Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,923
Baada ya uchaguzi wa mwaka huu Chama Cha Chadema kimetokea kuwa chama mashuhuri kati ya vyama vya upinzani dhidi ya CCM. Si ajabu kuona kuna mikakati ya kukisambaratisha.
Tunahitaji chama kimoja chenye nguvu cha upinzani ili kuleta changamoto katika mabadiliko yenye kuleta ndoto za maendeleo tunazotafakari kila kukicha katika taifa, vinginevyo tutaendelea na kinogaubaga. Bila ushindani wa kisiasa hakuna maendeleo ya kasi. Kwani wapenda maendeleo hawashabikii mradi kuwa na vyama vya siasa ila maendeleo ya vyama vyenye kuleta nguvu za kimapinduzi katika kuhamasisha maendeleo ya taifa kiushindani. Kumbuka huwezi kuwa mchezaji maarufu na mfungaji mzuri wa magoli bila kuwa na ushindani wa wanaogombania nafasi hiyo, na lazima upitie kipindi kigumu na hata cha kukata tamaa kwani ugumu wo wote ndio ngazi ya kufikia malengo. Wapiga kinanda wanafunzi huanza kiulani tu lakini unapofikia kiwango cha kila mkono kwenda kila upande peke yake hapo wanaanza toka jasho, kumbe ndio kipindi cha kuvuka na kuwa mpiga kinanda mzuri na mahiri.
USHAURI NASAHA: Chadema wawe makini na ye yote ambaye hata kama amekuwa wa kuaminika kwa muda mrefu iwapo mwenendo wake ni hatari kwa kukiimarisha Chama. Kuwa waangalifu na chachu mbaya inayoweza kumega chama, kwani mwenye mapenzi mema atayazungumza yanayohusu chama ndani ya chama, lakini kutoka nje ya chama ni hatari sana na haieleweki, na kabisa kuweka makundi ndani ya chama ni ufa wenye kulinganishwa na donda ndugu. Cha msingi kuwa makini na ndumilakuwili, isijetokea kulaumiana baadaye wakati nyoka anayekusudia kukuuma unaona movement zake nafasi ya kukwepa inakuruhusu. Leo amevuta mmoja, kisho utaona kikundi hapo mwenye macho huambiwi tazama. Uroho wa madaraka hupumbaza akili timamu.
BANIANI MBAYA KIATU CHAKE DAWA: Kuna mengi ya kujifunza toka CCM kwani humaliza mambo yao kwenye vikao, na huoni mwenye kuongelea mambo ya chama nje ya vikao, hapo huo ndio umoja unaotakiwa. Na kama umekosea unatakiwa kumalizana na wenzako vikaoni. Hilo la lugha za utata za nani sijui ana udini au utawala wa imla ni sumu mbaya sana. Rais Kikwete asingekuwa mnyenyekevu na msikivu leo asingekuwa Rais wa Tanzania, lakini baada ya kupata mwanguko wa mende kule Dodoma na Mkapa kutoka kifua mbele, alinyenyekea na kuvuta subira leo huyo kaukwaa Urais. Wapo wengi wa kutolea mizani lakini mwenye kuelewa anaelewa. Ulizeni CUF wamefanyeje kwani imeshindikana kuwasambaratisha kwa nini isiwezekane CHADEMA?
Wapenda mabadililiko tunasoma ishara za nyakati na wahusika wanatakiwa kuchukulia hatua zinazofaa vinginevyo itabaki historia kama ilivyotokea kwa Chama cha NCCR Mageuzi. Na ukiona mmoja hatetereki katika msimamo wake na wakati wengi wanaona yuko nje ya upeno wa nyumba tunayojenga wote ujue kuna anakopata ubavu, na bila kuwa na jicho makini ataendelea eneza sumu, isha kesho utaona wengine wanakuja na jingine hapo ujue mambo ndo yanaanza iva. Kuwa makini na mwendo wa kinyonga wa kubadilikabadilika rangi bila kukusudia mradi amepitia kuliko na rangi anaakisi rangi sawia.
Tamaa ilimshinda Sungura kupata mbivu kwa wanaokumbuka hekaya za Abunuwasi. Na hata katika siasa tunakumbuka wenye majina kama akina Masumbuko Lamwai, Kaburu na hawasikiki kabisa, na sijui kama wana ubavu wa kurudia hadhi waliyokuwa nayo hapo awali katika ulingo wa siasa.
Wana JF mnaweza kutia kapuni maoni yangu lakini ndio ishara za nyakati na kuna siku mtakumbuka ninayoyaongea leo. Ukimdaka nyani anakumalizia mahindi shambani ukiamua kumpiga anakuangalia kwa huruma sana na utamwacha, utajuta kesho ukirudi shambani utakuta mabua tu, kwani njaa ndiyo nyani anaona kitu muhimu kwake kuliko haki ya jasho lako.
