CHADEMA imeweka Mgombea jimbo la Konde. Je, ni kuhalalisha Tume ya Uchaguzi?

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
319
345
Katika siku za hivi karibuni Chama cha Demokrasia na maendeleo, kupitia viongozi, wanachama na washabiki wake kote nchini, waliutangazia umma kuwa hawatashiriki uchaguzi wowote kama hakutakuwa na tume huru ya Uchaguzi.

Mbaya zaidi ikakinyooshea kidole chama cha ACT Wazalendo, kilichoshiriki katika chaguzi za marudio kwenye majimbo ya Buhingwe na Muhambwe na kueleza kuwa chama hicho kinatumika kuisafisha CCM kutokana na makando kando ya uchaguzi wa 2020.

Kama haitoshi wakawaonya hata wananchi walioamini kuwa ni wapiga kura wasioweza kuipigia CCM wasiende kumchagua mgombea wa ACT katika chaguzi hizo kwa kuwa chama hakitambui juu ya uchaguzi huo.

Ikumbukwe katika majimbo hayo ya Buhigwe na Muhambwe CCM ndiyo waliokuwa wanawakilisha awali na nguvu yoyote ya upinzani ilikuwa inaiminya CCM kupata ushindi,lakini Chadema wakasusa na wakazuia watu wao wasipige kura.

Kiufupi waliwaambia CCM sisi hatushiriki na kura zetu hatuwapigii wapinzani wengine ili CCM ishinde.

Leo haijatimia hata miezi miwili katika jimbo la Konde kisiwani Pemba ambako kulikuwa na Mbunge anayetokana na ACT Wazalendo kabla ya kukutwa na umauti Chadema imesimamisha mgombea kwa lengo la kwenda kupambana na ACT na kuipa afueni CCM inayohaha kulitwaa jimbo hilo.

Konde.jpg

Maswali yangu Kwa wanachadema ni haya:
1. Je, tume huru imepatikana?

2. Lengo la ushiriki wa Uchaguzi huo ni lipi zaidi ya kuisaidia CCM jimbo la Konde?

3. Kwanini hawakushiriki uchaguzi wa Muhambwe na Buhigwe ambako CCM ilikuwa inatetea majimbo hayo,tofauti na sasa ambako Konde ACT ndiyo inatetea jimbo hilo?

Ni lini Chadema itaacha kuwapelekesha wanachama wake kama mazuzu kwa kuwaaminisha ambavyo haviaminiwi na viongozi wao?

CC Freeman Mbowe, Heche, Msigwa, Maria Sarungi.

Zaidi, soma: CHADEMA wachanganyana uchaguzi jimbo la Konde, Wadai Mgombea hawajampitisha wao
 
"za kuambiwa changanya na zako".

Ukiwa mfia chama lazma ufate kile kitachosemwa hata kama si chema wengi hukilazimisha kwa sababu hata zisizo za msingi kua chema,(unafki).

Ipo kote kote hii si huku wala kule.
 
Maswali yangu Kwa wanachadema ni haya

1.Je, tume huru imepatikana?
Tume huru iliyo lalamikiwa ni ipi? Au hujui kuwa Kuna ZEC na NEC.

Halafu wewe mkurupukaji ktk siasa ni kama hali ya hewa muda wowote hubadilika. Hakuna kauli wala rafiki wa kudumu. Kama hulitaki hili acha kushabikia siasa.

Mfano Walioimba nyimbo za kumwabudu Magufuli mwezi February leo ukiwatajia jina hilo watakupiga hata ngumi.
 
Tume huru iliyo lalamikiwa ni ipi? Au hujui kuwa Kuna ZEC na NEC.

Halafu wewe mkurupukaji ktk siasa ni kama hali ya hewa muda wowote hubadilika. Hakuna kauli wala rafiki wa kudumu. Kama hulitaki hili acha kushabikia siasa.

Mfano Walioimba nyimbo za kumwabudu Magufuli mwezi February leo ukiwatajia jina hilo watakupiga hata ngumi.
Uchaguzi wa ubunge unasimamiwa na NEC
 
Viongozi CHADEMA wapo Pemba, ACT = CCMB wanaona wananyang’a nywa wanamageuzi . Wameamua kuleta huu Upuuzi.
 
Alama za mtu mnafiki ni tatu

Mliwacheka ACT walivyoweka mgombea kule kigoma mkawatukana sasa nyie si mlisema hamuweki wagombea, haya huyu wa jimbo la konde imekuaje tena
FB_IMG_16255668169175650.jpg
 
Alama za mtu mnafiki ni tatu

Mliwacheka ACT walivyoweka mgombea kule kigoma mkawatukana sasa nyie si mlisema hamuweki wagombea, haya huyu wa jimbo la konde imekuaje tenaView attachment 1843194
Chadema hawa Akili za kijinga za ACT na CCM kuweka Mgombea Huko Chadema Weshasema Hawashiri Chaguzi za KIHUNI ni Utoto wa hivyo Vyama Kupotosha Umma
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom