CHADEMA Kuchagua Siasa: Plan "A" Vs Plan "B". (Hakikisha unapitia kwa makini.)

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Salaam ndugu zangu,

Naomba mtu asichangie kama hajasoma.
Mnaokumbuka, toka awali nilisema nitakuwa nikitoa ushauri tu kwa CHADEMA na sina nia ya kugombea nafasi yeyote.Hata hivyo mara zote nikishauri kitu tu nimekuwa nikishambuliwa kwamba nimetumwa.Sasa leo nawaletea Plan "A" na plan "B" na nijukumu la kila mtu kufikiri na kuchagua mwenyewe.

Kwenye taasisi ya kisiasa ni lazma kwanza ijengwe na nadharia za kifalsafa juu ya muelekeo wa kifikra wa ndani (internal philosophical paspective) halafu ndio ichague falsafa za nje (sera, mikakati dhidi ya vyama vingine n.k).

Jaribu kupitia Mitizamo ya aina ya siasa za Ndani ambayo CHADEMA inaweza kuchagua na kujijenga katika mtizamo mmoja ikijua wazi ni nini kinachotarajiwa mbeleni.


PLAN "A "
MTIZAMO WA VIONGOZI WA JUU WA CHAMA
MTIZAMO


FAIDA
CHANGAMOTO

Kuhodhi fikra na kujenga utiifu wa woga kwa viongozi wa chini na wafuasi kwa kuwashughulikia wenye fikra tofauti

Kujenga chama chenye utiifu wa hali ya juu kwa viongozi wa kuu,utiifu unaowafanya wasihoji wala kuchunguza jambo na hivyo kuleta utulivu wa kifikra kwa Viongozi.Wanachama/viongozi wa kati na chini , kuwa na dhamira mbili zinazopingana.
(a)dhamira ya nje inayolenga kuonesha utiifu wa hali ya juu kwa kuyakubali yote yanayosemwa na wakubwa 100%
(b) dhamira ya ndani inayosukumwa na mawazo na imani binafsi ya muhusika.
-Kwa ujumla kuishi katika mazingira ya unafiki.
AINA YA VIONGOZI WA NGAZI YA KATI
MTIZAMO

FAIDA CHANGAMOTO
Wenye elimu ya kati au ndogo, wasio sukumwa na fikra huru, wasio wabunifu, wasioweza/penda kutafiti mambo na wanaofanya kile wanachoelekezwa tu.Hawatahoji mapato wala matumizi,hawataanzisha ajenda, wala hawatalalamikia jambo hadharani.Hii itasaidia kuwapunguzia viongozi wakuu msongo wa mambo na kujikita katika kukabiliana na wapinzani wa nje tu.

-Itaepusha hali ya kudhaniana kwamba wahusika wametumwa na CCM n.k
-Itachochea ukiritimba wa fikra ndani ya taasisi kutoka miongoni mwa watu wachache
-kudumaa kwa fikra miongoni mwa wadau na watendaji
-kudumaa kwa ukuaji wa taasisi kwa ndani.
-wadau kukaa na duku duku moyoni
-Kuibuka kwa migogoro mizito mizito
AINA YA WASHAURI WA CHAMA
-Wasiwe wataalam/wasomi waliobobea kwenye fani husika -wasioheshimu ukweli "Facts" na wanaosema kile ambacho kinaweza kufurahisha viongozi tu-Watakuwa wakiwafariji viongozi hasa wakati wa misuko suko inayotokana na upinzani wa nje


-Watakuwa wakiwatia moyo viongozi na hivyo kupata ari zaidi.
-Daima hawatasema ukweli
-daima hawatatumia taaluma na uzoefu wao
-Watawalewesha sifa viongozi wa chama
-Wataua Chama.
MBINU ZA UENEZI WA CHAMA

