CHADEMA inatakiwa kuwa makini juu ya mwanajeshi wa JWTZ

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
Heri ya Krismas wadau,

Nimefuatilia kwa kina comments za wadau wa jukwaa hili kufuatia mwanajeshi aliyepiga picha na Lema kwenye mkutano wake pale Mererani.

Katika mazingira ya kawaida tunaweza kusema kumbe hata jeshi limeguswa na ugumu wa maisha, ama kumbe ndani ya jeshi kuna baadhi ya maafande nao wanachukizwa na utawala mbovu wa serikali ya chama cha mapinduzi.

Lakini katika sakata hili la mwanajeshi wa JWTZ kuonyesha mapenzi take kwa chadema, na kudhiriki hata kutamka wazi kuwa yupo tayari hata kufukuzwa kazi ya jeshi kwa ajili ya chadema iangaliwe kwa macho mawili kumtambua vizuri kama ni kweli ana mapenzi ya dhati na chadema, na siyo kwamba anatumiwa kwa ajili ya kuihujumu chadema.

Inawezekana kabisa kuwa labda ni kweli ameguswa na ugumu wa maisha, ama amechukizwa na utawala mbovu wa Jk ambao umesababisha ugumu wa maisha kwa wananchi wakiwamo familia ya mwanajeshi.

Ikumbukwe kuwa Makamba alishawahi kutamka wakati wa kampeni.za uchaguzi 2010 kuwa CCM wana mbinu zaidi ya 100 kuitawala Tanzania.

Pia ikumbukwe kuwa ni majuzi tu tuliweza kusoma tuhuma mbalimbali kupitia mtandao huu juu ya tuhuma zinazowahusu viongozi na wanachama wa chadema kuihujumu chadema.

Ni ukweli usiopingika kuwa hata mkuu wa nchi ankubali kuwa chadema ni tumaini la watanzania. Sasa katika muktadha huo mwanya unaweza kutumika kuwahadaa wananchi, inawezekana amekuja kufanya kazi maalum.

Kauli ya mwanajeshi huyu kusema kuwa yupo tayari kufukuzwa kazi kwa ajili ya kuishabikia chadema inanipa mashaka, mwanajeshi wa jwtz. Inanifanya niamini kuwa yupo kwa kazi maalum kumdadisi au kufiatilia nyendo na kauli za Lema na viongozi wa chadema, pia ili afanikiwe kazi yake maalumu ni lazima atafukuzwa kazi, ambapo chadema na Lema wanaweza kuwekeza imani kwa mwanajeshi huyo. Maana yake ikigundulika kuwa ni kweli ni mwanajeshi wa Jwtz kwa mujibu wa sheria za jeshi adhabu atakayopewa ni kufukuzwa kazi.

Lakini kwakuwa ni kazi maalum, kitakachofanyika itakuwa ni kufukuzwa kazi kama kiini macho, huku akiendelea kupokea mshahara wake kama kawaida, huku akiendelea kukusanya habari na kuripoti kwa waliomtuma.

Kitendo cha Lema kurudi mjengoni kimewaumiza sana serikali ya CCM.

Mfano leo nilikuwa mahali wadau fulani wa taasisi nyeti walikuwa wanazungumza kwamba Lema lazima aundiwe zengwe kwa namna yoyote ile, niliposikia vile nikaanza ku-refer na mjeshi nikaona kuna mchezo.

All in all chadema inaaminika kwa sera za wazi bila kificho, hivyo hata wangeletwa FBI bado ingekuwa shida kwakuwa chadema kimejiwekeza kwenye mioyo ya watanzania, na kubwa zaidi chadema ina mkono wa Mungu.
 
Kweli mkuu angalizo lako, liko sahihi kabisa. Kwa sasa CDM inabidi wazidi kuwa makini zaidi.
 
Mungi kuna haja ya kulitazama upya jambo hili, kwenye thread yako kuna logic, nitarudi
 
Last edited by a moderator:
Mungi kuna haja ya kulitazama upya jambo hili, kwenye thread yako kuna logic, nitarudi
 
Last edited by a moderator:
Poor analysis..Don't scare people, the very military man is genuine supporter and determined to back M4C by all means. He's just a sample among many of them.

I bet you might be a "gamba" sent out for a special mission to scare people. Be informed that many members of the armed forces are behind M4C. You gonna remain with police-CCM and in the end we'll see who is goin' to win the battle of 2nd liberation.

The intelligence within CDM is well organized and more than what u can think of..
 
kwani Tatizo ni Kupiga Picha? Make hata Mjeshi mwenyewe hajatamka wazi zaidi ya Magazeti kumnukuu tu,
 
Njia muhimu na madhubuti ya CCM kuihujumu CDM ni serikali kutekeleza ahadi zake na kuwashughulikia MAFISADI wote. Hizi siasa chafu zimepitwa na wakati, sasa wananchi wanahitaji kuona outputs za ukweli.
 
Inawezekana maana hivi vyombo vinatumika sana kisiasa...kama nilishawahi sikia (znz) watu walovaa kijeshi kukimbia na mibox ya kura..
 
kwani Tatizo ni Kupiga Picha? Make hata Mjeshi mwenyewe hajatamka wazi zaidi ya Magazeti kumnukuu tu,

Tatizo ni mapenzi yake aloonyesha kwa chadema mkuu, pamoja ba matamshi yake kuwa yupo tayari kufukuzwa kazi kwa kuishabikia chadema.................. hapo pia ndo mashaka yanapoanzia.................. kwa uelewa wangu kama jeshi limeamua kufanya mabadiliko siyo lazima mpaka wakajionyeshe hadharani kusapoti vyama vya siasa.

