Ni ukweli kuwa vyama vya siasa vimeundwa na binadamu, hivyo kuwepo au kutokuwepo kwake kunategemea akili za binadamu. Tofauti na ardhi na vyote vilivyomo ambavyo kwa pamoja hujulikana kama nchi, vilivyoumbwa na mwenyezi mungu.
Hivyo Tanzania itaendelea kuwepo hata kama vyama vyama vya siasa vitaendelea kuwepo au kufutika kabisa. Hivyo mantiki na busara inanielekeza kuwa nchi ni bora kuliko chama.
Kutokana na ubovu wa sheria zetu, watawala wetu wa CCM wanatulazimisha watanzania wote tunaotaka kushiriki kwa namna moja au nyingine katika uongozi wa nchi yetu kupitia katika vyama vya siasa. Awali chama kilikuwa kimoja tu yaani TANU na baadaye CCM hivyo wengi wetu tulilazimka kuwa katika chama hicho. Ujio wa vyama vingi kidogo kidogo ukaanza kutoa uhuru wa mawazo, maoni na kupingana bila kupigana na leo ndio tulipo katika mhjadala wa katiba mpya.
Kwa kuwa vyama vya siasa navyo hubuniwa na kuongozwa na binadamu mara nyingi udhaifu wa binadamu ndani ya vyama vya siasa hususan viongozi mara nyingi hukiganda chama husika kama ambavyo CCM ilivyogandwa na ufisadi baada ya kuchelewa kuwashughulikia watu wenye tuhuma za ufisadi ndani ya CCM.
Tukio la hivi karibuni la Diwani wa chama chetu wa CHADEMA kukutwa na silaha ya kivita AK 47 haliwezi kupita hivi hivi kwa watu wazima wenye mapenzi mema na nchi yetu ambao kila kukicha tunapoteza raslimali na muda kupambana na vitendo viovu ndani ya jamii yetu.
Naomba kuuliza uongozi wa CHADEMA unachukua hatua gani dhidi ya Diwani wetu alikutwa na silaha ya kivita? Kutokana na ufisadi uliotalamaki ndani ya CCM tumepata taabu sana kuikuza CHADEMA ili angalau sauti za watanzania wanyonge ziweze kusikika. Hivyo hatuwezi kuvumilia mambo ya kuoneana haya na kukaa nyumba moja aina ya watu kama diwani huyu. Kwa kuwa hizi ni tuhuma nzito, hata kama Serikali imeamua kumsamehe naomba sisi wanachama wa CHADEMA tusimsamehe. Hakuna kutafuta ushaidi wala nini, ni yeye mwenyewe aliyjiweka katika mazingira ya kuchafuaka hivyo ang'oke kwa kuwa ametuchafua wote.
Nashauri hakuna kuhurumia kata itapotea wala nini atakiwe ajihudhuru mara moja au afukuzwe na uchaguzi mdogo ufanyike hata tukipoteza kata hiyo potelea mabili ilikuwa ni katika jitihada za kulinda maadili mema.
Naomba kuwasilisha!!!!
Hivyo Tanzania itaendelea kuwepo hata kama vyama vyama vya siasa vitaendelea kuwepo au kufutika kabisa. Hivyo mantiki na busara inanielekeza kuwa nchi ni bora kuliko chama.
Kutokana na ubovu wa sheria zetu, watawala wetu wa CCM wanatulazimisha watanzania wote tunaotaka kushiriki kwa namna moja au nyingine katika uongozi wa nchi yetu kupitia katika vyama vya siasa. Awali chama kilikuwa kimoja tu yaani TANU na baadaye CCM hivyo wengi wetu tulilazimka kuwa katika chama hicho. Ujio wa vyama vingi kidogo kidogo ukaanza kutoa uhuru wa mawazo, maoni na kupingana bila kupigana na leo ndio tulipo katika mhjadala wa katiba mpya.
Kwa kuwa vyama vya siasa navyo hubuniwa na kuongozwa na binadamu mara nyingi udhaifu wa binadamu ndani ya vyama vya siasa hususan viongozi mara nyingi hukiganda chama husika kama ambavyo CCM ilivyogandwa na ufisadi baada ya kuchelewa kuwashughulikia watu wenye tuhuma za ufisadi ndani ya CCM.
Tukio la hivi karibuni la Diwani wa chama chetu wa CHADEMA kukutwa na silaha ya kivita AK 47 haliwezi kupita hivi hivi kwa watu wazima wenye mapenzi mema na nchi yetu ambao kila kukicha tunapoteza raslimali na muda kupambana na vitendo viovu ndani ya jamii yetu.
Naomba kuuliza uongozi wa CHADEMA unachukua hatua gani dhidi ya Diwani wetu alikutwa na silaha ya kivita? Kutokana na ufisadi uliotalamaki ndani ya CCM tumepata taabu sana kuikuza CHADEMA ili angalau sauti za watanzania wanyonge ziweze kusikika. Hivyo hatuwezi kuvumilia mambo ya kuoneana haya na kukaa nyumba moja aina ya watu kama diwani huyu. Kwa kuwa hizi ni tuhuma nzito, hata kama Serikali imeamua kumsamehe naomba sisi wanachama wa CHADEMA tusimsamehe. Hakuna kutafuta ushaidi wala nini, ni yeye mwenyewe aliyjiweka katika mazingira ya kuchafuaka hivyo ang'oke kwa kuwa ametuchafua wote.
Nashauri hakuna kuhurumia kata itapotea wala nini atakiwe ajihudhuru mara moja au afukuzwe na uchaguzi mdogo ufanyike hata tukipoteza kata hiyo potelea mabili ilikuwa ni katika jitihada za kulinda maadili mema.
Naomba kuwasilisha!!!!