Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,580
- 217,964
Kauli ya Dr Magufuli kwamba Tundu Lissu alitelekeza jimbo kwa kipindi chote cha matibabu yake haiwezi kuachwa ikapita hivi hivi kizembe bila kukanushwa na kupingwa , Natambua kwamba wadau wengi wamepinga kauli ile ambayo ni kama inamdhalilisha Tundu Lissu binafsi , inadhalilisha wananchi wa Singida na kwa uhakika inadhalilisha nchi kwa ujumla , lakini kuna haja kwa Chadema yenyewe kama Chama ambacho Tundu Lissu ni kiongozi wake na mhusika mkuu kutoa tamko kuhusiana na uongo huu
Nimesubiri kuona kama chama kinaweza kukanusha huu uongo kwa wakati lakini nimeona kimya , ni lazima sasa viongozi wakuu wa Chadema wajitokeze hadharani kuiambia dunia kwamba kilichozungumzwa ni uongo wa mchana , Tundu Lissu hakutelekeza jimbo lake , yuko nje ya nchi kwa zaidi ya miaka miwili kwa ajili ya Matibabu baada ya kushambuliwa bungeni Dodoma na waliopachikwa jina la kizushi la watu wasiojulikana , huku uchunguzi wa tukio hilo ukiwa umezimwa ikiwa ni pamoja na kung'olewa kwa CCTV camera zilizokuwa eneo la tukio
Uongo ukiachwa bila kukanushwa hugeuzwa kuwa Kweli .
Naomba kuwasilisha
Nimesubiri kuona kama chama kinaweza kukanusha huu uongo kwa wakati lakini nimeona kimya , ni lazima sasa viongozi wakuu wa Chadema wajitokeze hadharani kuiambia dunia kwamba kilichozungumzwa ni uongo wa mchana , Tundu Lissu hakutelekeza jimbo lake , yuko nje ya nchi kwa zaidi ya miaka miwili kwa ajili ya Matibabu baada ya kushambuliwa bungeni Dodoma na waliopachikwa jina la kizushi la watu wasiojulikana , huku uchunguzi wa tukio hilo ukiwa umezimwa ikiwa ni pamoja na kung'olewa kwa CCTV camera zilizokuwa eneo la tukio
Uongo ukiachwa bila kukanushwa hugeuzwa kuwa Kweli .
Naomba kuwasilisha