CHADEMA kesho kutoa takwimu za vifo vilivyotokana na mgomo, Dar es salaam

Tutatoa tamko Rasmi la Chama kanda hii ya Dar es salaam kuhusiana na mgomo huwo na athari zilizojitokeza mpaka sasa.

Nilitegemea vyama vingepigana vikumbo mahospitalini kuongea na madaktari au kuwapa misaada madaktari wasigome na si kusubiri na vikamera na visimu koko vya kunasa sauti vilio vya wagonjwa wasiopata matibabu na kukaa nje ya chumba cha motuary na kuhesabu maiti ngapi zinatoka mawodini kuingia motuary na kwenda kuhutubia kueleza idadi ya waliokufa na wanaogalagala kwa maumivu mawodini .Hekima ya kisiasa inatakiwa.Nchi zingine vyama vingekuwa vinahangaika kujaribu kuepusha mgomo maana wakigoma wafao ni wa kutoka vyama vyote na msiba kwa kila chama na si serikali pekee.Nyongeza za mishahara na marupurupu kwa madaktari wabunge n.k ni kilio kwa mtu wa kawaida sababu yeye ndiye atakiwaye kukamuliwa hiyo kodi ya kugharimia hizo starehe za posho na nyumba nzuri watakazo hao madaktari.Iko siku wananchi watawavamia hawa wadai posho na marupu rupu mazuri bila kujali ni wabunge au madaktari.Kila mtu anadai aongezewe mwalimu anadai,askari anadai,daktari anadai,pesa yote inatoka kwa mlipa kodi ambaye tayari kachoka na mlundikano wa kodi mwisho wa siku kuna siku wagonjwa wataamka vitandani wawalambe makofi kuanzia serikali,vyama na hao wafanyakazi wawe madaktari au nani kwa kutumia matatizo yao kujinufaisha kisiasa na ki-kuongezeana mapato kutokana na kodi zao wagonjwa.
 
Chadema bana kwa kurukia mambo! Nataka kujua nani kawapa mamlaka ya kutoa ripoti masuala mengine ni ya taaluma sio siasa.
 
OK sasa nimebaini kumbe hawa jamaa wamepeana zamu za kuingia jamvini kwa uzi huu ni zamu ya; thatha na GeniusBrain

Tuachane nao hawa ninacho kumbuka Chadema walisema mwaka huu wataongelea chanzo/kiini cha matatizo tunayo yapata nategemea hili kutekelezwa kesho all the best CHADEMA
 
cdm mnanifurahisha hapo tu mpo makini sana na mambo ya msingi, mnatimia wajibu wenu sana iumbueni magamba maana wananchi hawajui yanayojiri. ila mcheck sheria kwanza kabla ya kutoa takwimu wasije wakapata sababu ya kuwapa kesi
 
huu si utaahir a sasa badala ya kusaidia erikali isolve ,,ila najua sio kweli hakuna hilo tamko
 
Kwani CHADEMA ndiyo Serikali au Daktari mkuu mpaka mtoe takwimu za vifo vilivyotokana na mgomo? Au tuamini kwmaba ninyi ni miongoni wa makundi yaliokuwa nyuma ya mgomo huo?
Hamna hata haya, yaani mnakuwa kimbelembele kutoa tamko kwa jambo ambalo mmelianzisha ninyi? Acheni siasa za mauaji.
Serikali ya CCM ndiyo inayosababisha mauaji kwa ajili ya utendaji mbovu! Kwa mang'amuzi yako unadhani serikali hiyo inaweza kutoa takwimu halisi za vifo? Takwimu halisi zitakuwa za CHADEMA. Lakini za CCM itabidi zichakachuliwe kwanza!
 
Chadema bana kwa kurukia mambo! Nataka kujua nani kawapa mamlaka ya kutoa ripoti masuala mengine ni ya taaluma sio siasa.
Ama kweli! kazi kweli kweli!! Nani kakuambia kuwa vifo vinavyotokana na udhaifu wa serikali kutowatendea haki watumishi wa uma ni suala la taaluma?
 
Well, labda mimi niseme kwamba nimempoteza rafiki yangu ktk mgomo huu na ina niuma vibaya sana kwa sababu angeweza kabisa kupona ama kupata nafuu..CDM acheni hizi siasa mnatutia machungu zaidi maana wengine ndio hatuelewi Madaktari wala viongozi.. Hawa wote wanagombana bila kujali uhai wa wananchi wake.
 
Back
Top Bottom