Utumiaji wa Propaganda safi na chafu kama mbinu kuu ya ueneziWatapatikana waungaji mkono na washabiki wengi hasa vijana wa kiume.-chama kitapoteza uungwaji mkono kutoka kwa wasomi walio wengi.
-Chama kitapoteza uungwaji mkono kutoka kwa watu wanaofikiri na kuchambua mambo.
-chama kitapoteza uungwaji mkono kutoka kwa watu wanaopenda siasa za kistaarabu.
-watakaokiunga mkono chama, wanaweza kubadili fikra masaa24, kabla ya uchaguzi kwa kuwa hawana msingi imara wa kusimamia zaidi ya emotions.
UHUSIANO KATI YA CHAMA NA TAASISI NYINGINE
Kujenga uadui na uhasama na taasisi nyengine nje ya chama chenyewe.Taasisi nyengine zitakiogopa chama na hivyo ni vigumu kuingilia shughuli za chama
-Taasisi nyingine zitaogopa kushirikiana na chama kwa kuhofia kutuhumiwa
-Hazitatoa ushirikiano mwema wakati wa uchaguzi (kwa roho safi)
-Chama kikishika dola kitashindwa kuiongoza serikali.
UFUAJI WA VIJANA NDANI YA CHAMA
Kuandaa vijana watiifu na wanaowashabikia viongozi wao kwa 100%Viongozi wa chama watapata hamasa kubwa kufanya kazi wakiwa wana matumaini makubwa
Kutakuwa na kundi kubwa la viongozi/vijana ndani ya chama wasio na uelewa wowote katika uongozi; vijana wasio na fikra pembuzi.
AINA YA AJIRA YA WATUMISHI NDANI YA CHAMA
Ajira za muda mfupi na kujitolea
Fedha kidogo tu itatumika
-Ni rahisi watumishi hao kubadilika badilika kutokana na kutokuwa na uhakika wa maisha yao.
-ni rahisi watu hao kurubuniwa na kufanya kazi binafsi.
RASILIMALI NA UCHUMI/UTUMIAJI WA FEDHA.
Kuwekeza katika operesheni fupi fupi zinazokatika.Mf.Kulipia mkutano hotelini, kukodi vifaa n.k-Haina haja ya kutumia akili nyingi katika utekelezaji.

-inafaa sana kama wahusika hawana uhakika juu ya kesho yao
Kutumia fedha nyingi bila mipango endelevu na kusababisha uwepesiwa taasisi "org fragility"

===================================================
PLAN "B" INAFUATA HAPO CHINI
 

PLAN "B"

MTIZAMO WA VIONGOZI WA JUU WA CHAMA
MTIZAMO​
FAIDA​
CHANGAMOTO
Kuruhusu uhuru wa hali ya juu wa mawazo lakini kuheshimu kanuni vile vile

Kujenga chama chenye domokrasia ya kweli kweli na yenye nguvu
Kuibuka kwa minyukano ya kifikra ya ndani kwa ndani (ambayo inaweza kusababisha wenye hoja dhaifu kuchukia)
AINA YA VIONGOZI WA NGAZI YA KATI
MTIZAMO

FAIDA
CHANGAMOTO
Wenye elimu kubwa ,wabunifu na wanaohoji na kufikiri kisomi hasa.

Watahoji,kukosoa na kushauri kila inapobidi na watafanya hivyo kwa kutumia hekima "Professional ethics"
Wakati mwingine Wanaweza kuonekana ni watovu wa nidhamu, wametumwa kupinga,ni wachokonozi, ni wanoko n.k

AINA YA WASHAURI WA CHAMA
Wenye weledi wa kutosha, fikra pevu,watafiti na wanaosema kweli daima

Watakuwa wanaongea na kushauri vitu halisia "Facts" ,KITU AMBACHO NI CHA MUHIMU SANA KATIKA KARNE HII YA 21.
Wanaweza kuonekana kwamba ni kikwazo hasa pale watakapofikiri na kupendekeza jambo ambalo litagusa masilahi ya mtu binafsi.
MBINU ZA UENEZI WA CHAMA
Utumiaji wa hoja nzito,tafiti maridhawa, vielelezo thabiti na ushawishi wa busara pamoja na propaganda safi.

-Kupata uungwaji mkono kutoka kwa wasomi, watu wanaopenda siasa za kistaarabu, wenye fikra pevu pamoja na watu wa kawaida.
-kupata wafuasi wa kudumu waliojikita katika misingi imara inayoeleweka.
Ili kutumia mbinu hii kwa ufanisi, inahitaji muda wa kutosha , watu wenye uwezo mkubwa na nia njema.
UHUSIANO KATI YA CHAMA NA TAASISI NYINGINE
Kujenga uhusiano mwema na vyama/taasisi nyingine

Kupata ushirikiano na uungwaji mkono kutoka taasisi/vyama vingine na hata kuweza kupata ushirikiano kama chama kikishika dola na hivyo kuweza kuunda serikali.
Uwepo wa watu wenye chuki na watu wa taasisi nyengine zote isipokuwa chama chao tu.
.
UFUAJI WA VIJANA NDANI YA CHAMA
Kuandaa vijana wapembuzi,wadadisi,watundu lakini waadilifu na wenye hekima

