TAARIFA KWA UMMA
Sekretarieti ya jimbo la Segerea inawataarifu viongozi wote wa kata,wanachama na wapenda mabadiliko kwamba,katika kufuatilia utekelezaji wa shughuli za kila siku za chama,imeanza ziara kwenye kata nane za jimbo la Segerea kukagua utekelezaji wa kazi cha kila siku za chama kwa kupitia ripoti zote za chama na mabaraza(BAVICHA,BAWACHA NA BARAZA LA WAZEE) pia itapitia mihutasari ya vikao vyote vya kikatiba na vya dharura pamoja na kutembelea matawi na misingi kwa kujiridhisha yale yaliyoko kwenye maandishi kama yanakwenda sambamba na kwenye field.
Ziara hizi tayari zimeanzia Kata ya Segerea siku ya 1/12/2012 na zitaendelea tena siku ya tarehe 7/12/2012 ijumaa sekretarieti itakuwa kata ya Kinyerezi na tarehe 8/12/2012 itakuwa kata ya Kimanga na tarehe 14/12/2012 itakuwa kata ya Tabata.
Kwa kata za Vingunguti,Kipawa,Kiwalani na Buguruni taarifa itatolewa tena ikionyesha tarehe ya ziara kwa kila kata.
Sekretatrieti inaomba ushirikiano kutoka kwa viongozi wote kuanzia ngazi za misingi,matawi na kata husika.
Pamoja tutashinda-M4C
Imetolewa na Katibu wa sekretarieti ya Jimbo la Segerea