Kididimo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 3,791
- 3,360
Nimemsikiliza Mgombea Urais kupitia Chadema. Kiujumla anapaswa kuongea zaidi kuliko wagombea wa vyama vingine.
Kwa kuwa hakuweponchini kwa muda mrefu tofauti na wale wengine, inaweza kuwa sababu ili afahamike. Lakini pia siyo mgeni kwa mambo ya nchi yetu. Watu wana shauku ya kujua "SERA MBADALA" na siyo " SERA FITINA".
Hapa nina maana kwa mfano JPM kanunua ndege kadhaa, je, yeye ana maoni gani mbadala? Mfano mwngine JPM kakopa korosho za wakulima na malipo yakasuasua, je yeye kwenye hili ana maoni gani?
Haya ndiyo watu wengi kama siyo wote wangependa kuyasikia na ndiyo yatawapa credibility Chadema ya kura nyingi.
Siyo wakati wa kupoteza muda kuponda hata vile ambavyo mwananchi wa kawaida anaona vimemsaidia.
Mfano, ukisimama hadharani ukasema JPM anatoa au kupokea rushwa wananchi watakudharau kwa vile wamejionea alivyopambana na ulaji rushwa, alivyotumbua wengi nk.
Hapo utapoteza credibility haraka na wananchi watawachoka mapema tuu. Nchi imebadilika sana.
Hivyo, kwa vile Mgombea wenu ni jina kubwa hapa nchini, awe makini na anachokiongea, na kuwe na jopo la kumfunga breki mapema. Bado hamjachelewa.
Hayo ni maoni yangu binafsi.
Kwa kuwa hakuweponchini kwa muda mrefu tofauti na wale wengine, inaweza kuwa sababu ili afahamike. Lakini pia siyo mgeni kwa mambo ya nchi yetu. Watu wana shauku ya kujua "SERA MBADALA" na siyo " SERA FITINA".
Hapa nina maana kwa mfano JPM kanunua ndege kadhaa, je, yeye ana maoni gani mbadala? Mfano mwngine JPM kakopa korosho za wakulima na malipo yakasuasua, je yeye kwenye hili ana maoni gani?
Haya ndiyo watu wengi kama siyo wote wangependa kuyasikia na ndiyo yatawapa credibility Chadema ya kura nyingi.
Siyo wakati wa kupoteza muda kuponda hata vile ambavyo mwananchi wa kawaida anaona vimemsaidia.
Mfano, ukisimama hadharani ukasema JPM anatoa au kupokea rushwa wananchi watakudharau kwa vile wamejionea alivyopambana na ulaji rushwa, alivyotumbua wengi nk.
Hapo utapoteza credibility haraka na wananchi watawachoka mapema tuu. Nchi imebadilika sana.
Hivyo, kwa vile Mgombea wenu ni jina kubwa hapa nchini, awe makini na anachokiongea, na kuwe na jopo la kumfunga breki mapema. Bado hamjachelewa.
Hayo ni maoni yangu binafsi.