Kuandaa viongozi wanaoweza kumudu mikikimiki ya kiuongozi katika karne ya 21.
-Uwepo wa vijana wanaopenda ushabiki zaidi ya kitu kingine chochote
-Uwepo wa wanasiasa wanaopenda kuwatumia vijana kwa maslahi yao binafsi
AINA YA AJIRA YA WATUMISHI NDANI YA CHAMA
Ajira za kudumu

Watumishi watakuwa na utulivu wa nafsi na hivyo kufanya kazi kwa moyo mmoja
-Gharama kubwa itatumika kulipa mishahara.
-Kama kuna kiongozi angependa kuwatumia na ikishindikana kuwatimua atakuwa ni kikwazo.
RASILIMALI NA UCHUMI/UTUMIAJI WA FEDHA.
Kufanya operesheni na mikakati ya muda mtefu.Mf.Kujenga ukumbi wa mikutano badala ya kufanyia mikutano hotelini.

Kutakuwa na utunzaji fedha,kuweka vitega uchumi na kutabiri hatma ya wakati ujao
Inahitaji uamuzi mgumu na malengo ya mbali .
 
I like this well-thought out analysis,It has illustrated constructive & destructive Party building plans so it's up to Chadema's higher echelon of leadership to decide which way to go with.In my opinion the Party is applying Plan A at the moment.This can be good on the side of leaders' personal interests but really bad on the Party's interest side.Plan B is the sure way to go with if we really care about the Party and a Country as a whole.I know it's hard for the devious Politicians to opt Plan B since they will have to deal with very independent & free thinking minds,critical,curious & skeptical audience & very outspoken individuals so i know for sure they will keep sticking with Plan A where there's their friendly audience.So the answer is obvious.
 
I like this well-thought out analysis,It has illustrated constructive & destructive Party building plans so it's up to Chadema's higher echelon of leadership to decide which way to go with.In my opinion the Party is applying Plan A at the moment.This can be good on the side of leaders' personal interests but really bad on the Party's interest side.Plan B is the sure way to go with if we really care about the Party and a Country as a whole.I know it's hard for the devious Politicians to opt Plan B since they will have to deal with very independent & free thinking minds,critical,curious & skeptical audience & very outspoken individuals so i know for sure they will keep sticking with Plan A where there's their friendly audience.So the answer is obvious.
Mkuu TECH WIZ nikujibu kwa kiswahili maana kingereza kinanisumbua kidogo,
Sipendi sana kuzundumzia kwamba kwa sasa CHADEMA imechagua plan ipi kati ya hizi na nawaachia wadau wenyewe watafakari.Hata hivyo taasisi ya kisiasa itakayochagua Plan "A" Kitaalam haiwezi kutoboa katika karne hii ya 21.Kitakachotokea ni kwamba itakuwa ni taasisi isiyotabirika, taasisi inayofuata upepo, mtiririko wa matukio, hizia za watu n.k mwishowe kutakuwa hakuna "Strategist" na watakapotokea hawatapata ushirikiano wa kutosha au mipango yao haitakuwa ikiratibiwa vizuri na hatimae ni kuyumba na kusambaratika.Hii ni kwa taasisi yoyote ile itakayojikita katia plan "A" Katika zama hizi.
 
Last edited by a moderator:
wewe mwenyewe umeshusha theory ndeeeeeefu, ghafla inakuwa soo kuku-check kabla ya kuku-balance, usiwe mwoga, ndo ushalianzisha ivo.
 
wewe mwenyewe umeshusha theory ndeeeeeefu, ghafla inakuwa soo kuku-check kabla ya kuku-balance, usiwe mwoga, ndo ushalianzisha ivo.
Sijui kama nimekuelewa.Kuhusu urefu, ili kitu kiweze kuwa kamili na kuleta maana wakati fulani inabidi kiwe kirefu kidogo.Tatizo ni kwamba vizazi vya siku hizi havipendi kusoma na ndio maana unaona mtu anakurupuka anacomment bila hata kusoma.
 
betlehem
Nimekusoma ndugu yangu na kwa ulivyo viandika ni MAJI na MAFUTA haviwezi kuenda pamoja hata siku moja.

