Mbelwa Germano
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 789
- 289
Kuna wakati ilikuwa ni vigumu kufikiri kwamba CHADEMA kinaweza kupata kiti cha ubunge kutoka Singida lakini Kamanda Tundu Lissu akadhihirisha kwamba hakuna ngome isiyopitika. Na si ajabu mwaka 2015 vitapatikani viti zaidi vya ubunge kutoka singida tukianza na jimbo la Iramba Magharibi.
Vilevile kuna wakati ilikuwa ni vigumu kufikiri CHADEMA inaweza kupata kata hata moja kutoka Tabora lakini hili likawezekana. Tofauti ya kura za ubunge kule Igunga imedhihirisha hakuna ngome isiyopitika. Lakini vilevile alama ya kukosa kata kule Shinyaga inatupa tafakari nyingine.
Kuna wakati baadhi ya wanachama/wafuasi wa CHADEMA wanaweza kufikiri wanaweza kushinda kwa ngazi ya uraisi kwa kutegemea baadhi ya mikoa (Arusha, Mwanza, Kilimanjaro, Mbeya, Shinyanga n.k. ) kwa kisingizio cha chama kukubalika sana na idadi kubwa ya watu bila ya angalau asilimia 40 ya kura kutoka Tanga. Hili ni jambo la kutilia shaka. Naomba nikumbushe:
Kwa mfano: Ukiwa unaamini kwamba Mkoa wa Arusha na Mwanza au Shinyanga ni ngome imara ya CHADEMA na kinashindwa kupata zaidi ya asilimia sitini ya kura na wakati huohuo CCM inapata zaidi ya asilimia 60 ya kura kutoka Tanga (tena mkoa wenye idadi wa watu zaidi ya milioni 1.5) ujue hapa ushindi upo mashakani.
Vilevile unapoona Mbunge wa CHADEMA anashinda jimbo fulani na wakati huohuo mgombea uraisi wa CHADEMA anashindwa na mgombea wa CCM ushindi kwa ngazi ya uraisi ipo mashakani.
Ushindi wa CHADEMA kwa ngazi ya uraisi hauwezi kutokana na wingi wa kura toka kwenye baadhi ya mikoa bali wastani usiopungua chini ya asilimia 40 kutoka mikoa yote ya Tanzania bara.Nguvu ya ziada inahitajika.
Nawakilisha.