TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 24,846
- 11,210
Some quick explanations:
i) Utaratibu wa CHADEMA wa kuteua wabunge ni kama ifuatavyo:
ii) Kuhusu majimbo ya Kilombero na Segerea: Kulikuwa na rufaa kutoka kwa wagombea waliopata kura chache zikilalamikia kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi na misingi ya chama.
- Kamati Tendaji ya Jimbo inafanya uteuzi wa awali, kwa kuwa-rank wagombea kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho. Kamati Tendaji ya Wilaya inaweza kushirikisha wanachama wengine katika jimbo kwa njia ya kura ya maoni ili kujiridhisha na uungwaji mkono wa wagombea husika. Kwa mwaka huu, kulikuwa na waraka maalumu wa Katibu Mkuu unaowataka Makatibu wa Wilaya, pale inapowezekana, kufanya kura ya maoni kabla ya kufanya uteuzi wa awali.
- Kamati Kuu inafanya utafiti kuhusu wagombea wa kila jimbo. Kwa kutumia matokeo ya utafiti na maoni ya Kamati Tendaji za Jimbo inafanya uteuzi wa mwisho. Uteuzi wa Kamati Kuu unaweza kuzingatia maoni ya Kamati Tendaji, Taarifa za utafiti au yote.
- Katika uteuzi wake, Kamati Kuu inazingatia mambo makubwa mawili: Kuchagulika kwa mgombea kwa wananchi wa jimbo na jinsi mchakato wa kumpata mgombea ulivyofanyika-lengo ni kuhakikisha kuwa wagombea wote wanapatikana kwa utaratibu unaozingatia misingi mama ya CHADEMA, namely: maadili na uadilifu, pamoja na taratibu za uchaguzi ndani ya CHADEMA.
iii) Kamati Kuu ilikubaliana na rufaa ya Kilombero na inaendelea kushughulikia.
iii) Kamati Kuu haikukubaliana na rufaa ya Jimbo la Segerea na hivyo iliitupalia mbali.
iv) Katika taarifa ya utafiti iliyowasilishwa, pamoja na umahiri wa kisiasa wa Mhe Masishanga, Kamati Kuu ilijiridhisha kabisa kuwa Mhe Mpendazoe ana nafasi zaidi kwenye nafasi ya ubunge kwa sasa. Mazungumzo yanaendelea kuhakikisha kuwa wananchama hawa wawili wanafanya kazi pamoja kuhakikisha kuwa CHADEMA inashinda ubunge na nafasi za madiwani katika jimbo la Segerea.
Kwa hiyo utaona hapa kuwa utaratibu wa kuwapata wagombea ubunge ndani ya CHADEMA unatofautiana mno na ule wa CCM. Kwa hiyo ulinfganifu uliofanywa sio wa kimantiki.
kitila,
without going deep, inakuaje utaratibu uliouweka wewe mwenyewe, unakiukwa kwenye hiyohiyo taratibu na kuanza kwenda beyond chadema kusema huyu anachagulika au huyu la???
hiyo intelligensia mnayo-apply sasa si mngeitumia toka mwanzo tu m-save pesa basi kwa uchaguzi mkuu??? You guys are contradicting yourselves and the main reason is you look to who has money, which to me say that kwenye procurement na nyinyi mpo
I am just disappointed because you dont practice what you preach