Tunahitaji chama kimoja chenye nguvu cha upinzani ili kuleta changamoto katika mabadiliko yenye kuleta ndoto za maendeleo tunazotafakari kila kukicha katika taifa, vinginevyo tutaendelea na kinogaubaga. Bila ushindani wa kisiasa hakuna maendeleo ya kasi. Kwani wapenda maendeleo hawashabikii mradi kuwa na vyama vya siasa ila maendeleo ya vyama vyenye kuleta nguvu za kimapinduzi katika kuhamasisha maendeleo ya taifa kiushindani. Kumbuka huwezi kuwa mchezaji maarufu na mfungaji mzuri wa magoli bila kuwa na ushindani wa wanaogombania nafasi hiyo, na lazima upitie kipindi kigumu na hata cha kukata tamaa kwani ugumu wo wote ndio ngazi ya kufikia malengo. Wapiga kinanda wanafunzi huanza kiulani tu lakini unapofikia kiwango cha kila mkono kwenda kila upande peke yake hapo wanaanza toka jasho, kumbe ndio kipindi cha kuvuka na kuwa mpiga kinanda mzuri na mahiri.
USHAURI NASAHA: Chadema wawe makini na ye yote ambaye hata kama amekuwa wa kuaminika kwa muda mrefu iwapo mwenendo wake ni hatari kwa kukiimarisha Chama. Kuwa waangalifu na chachu mbaya inayoweza kumega chama, kwani mwenye mapenzi mema atayazungumza yanayohusu chama ndani ya chama, lakini kutoka nje ya chama ni hatari sana na haieleweki, na kabisa kuweka makundi ndani ya chama ni ufa wenye kulinganishwa na donda ndugu. Cha msingi kuwa makini na ndumilakuwili, isijetokea kulaumiana baadaye wakati nyoka anayekusudia kukuuma unaona movement zake nafasi ya kukwepa inakuruhusu. Leo amevuta mmoja, kisho utaona kikundi hapo mwenye macho huambiwi tazama. Uroho wa madaraka hupumbaza akili timamu.
BANIANI MBAYA KIATU CHAKE DAWA: Kuna mengi ya kujifunza toka CCM kwani humaliza mambo yao kwenye vikao, na huoni mwenye kuongelea mambo ya chama nje ya vikao, hapo huo ndio umoja unaotakiwa. Na kama umekosea unatakiwa kumalizana na wenzako vikaoni. Hilo la lugha za utata za nani sijui ana udini au utawala wa imla ni sumu mbaya sana. Rais Kikwete asingekuwa mnyenyekevu na msikivu leo asingekuwa Rais wa Tanzania, lakini baada ya kupata mwanguko wa mende kule Dodoma na Mkapa kutoka kifua mbele, alinyenyekea na kuvuta subira leo huyo kaukwaa Urais. Wapo wengi wa kutolea mizani lakini mwenye kuelewa anaelewa. Ulizeni CUF wamefanyeje kwani imeshindikana kuwasambaratisha kwa nini isiwezekane CHADEMA?
Wapenda mabadililiko tunasoma ishara za nyakati na wahusika wanatakiwa kuchukulia hatua zinazofaa vinginevyo itabaki historia kama ilivyotokea kwa Chama cha NCCR Mageuzi. Na ukiona mmoja hatetereki katika msimamo wake na wakati wengi wanaona yuko nje ya upeno wa nyumba tunayojenga wote ujue kuna anakopata ubavu, na bila kuwa na jicho makini ataendelea eneza sumu, isha kesho utaona wengine wanakuja na jingine hapo ujue mambo ndo yanaanza iva. Kuwa makini na mwendo wa kinyonga wa kubadilikabadilika rangi bila kukusudia mradi amepitia kuliko na rangi anaakisi rangi sawia.
Tamaa ilimshinda Sungura kupata mbivu kwa wanaokumbuka hekaya za Abunuwasi. Na hata katika siasa tunakumbuka wenye majina kama akina Masumbuko Lamwai, Kaburu na hawasikiki kabisa, na sijui kama wana ubavu wa kurudia hadhi waliyokuwa nayo hapo awali katika ulingo wa siasa.
Wana JF mnaweza kutia kapuni maoni yangu lakini ndio ishara za nyakati na kuna siku mtakumbuka ninayoyaongea leo. Ukimdaka nyani anakumalizia mahindi shambani ukiamua kumpiga anakuangalia kwa huruma sana na utamwacha, utajuta kesho ukirudi shambani utakuta mabua tu, kwani njaa ndiyo nyani anaona kitu muhimu kwake kuliko haki ya jasho lako.