oba
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 310
- 65
Kuna methali isemayo,"Mgema akisifiwa, tembo hulitia maji"
Kadri siku zinavyokwenda ndivyo umaarufu wa CHADEMA unavyoongezeka na kwa ukweli mkiendelea hivyo mwaweza kuwa chama mbadala cha kushika dola hivi karibuni.
Wasiwasi wangu ni wanachama wapya mnaowapokea na kuwapa position kwenye chama.
Kwa kuwa CHADEMA kinakua kwa kasi, mtapata wanachama ambao lengo lao si mageuzi kama sera zenu zinavyodai bali ni kutafuta kimbilio la maslahi yao na ubinafsi wao pindi CCM itakapokuwa imeanguka rasmi.
Kuweni waangalifu na wakimbizi wa kisiasa, wengine siyo wazuri, watageuza chama chenu kuwa chama cha mafisadi na wababaishaji kama ilivyo CCM.
Aidha ninawashauri muwe tayari kumuadabisha mtu yeyote bila kujali position yake ktk chama pale anapokengeuka na kuacha misingi ya chama, mkifanya hivyo mtaondoa dhana ya kulindana inayokivunja CCM na mtajijengea imani zaidi kwa wanachi na mwanachama yeyote anayejiunga atajua kuwa ninyi siyo chama kingine cha siasa bali chama cha wawajibikaji.
Nawasilisha!
Kadri siku zinavyokwenda ndivyo umaarufu wa CHADEMA unavyoongezeka na kwa ukweli mkiendelea hivyo mwaweza kuwa chama mbadala cha kushika dola hivi karibuni.
Wasiwasi wangu ni wanachama wapya mnaowapokea na kuwapa position kwenye chama.
Kwa kuwa CHADEMA kinakua kwa kasi, mtapata wanachama ambao lengo lao si mageuzi kama sera zenu zinavyodai bali ni kutafuta kimbilio la maslahi yao na ubinafsi wao pindi CCM itakapokuwa imeanguka rasmi.
Kuweni waangalifu na wakimbizi wa kisiasa, wengine siyo wazuri, watageuza chama chenu kuwa chama cha mafisadi na wababaishaji kama ilivyo CCM.
Aidha ninawashauri muwe tayari kumuadabisha mtu yeyote bila kujali position yake ktk chama pale anapokengeuka na kuacha misingi ya chama, mkifanya hivyo mtaondoa dhana ya kulindana inayokivunja CCM na mtajijengea imani zaidi kwa wanachi na mwanachama yeyote anayejiunga atajua kuwa ninyi siyo chama kingine cha siasa bali chama cha wawajibikaji.
Nawasilisha!