Nicky82
JF-Expert Member
- Mar 14, 2009
- 941
- 64
Mara nyingi tumewasikia viongozi wa CHADEMA wakisema kuwa wanakijenga chama na kukiandaa kushika dola baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa 2015, lakini hawasikiki wakielezea kwa msisitizo ulio sawa kuhusu uchaguzi wa serikali za vijiji/mitaa wa 2014.
Katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2009, CHADEMA walilalamika kuwa wagombea wao wengi walikosa sifa za kushiriki uchaguzi ule kwa sababu utaratibu wa uchaguzi uliwataka wagombea wachaguliwe katika ngazi za vijiji na mitaa wanakoishi, huko ambako katika maeneo mengi CHADEMA hawana matawi/ofisi za chama na hivyo kutoa nafasi kwa wagombea wengi wa CCM kupita ama bila kupingwa au kushinda kwa kishindo na overall ya matokeo kuipa CCM usindi wa 97% nchi nzima.
Nilifikiri lile lingekuwa somo kwa CHADEMA kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa 2014, lakini wengi wa viongozi wanahubiri uchaguzi wa 2015 wakisahau umuhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2014
Itakuwa kazi ngumu sana kwa CHADEMA kushinda mwaka 2015 ikiwa kama watashindwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2014. Sababu ziko wazi;
Kwanza, kuruhusu kushindwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kutawavunja nguvu wafuasi wao, na itawapa CCM nguvu ya campaign huku ikiwaaminisha watu kuwa kama CHADEMA wameshindwa kutawala vijiji basi hawawezi kutawala majimbo/taifa
Pili, mara nyingi tumeshudia CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vikinyimwa maeneo hata ya kufanyia mikutano yao ya kampeni, au mikutano yao kuhujumiwa. Lakini kama wao ndo watakuwa watawala wa hayo maeneo itakuwa rahisi wao kuzuia na kupambana na hujuma zozote, na kinyume chake ni kuwa kama watashindwa basi kwenye hayo maeneo, wimbo wa hujuma utaendelea kusikika.
Tatu, tumeshuhudia CHADEMA ikikosa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura sababu ya kukosa kuwepo kwa watu wenye kulisimamia hili. Lakini uwepo wa serikali inayoongozwa na chama chao itasaidi kuognize watu wa kwenda kusimamia vituoni.
Nne, Uhujumu wa matokeo hufanyika kirahisi pale ambapo hakuna mtu wa kusimamia kile kilicho hesabiwa kuwa ndo kama kile kinachowasilishwa, pia hata katika usimamizi wa kuwachagua wasimamizi wasidizi wa tume, uwepo wa uwakilishi wa chama katika maeneo husika utasaidi kupunguza hatari ya kuchomekwa kwawasimamizi wasio waminifu watakaokuwa na nia ya kupendelea chama tawala
Nawashauri CHADEMA badala ya kuconcentrate kwenye uchaguzi wa 2015, ni vema wakaelekeza nguvu zao kwenye uchaguzi wa 2014, kwa kufanyia kazi yale mapungufu yaliyowaengua mwaka 2009 kwa kuhakikisha wanajenga na kuimarisha matawi kuanzia ngazi ya vijiji/mitaa kwani mfumo huu ndo umekuwa mtaji mkubwa wa CCM na kwa kufanya hayo automatically watakuwa wanajenga mfumo kwa ajili ya kutimiza azma yao ya kuchukua nchi 2015.
Ni wakati sasa wa kila mbunge mchaguliwa na mteuliwa kuhakikisha anaimarisha chama jimboni kwake na mkoa wake ili kukipa chama mfumo imara wenye nguvu kuanzia ngazi ya mashina, vinginevyo itakuwa ngumu sana kushinda 2015.
Angalizo
Ili kushinda uchaguzi ni lazima chama kiwe na mfumo tangu ngazi ya shina.
Wengine wanaweza wakafikiri kuwa wimbi la 2015 huenda likafanana na 2010, lakini tukumbuke kuwa mazingira ya wimbi la ushabiki na mvuto aliokuwa nao mgombea wa CHADEMA mwaka 2010 yanaweza kuwa tofauti na mwaka 2015.......hivyo ni wajibu wa chama kujijenga kimfumo kuanzia ngazi ya shina, na kazi hii ilipaswa kuanza miezi 9 iliyopita...........yawezekana imeshaanza lakini kasi yake haitoshi inabidi kuongezwa.
