CHADEMA ituwakilishe mazungumzo ya mpaka na Malawi tar 20

Ulukolokwitanga

JF-Expert Member
Sep 18, 2010
8,396
7,968
Kwa kuwa mustakabali wa nchi yetu ni wa miaka mingi ijayo bila kujali chama gani kitatawala miaka hiyo...
Na kwa kuwa serikali hii dhaifu ilifumbia macho suala la mpaka na Malawi ili kuacha huu upepo upite hadi 2015 awamu ya nne iishe...
Na kwa kuwa rais wetu ameonekana anachekacheka mbele ya rais wa Malawi badala ya kuwa serious, achilia mbali udhaifu wa wanaume kwa wanawake...
Na kwa kuwa rais amesema nchi haitaingia vitani na malawi, no matter what, yaani hata malawi wakipora nchi...
Kwa kuwa Membe na serikali hawajui mpaka halisi na Malawi akaliambia bunge kuwa ni 7E to 11E...
Na kwa kuwa ccm imekuwa madarakani miaka 50 bila kutafuta suluhisho la kudumu la mpaka wetu na Malawi...
Na kwa kuwa historia inaonyesha serikali ya CCM ni dhaifu katika majadiliano ya mikataba ya kimataifa, mfano Richmond, Dowans na mikataba yote ya madili, hivyo ni dhahili hawatakuwa na hoja za kuishawishi Malawi kuwa ziwa na pasupasu kati yetu na wao...
Na kwa kuwa viongozi wengi wa ccm ni wapenda rushwa na kuna hadi wabunge wa ccm wanachunguzwa kwa rushwa na wenye kesi mahakamani, hivyo kuwepo uwezekano wa wao kupewa rushwa na Malawi wauze ziwa Nyasa...
Na kwa kuwa tarehe ya Mazungumzo iliwekwa makusudi siku ya sikukuu na hivyo kuwepo uwezekano wa wajumbe wetu kwenda kwenye mazungumzo wakiwa wamelewa au wana hangover, kama alivyowabaini spika Ndugai kuwa kuna wabunge wa CCM wanaingia bungeni wamelewa au wamepiga cha Arusha, kudhihirisha hii ni tabia ndani ya serikali ya ccm...

Napendekeza CDM wakiongozwa na Antipace Tundu Lissu waongoze mazungumzo na Malawi ili haki yetu ya kumiliki maji ya ziwa nyasa isiibiwe mchana kweupe. Haya ni maoni yangu na haki yangu ya kikatiba ya kutoa maoni, sasa tujadili.
 
Mh...sasa chadema washiriki kivipi na wao kama nani?
Kwa uelewa wangu nadhani ni serikali ndio inahusika na mazungumzo hayo...bahati mbaya serikali yenyewe ndio hiyo ya CCM!
 
Chadema inuwezo wa kulalama tu na kuandamana.
Ligi la mazungumzo ya kimataifa ikiwa na maana ya negotiations ni geni kwao.
Wamezoea monologue, kuongea tu na si kusikiliza.
 
Chadema inuwezo wa kulalama tu na kuandamana.
Ligi la mazungumzo ya kimataifa ikiwa na maana ya negotiations ni geni kwao.
Wamezoea monologue, kuongea tu na si kusikiliza.
Tundu Lissu ni mtaalam wa negotiation, akisimama pale hakiharibiki kitu
 
Mh...sasa chadema washiriki kivipi na wao kama nani?
Kwa uelewa wangu nadhani ni serikali ndio inahusika na mazungumzo hayo...bahati mbaya serikali yenyewe ndio hiyo ya CCM!
Kama umesoma magazeti leo serikali ya awamu ya nne ndio inaongoza kwa kutorosha fedha nje ya nchi. Kwa maana hiyo hawa jamaa hawana mpango wa kukaa hapa, hawana maslahi na nchi, watatuuza hawa. Heri tuwakilishwe na wenye uchungu na nchi hata kama hawako madarakani.
We unaona ni halali Wassira kukaa kwenye meza ya majadiliano kisa tu anatoka chama tawala!?
 
