The golden
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 1,381
- 2,553
Nilianza kukifahamu hiki chama mwaka 2005 ,kipindi kile Free man anagombea urais . Alifika huku Arusha kwa helkopita huku akiwa amevaa mavazi Fulani hivi aina ya kombati. Vazi hili lilivutia vijana wengi kipindi kile. Sikuwa namfahamu vizuri huyu jamaa labda kwa sababu ya umri wangu kipindi hicho .
Tangu nyakati hizo nimekuwa nakifuatilia sana hiki chama ,pamoja na baadhi ya viongozi wake .
Chadema kama vilivyo vyama vingine au kama tulivyo binadamu wote wamekuwa na mapungufu yao ya kawaida ambayo kama chama lazima wakae chini na kuyatafutia ufumbuzi.
Lakini naomba niseme ukweli pamoja na mapungufu yao kama chama , chama hiki kina bahati ya kupata viongozi wenye vipaji na ushawishi ukubwa. Hapo nyuma kidogo walikuwepo watu kama Zito, Dr Slaa na wengine wengi ambao kwa hakika walikuwa na mvuto wa ajabu.
Leo nimeona press iliyofanywa na jamaa ambaye namfahamu kwa jina moja tu Benson , huyu jamaa siyo wa kawaida .Nimejionea uwezo wake kutoa maelezo na kujibu maswali ni wa kiwango cha juu kabisa huwezi kuchoka kumsikiliza . Watu kama Benson lazima watafutiwe watu makini wa kujibizana nao.
Hapa sitaki kuwataja wengine kama yule anayetibiwa huko nje . Unaweza kudhani labda wameisha wanaoweza kuzungumza kumbe bado wapo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tangu nyakati hizo nimekuwa nakifuatilia sana hiki chama ,pamoja na baadhi ya viongozi wake .
Chadema kama vilivyo vyama vingine au kama tulivyo binadamu wote wamekuwa na mapungufu yao ya kawaida ambayo kama chama lazima wakae chini na kuyatafutia ufumbuzi.
Lakini naomba niseme ukweli pamoja na mapungufu yao kama chama , chama hiki kina bahati ya kupata viongozi wenye vipaji na ushawishi ukubwa. Hapo nyuma kidogo walikuwepo watu kama Zito, Dr Slaa na wengine wengi ambao kwa hakika walikuwa na mvuto wa ajabu.
Leo nimeona press iliyofanywa na jamaa ambaye namfahamu kwa jina moja tu Benson , huyu jamaa siyo wa kawaida .Nimejionea uwezo wake kutoa maelezo na kujibu maswali ni wa kiwango cha juu kabisa huwezi kuchoka kumsikiliza . Watu kama Benson lazima watafutiwe watu makini wa kujibizana nao.
Hapa sitaki kuwataja wengine kama yule anayetibiwa huko nje . Unaweza kudhani labda wameisha wanaoweza kuzungumza kumbe bado wapo.
Sent using Jamii Forums mobile app