Chadema kaeni chonjo! Moto huu hauzimiki leo ama kesho

CCM hamjajibu hoja za msingi. Hamkutueleza habari za kuvuana magamba zimefikia wapi? Maisha bora mliyoyaahidi yapo wapi, mbona siku hizi hamyasemei? Ninyi mmeshika dola wala hamkuhitaji kufanya mkutano wa hadhara! Matendo yenu tu yangetosha kutueleza kwamba kuna vitu mmefanya. Mwenye macho huwa haambiwi tazama. Sasa mafanikio mnayosema mpaka tuyatafute kwa tochi?

Si kwamba hamjafanya kitu kabisa, la hasha, ila mlichofanya ni kiduchu ukilinganisha na umri wenu! Mkae mkielewa kuwa watz wa leo wanafahamu kutenga mchele na pumba. Zile za jangwani mbona fiksi tu, hata mioyoni mwenu mnajua kuwa mlichofanya ni fiksi na hamuwezi kujivunia! Kwanza mmewasomba watu kama kawaida yenu. Pili mmewapa elfu tano tano, t- shirt na kofia. Hata mdogo wangu alipokea hiyo hela. Hapo si mnafanya kazi ya kupaka rangi upepo? Toka hapo zamani mlipoanza kuahidi hamtekelezi, mkifanya, ni kudogo tu kwa ajili ya kuzuga, mbona ahadi zenu hazitofautiani na za kuku?
 
CCM hamjajibu hoja za msingi. Hamkutueleza habari za kuvuana magamba zimefikia wapi? Maisha bora mliyoyaahidi yapo wapi, mbona siku hizi hamyasemei? Sasa mafanikio mnayosema mpaka tuyatafute kwa tochi? Toka hapo zamani mlipoanza kuahidi hamtekelezi, mkifanya, ni kudogo tu kwa ajili ya kuzuga, mbona ahadi zenu hazitofautiani na za kuku?

Serikali ya Awamu ya nne kusema ukweli hakuna walichofanya ambacho kinaonekana. Na ndio maana katika uchaguzi 2010 CCM ilipata shida sana na upinzani mkubwa sana. Raisi Kikwete mwaka 2005 alichaguliwa kwa kura nyingi kwa sababu tulitegemea atakuwa mkombozi wa taifa letu kumbe imekuwa tofauti sasa amekuwa muuaji wa Taifa.

Akiongea kwa kujiamini, endapo kama humjui utasema "kiongozi ndiye huyu!!!!!!"

kikwetehotuba.jpg

kumbe hakuna lolote ni maneno na ahadi kama za kuku miaka nenda miaka rudi.

Juzi pale uwanja wa Kaburi la CCM (zamani Jangwani) walikosa hata mvuto wa kuwaeleza wananchi, wameshindwa kujibu hoja za msingi za wananchi wa Tanzanai. Mfano: Mfumuko wa bei, hali mbaya ya uchumi, kipato kidogo, Ubadhirifu wa mali za umma, Kukithiri kwa Rushwa kutoka kwa watendaji wa Serikali, Rushwa katika chaguzi za CCM, nk.

Badala yake ilikuwa ni Blabla tupu za akina Wassira, View attachment 56094 na akina Maguu Fuli, Mwakye embe, nk.

View attachment 56084

Tunahitaji vitendo toka Serikali tawala na siyo ahadi, Hawakupaswa kusema wamefanya nini isipokuwa Wananchi ndio tuseme serikali yetu imefanya nini (Yaani mambo yaonekane)

Wamepoteza pesa tu, kwa kuandaa mkutano, usafiri na kugawa kwa washiriki.

"NIMELIONA KABURI LA CCM PALE JANGWANI"


View attachment 56083


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Nyie pigeni kelele tu mnadhani wenzenu bado miaka ya 2010. Sasa hivi CCM inabadilika. Kinachotakiwa CDM wabadilishe mfumo wa sera zao maana kiukweli kelele za CDM kimewafanya CCM wanabadilika.

USHAURI:

Wanatakiwa CDM wabadilishe mfumo wa Sera zao la sivyo mwaka 2015 itakuwa hivi:-

CCM 75%
CUF 10%
NCCR 7%
CDM 5%
UDP 2.5%
Others 0.5 %


Kuweni chonjo watanzania wanaakili sio wajinga. Vyama vyote vinatakiwa kubadilika

TRUTH SHALL SET YOU FREE

kwa kuiba,wapiga kura hewa.....lazima iwe ivi.....ila one on one on a fair ground....mnaangukia pua
 
Lakini katika mioto kuna mioto
Je huo moto CDM unasaidia nn nchi? kama sio uchu wa kutaka madaraka?
Mimi sina msosi na nimelala njaa hao CDM wanakula je ninapata faida gani?
Tuwe wakweli kuzunguka huku na huku na kutoa maneno haina faida yoyo sisi tunataka maendeleo bwana.

Wajaribu japo kuleta maendeleo hata kijiji kimoja Singida ambako watu njaa inawaua. Maneno matupu hayavunji mfupa bwana. Je hapo unasemaje?

we unafikiri nani mwenye uchu wa madaraka kati ya ccm na cdm? unasema moto unasaidia nini nchi? we kweli gamba yahani unadhani dhana ya kujivua gamba ingetoka wapi? mpaka siku mtakapojikuta mnaitwa wapinzani ndo utaona moto huu umesaidia nini. hebu angalieni mnavyochemshwa bungeni jana na badala yake mnatukana tu. cdm wameshona magwanda mmeiga, wameanziasha kauli mbiu ya vua gamba vaa gwanda napo mnaiga, mmeambiwa mtimue mawaziri mmewatimua, shame on you. Wameanzisha operation ya M4C na nyie mnaiga kupita kuzima ahhhhhh
 
Lakini katika mioto kuna mioto
Je huo moto CDM unasaidia nn nchi? kama sio uchu wa kutaka madaraka?
Mimi sina msosi na nimelala njaa hao CDM wanakula je ninapata faida gani?
Tuwe wakweli kuzunguka huku na huku na kutoa maneno haina faida yoyo sisi tunataka maendeleo bwana.

Wajaribu japo kuleta maendeleo hata kijiji kimoja Singida ambako watu njaa inawaua. Maneno matupu hayavunji mfupa bwana. Je hapo unasemaje?


maendeleo hayajaribiwi hiyo kujaribu ndo wamekuwa wakiifanya CCM miaka zaidi ya 40, wakipewa power wataweza saizi wanachokifanya ni mobilization kama uongozi ungekuwa unabinafsishwa basi mngewabinafsisha CDM baadhi ya wizara na mikoa muone kazi nyie magamba
 
Back
Top Bottom