Hapa kunatatizo wakuu wangu

Hakuna uwezekano, no matter what? Unless mr president decide otherwise to mix up the negotiating team.

Chadema ni makamanda, wanauwezo na mabingwa wa kusimamia na kutetea hoja zenye mashiko na maslahi kwa taifa, lakin katiba yetu inamtambua kikwete kama amirijesh mkuu na ndie mwenye mamlaka ya kuhakikisha mipaka ya inchi yetu inadum na kulindwa.

Tuendeleze m4c, tuwahamasishe watanzania na kuwaunganisha inchi inzima, vijana kwa wazee waislam kwa wakristu, mabohora, wahindu na wasio na iman, ili 2015 chadema washike hatam ili wapate mamlaka ya kikatiba kuilinda mipaka ya inchi, kutetea maslahi yetu kwa faida yetu kama watanzania na kwa maslahi ya vizazi vyetu hapo baadaye.

Kwa sasa katiba haiwapi nafasi chadema, bali wenyeidhin ni watan wetu ccm na serikali yake.
 
Kwaza nichagie kwamba watu dunia wamekuwa wapubavu sana sababu akili zao zote zimehamia kwenye mali nafaida ya Natural Resources, ndio mana Malawi wanadai kuwa yote lake nyasa yakwao nikwasababu ya ikili finyu kufikilia faida tu sio utu. LAKE NYASA SIO YA MALAWI WALA TANZANIA, wa Geremani nawa Ingereza walikuja wakati kuna watu kuzuguka ziwa hilo mwingereza ninani kuwapokonya watu hao aliwakuta huko.

Hata kichwani haliigii Malawi anawabia watu wa ziwa nyasa upande wa Tanzania kwamba tunawapokonya ziwa hilo kisa mtu akatoka ulaya kwasababu yake akaanza kuwanyima watu haki yao.

Inchi yote yikikubali kwamba kweli watu wetu hawausiki na ziwa hilo, basi wana mpango mbaya Tanzania
 
Kwaza nichagie kwamba watu dunia wamekuwa wapubavu sana sababu akili zao zote zimehamia kwenye mali nafaida ya Natural Resources, ndio mana Malawi wanadai kuwa yote lake nyasa yakwao nikwasababu ya ikili finyu kufikilia faida tu sio utu. LAKE NYASA SIO YA MALAWI WALA TANZANIA, wa Geremani nawa Ingereza walikuja wakati kuna watu kuzuguka ziwa hilo mwingereza ninani kuwapokonya watu hao aliwakuta huko.

Hata kichwani haliigii Malawi anawabia watu wa ziwa nyasa upande wa Tanzania kwamba tunawapokonya ziwa hilo kisa mtu akatoka ulaya kwasababu yake akaanza kuwanyima watu haki yao.

Inchi yote yikikubali kwamba kweli watu wetu hawausiki na ziwa hilo, basi wana mpango mbaya Tanzania
Kama ukiona kicheko na tabasamu la Kikwete wakati anaongea na Joyce ujue nchi imeishauzwa hii.
Resources sio muhimu sana kwani tunazo nyingi tunashindwa kuzitumia na kubakia maskini. Tunataka heshima ya nchi yetu na wananchi wanotumia lile Ziwa kwa maisha yao ya kila siku. Ukisoma gazeti lao la Nyasa times wanasema serikali ya Tanzania imewatelekeza wananchi ndio maana upande wa Tanzania wa ziwa ni maskini kuliko Malawi na Msumbiji
 
chadema ni chama,viongozi wake wanajazba..hawafai kikatiba,wala kwa kufikiria,wao kutuwakilisha.. It seems wangekua madarakan tungekua vitan tayar.. They talk much, tuiache serikali ya ccm ifanye kaz yake.. Kikwete kumchekea joyce hakuna ubaya wowote, usijarib kutupotosha juu ya chochote ulichofikiria wewe.. Chadema haina mamlaka yoyote, na haitoyapata.. Au basi na sisi wa CUF tuje tuwakilishe,mana hata sis tuna uchungu.. Tusiongee tu kwa mapenz ya chama, serikali ipo,na iheshimiwe
 
Back
Top Bottom