14 ziitwe "SIKU 14 ZA TAFAKARI YA UZALENDO". Wiki ya tatu yaani toka Julai15 mpaka Julai19-2013 iitwe "WIKI YA TUMAINI JIPYA KWA WATANZANIA". Napendekeza kuwa Tarehe 19 julai 2013 M/Kiti CDM Taifa awatangaze MASHUJAA WAPYA WA TZ, yaani wale wote waliouawa na POLISICCM maeneo mbalimbali nchini wakidai, wakitetea na kupigania haki AU wakitekeleza majukumu yao halali. Mfano Wenzetu waliouawa SONGEA, IGUNGA, IRINGA(Mwangosi), ARUSHA, MOROGORO(Ally Zona), MWANZA, ARUMERU MASHARIKI nk. Pia kutolewe kauli nzito juu ya kufungiwa GAZETI LA MwanaHALISI.
 
Back
Top Bottom