Mfano mwaka 2010 kina kituo cha kupiga kura jeshini ambapo Jk alipata kura tatu tu huki Slaa akiibuka mshindi kwenye hiyo kituo.
kwahiyo kama wanajeshi wamechoshwa na mfumo mbovu kuna njia mbilo tu kufanya mabadiliko, moja ni kupitia sanduku la kura, na pili kupitia military coup!

Hii stile ya mjeshi wa mererani ina mashaka, pia hatukatai kwakuwa hauwezi kijua hisia za mtu, inawezekana ni mapenzi yake kitoka moyoni mwake yalimfanya awe hivyo, kama siyo yupo kwa kazi maalum
 
Ok. Ila sioni ni kwa namna gani CDM wanaweza kumpa huyo "mjeda" umuhimu kiasi cha kupata upenyo na fursa ya kuwa informer. Mnawaogopa mamluki kiasi hicho mpk mmefikia hatua ya kutafsiri kila tukio??? No. CDM is in the next level bana, vitu sampuli hii visiwatishe
 
Hilo isiwape hofu cha muhimu chama kilinde uadhilifu kama kuna mtu analengo mbaya hatafanikiwa maana mkiogopa kuwashirikisha wanaotaka kuunga harakati itakuwa tatizo. TUMKARIBISHE ANAYEUNGA HARAKATI BILA WOGA.
 
Ok. Ila sioni ni kwa namna gani CDM wanaweza kumpa huyo "mjeda" umuhimu kiasi cha kupata upenyo na fursa ya kuwa informer. Mnawaogopa mamluki kiasi hicho mpk mmefikia hatua ya kutafsiri kila tukio??? No. CDM is in the next level bana, vitu sampuli hii visiwatishe

Mkuu wanaojua chadema is the next level ni chadema, serikali na chama tawala hawajui hilo.
pia tunachosema ni kwamba inawezekana amepewa kazi maalumu ili awepo kwenye mikutano ya M4C kurekodi baadhi ya matamshi ili kumhujumu Lema ama kiongozi mwingine yeyote.
Sote tunajua mtu kama Lema amekuwa mwiba kwa serikali ya ccm na ccm, hivyo kurudi kwake mjengoni ni sawa na kufanyiwa tohara bila ganzi!
Fikiria tu baada ya siku mbili tu Lema anatangazwa mshindi na mjeshi anajitokeza yupo full shangwe!
Umakini unahitajika
 
Tusimhofu kisa mwanajeshi, wanaotumika wanaweza ingia kwa njia nyingine nying tu. Ndo maana ukiangalia tayari kuna watu tunao wanaosaliti au ku2mika na wanafahamika. Mm nashauri 2siwaogope wanaunga hzi harakati lkn wasaliti watimuliwe wote.
 
mkuu wanaojua chadema is the next level ni chadema, serikali na chama tawala hawajui hilo.
Pia tunachosema ni kwamba inawezekana amepewa kazi maalumu ili awepo kwenye mikutano ya m4c kurekodi baadhi ya matamshi ili kumhujumu lema ama kiongozi mwingine yeyote.
Sote tunajua mtu kama lema amekuwa mwiba kwa serikali ya ccm na ccm, hivyo kurudi kwake mjengoni ni sawa na kufanyiwa tohara bila ganzi!
Fikiria tu baada ya siku mbili tu lema anatangazwa mshindi na mjeshi anajitokeza yupo full shangwe!
Umakini unahitajika

acheni hofu ataricord nn mi nachoamin viongoz wa cdm siwatukanaji mbali wanaenda kuelisha wananchi.
 
Mkuu wanaojua chadema is the next level ni chadema, serikali na chama tawala hawajui hilo.
pia tunachosema ni kwamba inawezekana amepewa kazi maalumu ili awepo kwenye mikutano ya M4C kurekodi baadhi ya matamshi ili kumhujumu Lema ama kiongozi mwingine yeyote.
Sote tunajua mtu kama Lema amekuwa mwiba kwa serikali ya ccm na ccm, hivyo kurudi kwake mjengoni ni sawa na kufanyiwa tohara bila ganzi!
Fikiria tu baada ya siku mbili tu Lema anatangazwa mshindi na mjeshi anajitokeza yupo full shangwe!
Umakini unahitajika

Kwenye red ndo kwenye hoja dhaifu Mungi. Kwani hao wabaya wa Lema wana uhakika gani huyo "mjeda" anaweza ku-deliver kile ambacho wengine wameshindwa??? Kurekodiwa kwa Lema na kufuatiliwa nyendo zake hakujaanza leo mkuu. Naheshimu sana mawazo yako mkuu, ila ninachoomba hapa ni hiki: tusimpe umaarufu asiostahili huyu jamaa. Wameshindwa akina ZZK na masalia wenzake ndo aje huyu mjeda feki??? Usiogope mkuu, wala usiwe chanzo cha hofu kwa makamanda wengine.
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom