Dalili za Uongozi wa Chama chochote, Umoja wowote, Kikundi chochote kuchokwa na wanachama wake ni pamoja na taarifa zake kuanza kuvuja hovyo hovyo.
Viongozi hawa huanza kutengeneza Makundi Makundi hasa pale inapotokea Wale wa juu kiuegemea/kupendelea upande mmoja. Makundi haya hayaishii kwa viongozi tu bali huenea mpaka kwa walaji ambao ni wanachama wa kawaida.
Siku za hivi karibuni limejitokeza ombwe la kinachoonekana wazi ni kuvuja kwa mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zikiwemo barua za taarifa kwa wanachama wake na watanzania kwa ujumla kuhusu mamnbo mbalimbali, taarifa ambazo hata hivyo zimekuwa zikikanushwa ndani ya kipindi kifupi sana tangu zianze kusambazwa, jambo ambalo kwa mjuzi wa mambo anaweza pasi na shaka kufikia hitimisho kwamba aliyesambaza ujumbe huo ndiye aliyejitokeza kukanusha. Sitaki niwafumbue macho watu wengine waamini hivyo. Miongoni mwa siri zilizovuja siku za hivi karibu ni pamoja na:
1.Kikao cha siri cha Wabunge Vijana wa chama hicho mjini Dodoma. Wabunge siyo tu ni kundi muhimu sana ndani ya chama bali wana nguvu katika maamuzi.
2. Barua iliyosambaa katika Mitandao ya Kijamii ikionekana kuandikwa na kundi lingine Muhimu sana, kundi la Wasomi wa vyuo vikuu kupitia umoja wao wa Chadema. students' Organisation (CHASO). Historia inaonesha wasomi wamekuwa ni chanzo cha mabadiliko katika nchi nyingi sana duniani.
3. Barua ya Mkuu. Wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama ikiwataarifu Wanachama na Watanzania wote juu kuteuliwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Mama Hellen Kijo Bisimba kuwa mjumbe wa Baraza la Wazee wa Chadema. Mama Bisimba anamaliza muda wake kuitumikia LHRC 30 may, 2018, hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa na kituo hicho katika Mitandao ya Kijamii jana wakati wakikanusha Madai ya uteuzi wa Mtumishi wao huyo kuwa Kiongozi ndani ya chama cha siasa. Siku chache kabla ya kusambaa kwa barua ya Mama Bisimba kuteuliwa kuwa mjumbe wa Baraza la wazee wa Chadema alionekana katika picha tofauti tofauti akiwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa Upande mmoja wa CUF, maalim Seif Sharif Hamad. Picha hizi oia zilisaambaa katika Mitandao ya Kijamii.
Chama au taasisi yoyote inapofikia hatua hii, mambo mawii tu ya msingi ya kujiuliza ni:
1. Tatizo ni nini?
2. Nini kifanyike?
Niende moja kwa moja kwenye tatizo. Kabla ya kujua tatizo nini, kwanza mnapaswa kukubali kuna tatizo, vinginevyo hakutakuwa na suluhu. Naandika haya kwa mapenzi mema kabisa. Ndani ya Chadema kuna uwezekano wa haya yakawa ni tatizo
1. Kuna watu hawaridhishwi na wanavyotendewa ukilinganisha na wengine (kuna upendeleo). Hapana siri hapa hili limekuwa likipigiwa kelele sana.
2. Basi tu watu wamechoka wanataka kuona mabadiliko hata kama mabadiliko hayo hayatakuwa na athari chana, ilimradi tu waone sura mpya,. Hiyo ni hulka ya binadamu.
Ni kifanyike baada ya kukubali kuna tatizo?
1. Ni kutafuta suluhu kati ya pande mbili ambazo hazikubaliani baadhi ya mambo
2. Kukubali mabadiliko, na hili ni la msingi sana.
3. Kudhibiti mfumo wa utoaji habari.
Viongozi hawa huanza kutengeneza Makundi Makundi hasa pale inapotokea Wale wa juu kiuegemea/kupendelea upande mmoja. Makundi haya hayaishii kwa viongozi tu bali huenea mpaka kwa walaji ambao ni wanachama wa kawaida.
Siku za hivi karibuni limejitokeza ombwe la kinachoonekana wazi ni kuvuja kwa mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zikiwemo barua za taarifa kwa wanachama wake na watanzania kwa ujumla kuhusu mamnbo mbalimbali, taarifa ambazo hata hivyo zimekuwa zikikanushwa ndani ya kipindi kifupi sana tangu zianze kusambazwa, jambo ambalo kwa mjuzi wa mambo anaweza pasi na shaka kufikia hitimisho kwamba aliyesambaza ujumbe huo ndiye aliyejitokeza kukanusha. Sitaki niwafumbue macho watu wengine waamini hivyo. Miongoni mwa siri zilizovuja siku za hivi karibu ni pamoja na:
1.Kikao cha siri cha Wabunge Vijana wa chama hicho mjini Dodoma. Wabunge siyo tu ni kundi muhimu sana ndani ya chama bali wana nguvu katika maamuzi.
2. Barua iliyosambaa katika Mitandao ya Kijamii ikionekana kuandikwa na kundi lingine Muhimu sana, kundi la Wasomi wa vyuo vikuu kupitia umoja wao wa Chadema. students' Organisation (CHASO). Historia inaonesha wasomi wamekuwa ni chanzo cha mabadiliko katika nchi nyingi sana duniani.
3. Barua ya Mkuu. Wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama ikiwataarifu Wanachama na Watanzania wote juu kuteuliwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Mama Hellen Kijo Bisimba kuwa mjumbe wa Baraza la Wazee wa Chadema. Mama Bisimba anamaliza muda wake kuitumikia LHRC 30 may, 2018, hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa na kituo hicho katika Mitandao ya Kijamii jana wakati wakikanusha Madai ya uteuzi wa Mtumishi wao huyo kuwa Kiongozi ndani ya chama cha siasa. Siku chache kabla ya kusambaa kwa barua ya Mama Bisimba kuteuliwa kuwa mjumbe wa Baraza la wazee wa Chadema alionekana katika picha tofauti tofauti akiwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa Upande mmoja wa CUF, maalim Seif Sharif Hamad. Picha hizi oia zilisaambaa katika Mitandao ya Kijamii.
Chama au taasisi yoyote inapofikia hatua hii, mambo mawii tu ya msingi ya kujiuliza ni:
1. Tatizo ni nini?
2. Nini kifanyike?
Niende moja kwa moja kwenye tatizo. Kabla ya kujua tatizo nini, kwanza mnapaswa kukubali kuna tatizo, vinginevyo hakutakuwa na suluhu. Naandika haya kwa mapenzi mema kabisa. Ndani ya Chadema kuna uwezekano wa haya yakawa ni tatizo
1. Kuna watu hawaridhishwi na wanavyotendewa ukilinganisha na wengine (kuna upendeleo). Hapana siri hapa hili limekuwa likipigiwa kelele sana.
2. Basi tu watu wamechoka wanataka kuona mabadiliko hata kama mabadiliko hayo hayatakuwa na athari chana, ilimradi tu waone sura mpya,. Hiyo ni hulka ya binadamu.
Ni kifanyike baada ya kukubali kuna tatizo?
1. Ni kutafuta suluhu kati ya pande mbili ambazo hazikubaliani baadhi ya mambo
2. Kukubali mabadiliko, na hili ni la msingi sana.
3. Kudhibiti mfumo wa utoaji habari.