Na nionavyo mimi PLAN A ni CHADEMA ya sasa na PLAN B ni chama ambacho kwa sasa hakipo lakini kwa Jinsi nilivyo isoma na kuisikia mikakati ya CHAUMMA basi PLAN B ni CHAUMMA.

USHAHURI WANGU KWAKO NA WENZAKO:

Ni wakati sasa wa kwenda kuimarisha CHAUMA na hakika mtafanya vizuri kwenye Siasa za TZ maana kila chama kina wenyewe na watu wake kwa maana ya Mashabiki na wapenzi.

Hakuna haja ya kuangaika na CHADEMA nyinyi songeni mbelew na mkumbuke tu kuwa makini msije makaleta watu wale wale walioshindwa NCCR, CUF, TLP au CHADEMA, Hakika leteni watu wapya kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu TECH WIZ nikujibu kwa kiswahili maana kingereza kinanisumbua kidogo,
Sipendi sana kuzundumzia kwamba kwa sasa CHADEMA imechagua plan ipi kati ya hizi na nawaachia wadau wenyewe watafakari.Hata hivyo taasisi ya kisiasa itakayochagua Plan "A" Kitaalam haiwezi kutoboa katika karne hii ya 21.Kitakachotokea ni kwamba itakuwa ni taasisi isiyotabirika, taasisi inayofuata upepo, mtiririko wa matukio, hizia za watu n.k mwishowe kutakuwa hakuna "Strategist" na watakapotokea hawatapata ushirikiano wa kutosha au mipango yao haitakuwa ikiratibiwa vizuri na hatimae ni kuyumba na kusambaratika.Hii ni kwa taasisi yoyote ile itakayojikita katia plan "A" Katika zama hizi.

Tatizo ni kwamba hiyo Plan A ulivyoi-draw up ni kama vile uli-sketch Plan inayotumiwa sasa na Uongozi wa sasa wa Chadema na hiyo Plan B ni kama advice kwa Chadema itoke huko iliko ili kipanuke na kikubalike zaidi na ile jamaa ambayo bado inasua sua kuiunga mkono Chadema.Sorry It's My Opinion.
 
Last edited by a moderator:
betlehem
Nimekusoma ndugu yangu na kwa ulivyo viandika ni MAJI na MAFUTA haviwezi kuenda pamoja hata siku moja.

Na nionavyo mimi PLAN A ni CHADEMA ya sasa na PLAN B ni chama ambacho kwa sasa hakipo lakini kwa Jinsi nilivyo isoma na kuisikia mikakati ya CHAUMMA basi PLAN B ni CHAUMMA.

USHAHURI WANGU KWAKO NA WENZAKO:

Ni wakati sasa wa kwenda kuimarisha CHAUMA na hakika mtafanya vizuri kwenye Siasa za TZ maana kila chama kina wenyewe na watu wake kwa maana ya Mashabiki na wapenzi.

Hakuna haja ya kuangaika na CHADEMA nyinyi songeni mbelew na mkumbuke tu kuwa makini msije makaleta watu wale wale walioshindwa NCCR, CUF, TLP au CHADEMA, Hakika leteni watu wapya kabisa.
Hivi wewe na wenzako mnaokazana kunifukuza CHADEMA, Hivi nimewafanya nini jamani? kosa langu nini nini hasa ndugu?
 
Mkuu TECH WIZ nikujibu kwa kiswahili maana kingereza kinanisumbua kidogo,
Sipendi sana kuzundumzia kwamba kwa sasa CHADEMA imechagua plan ipi kati ya hizi na nawaachia wadau wenyewe watafakari.Hata hivyo taasisi ya kisiasa itakayochagua Plan "A" Kitaalam haiwezi kutoboa katika karne hii ya 21.Kitakachotokea ni kwamba itakuwa ni taasisi isiyotabirika, taasisi inayofuata upepo, mtiririko wa matukio, hizia za watu n.k mwishowe kutakuwa hakuna "Strategist" na watakapotokea hawatapata ushirikiano wa kutosha au mipango yao haitakuwa ikiratibiwa vizuri na hatimae ni kuyumba na kusambaratika.Hii ni kwa taasisi yoyote ile itakayojikita katia plan "A" Katika zama hizi.

betlehem
Nakuuliza Tena CHADEMA ikifa leo wewe inakuuma NINI? Si uanzishe cha kwako kwa PLAN B na CHADEMA ikifa basi CHAUMMA ichukue Nafasi ?

Wansema ADUI MUOMBEE NJAA au ?
 
Last edited by a moderator:
betlehem
Nimekusoma ndugu yangu na kwa ulivyo viandika ni MAJI na MAFUTA haviwezi kuenda pamoja hata siku moja.

Na nionavyo mimi PLAN A ni CHADEMA ya sasa na PLAN B ni chama ambacho kwa sasa hakipo lakini kwa Jinsi nilivyo isoma na kuisikia mikakati ya CHAUMMA basi PLAN B ni CHAUMMA.

USHAHURI WANGU KWAKO NA WENZAKO:

Ni wakati sasa wa kwenda kuimarisha CHAUMA na hakika mtafanya vizuri kwenye Siasa za TZ maana kila chama kina wenyewe na watu wake kwa maana ya Mashabiki na wapenzi.

Hakuna haja ya kuangaika na CHADEMA nyinyi songeni mbelew na mkumbuke tu kuwa makini msije makaleta watu wale wale walioshindwa NCCR, CUF, TLP au CHADEMA, Hakika leteni watu wapya kabisa.

Nionavyo ni kwamba baadhi yenu ndani ya Chadema hata hamjui misingi ya hiki Chama.Hiki ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambapo kutofautiana kimtazamo & kukosoana ni moja wapo ya values za hiki Chama.You could be on the wrong Party for sure!Sorry!!??
 
Last edited by a moderator:
Hivi wewe na wenzako mnaokazana kunifukuza CHADEMA, Hivi nimewafanya nini jamani? kosa langu nini nini hasa ndugu?

betlehem

Hivi nimekufukuza nimekushahuri?
Hivi kama wewe ni msomi mwerrevu na bora zaidi ya wengine, sasa kwanini unangangania kukaa na wajinga? Hivi ujuhi Samaki mmoja akioza basi wanaoza wote ?

Huoni sasa na wewe pamoja na ubora wote unaojidai kuwa unao, Unavyoendelea kubaki CHADEMA na wewe unaonekana ni walewale ?
 
Last edited by a moderator:
betlehem
Nakuuliza Tena CHADEMA ikifa leo wewe inakuuma NINI? Si uanzishe cha kwako kwa PLAN B na CHADEMA ikifa basi CHAUMMA ichukue Nafasi ?

Wansema ADUI MUOMBEE NJAA au ?

You are flipping wrong dude!Bethlem have as much right as you to speak his mind & no one not even you who could deprive him of that constitutional right.The Party's Constitution provide him with that freedom of expression right,Philosophical dogma is not allowed in Chadema only is allowed in the Communist Party of CCM where its leaders are chosen but not elected through the ballot box.We don't wanna see Chadema following the suit.
 
Last edited by a moderator:
Betlehem,

Habari za weekend?

Ndugu yangu, nimekusoma vizuri. Plan A na B umeziweka bayana. Hata hivyo kuna upungufu mkubwa katika hizi plan ulizoweka.

Umefanya assumption kwamba lengo kuu la Chadema kama chama cha siasa ni kupata fursa ya kuunda serikali.

Hata hivyo kwa Chadema hilo sio lengo kuu. Chadema ikifika 2015 hata ukiwaonyesha marking scheme ya jinsi ya kushinda uchaguzi, hawako tayari kuifuata marking scheme hiyo iwapo vitu fulani havijatimia.

Fursa ya kuunda serikali Chadema wanaitaka but with conditions.

Cc Pasco
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu kwa uchambuzi wako.. Lakini kwa Tz ya sasa kupata chama kitakachoenda na plan B ni ngumu sana. Sbb viongozi wakuu wa vyama vya siasa nchini Tz wanaaply plan A ambayo inabeba maslahi ya wakubwa. Vijana na watu wenye mitazamo ya plan B wanapaswa kuunganisha nguvu na kuunda strong political party. Kwani tuliowategemea cdm wana madhaifu mengi sana.
 
Hivi wewe na wenzako mnaokazana kunifukuza CHADEMA, Hivi nimewafanya nini jamani? kosa langu nini nini hasa ndugu?

Kuwa Chadema na kuizungimzia Chadema au Chama chochote ni haki yako ya kikatiba. Vyama vinaendeshwa kwa kodi unayolipa.

Utaratibu huu wa kutoleana kauli za dharau uko Chadema kwa sababu kuna watu wanaoona chama ni mali yao binafsi.
 
Back
Top Bottom