Wananchi wanapaswa kuandaliwa kushika madaraka kwa chama chao kuanzia ngazi ya vijiji/mitaa na ndipo sasa kazi ya kushika dola itakuwa rahisi. Wakijisahau, kuna hatari ya kufika 2015 na chama kikaonekana bado hakina uwezo wa kuaminika kupewa dola.
Katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2009, CHADEMA walilalamika kuwa wagombea wao wengi walikosa sifa za kushiriki uchaguzi ule kwa sababu utaratibu wa uchaguzi uliwataka wagombea wachaguliwe katika ngazi za vijiji na mitaa wanakoishi, huko ambako katika maeneo mengi CHADEMA hawana matawi/ofisi za chama na hivyo kutoa nafasi kwa wagombea wengi wa CCM kupita ama bila kupingwa au kushinda kwa kishindo na overall ya matokeo kuipa CCM usindi wa 97% nchi nzima.
Nilifikiri lile lingekuwa somo kwa CHADEMA kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa 2014, lakini wengi wa viongozi wanahubiri uchaguzi wa 2015 wakisahau umuhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2014
Itakuwa kazi ngumu sana kwa CHADEMA kushinda mwaka 2015 ikiwa kama watashindwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2014. Sababu ziko wazi;
Kwanza, kuruhusu kushindwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kutawavunja nguvu wafuasi wao, na itawapa CCM nguvu ya campaign huku ikiwaaminisha watu kuwa kama CHADEMA wameshindwa kutawala vijiji basi hawawezi kutawala majimbo/taifa
Pili, mara nyingi tumeshudia CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vikinyimwa maeneo hata ya kufanyia mikutano yao ya kampeni, au mikutano yao kuhujumiwa. Lakini kama wao ndo watakuwa watawala wa hayo maeneo itakuwa rahisi wao kuzuia na kupambana na hujuma zozote, na kinyume chake ni kuwa kama watashindwa basi kwenye hayo maeneo, wimbo wa hujuma utaendelea kusikika.
Tatu, tumeshuhudia CHADEMA ikikosa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura sababu ya kukosa kuwepo kwa watu wenye kulisimamia hili. Lakini uwepo wa serikali inayoongozwa na chama chao itasaidi kuognize watu wa kwenda kusimamia vituoni.
Nne, Uhujumu wa matokeo hufanyika kirahisi pale ambapo hakuna mtu wa kusimamia kile kilicho hesabiwa kuwa ndo kama kile kinachowasilishwa, pia hata katika usimamizi wa kuwachagua wasimamizi wasidizi wa tume, uwepo wa uwakilishi wa chama katika maeneo husika utasaidi kupunguza hatari ya kuchomekwa kwawasimamizi wasio waminifu watakaokuwa na nia ya kupendelea chama tawala
Nawashauri CHADEMA badala ya kuconcentrate kwenye uchaguzi wa 2015, ni vema wakaelekeza nguvu zao kwenye uchaguzi wa 2014, kwa kufanyia kazi yale mapungufu yaliyowaengua mwaka 2009 kwa kuhakikisha wanajenga na kuimarisha matawi kuanzia ngazi ya vijiji/mitaa kwani mfumo huu ndo umekuwa mtaji mkubwa wa CCM na kwa kufanya hayo automatically watakuwa wanajenga mfumo kwa ajili ya kutimiza azma yao ya kuchukua nchi 2015.
Ni wakati sasa wa kila mbunge mchaguliwa na mteuliwa kuhakikisha anaimarisha chama jimboni kwake na mkoa wake ili kukipa chama mfumo imara wenye nguvu kuanzia ngazi ya mashina, vinginevyo itakuwa ngumu sana kushinda 2015.
Angalizo
Ili kushinda uchaguzi ni lazima chama kiwe na mfumo tangu ngazi ya shina.
Wengine wanaweza wakafikiri kuwa wimbi la 2015 huenda likafanana na 2010, lakini tukumbuke kuwa mazingira ya wimbi la ushabiki na mvuto aliokuwa nao mgombea wa CHADEMA mwaka 2010 yanaweza kuwa tofauti na mwaka 2015.......hivyo ni wajibu wa chama kujijenga kimfumo kuanzia ngazi ya shina, na kazi hii ilipaswa kuanza miezi 9 iliyopita...........yawezekana imeshaanza lakini kasi yake haitoshi inabidi kuongezwa.
Wananchi wanapaswa kuandaliwa kushika madaraka kwa chama chao kuanzia ngazi ya vijiji/mitaa na ndipo sasa kazi ya kushika dola itakuwa rahisi. Wakijisahau, kuna hatari ya kufika 2015 na chama kikaonekana bado hakina uwezo wa kuaminika kupewa dola.