CHADEMA imeshinda chaguzi kwa nguvu ya umma sio Tume ya Uchaguzi. Tusidanganywe

...
...Sababu ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ni hila na nongwa, na ni hiyo ninayokuambia katiba kutoa nguvu kubwa kwa rais kiasi kwamba anaweza kufanya maamuzi kwa kutegemea hisia zake. Kwenye mahali taasisi zilizo na nguvu msajili wa vyama vya siasa alipaswa kumuambia rais hapa unakosea kwa kuminya uhuru wa vyama vya siasa kufanya shughuli zake. ...
Niseme tu kuwa hoja zako zinajikita katika upinzani kupata mwanya/uwanja mpana wa kutangaza sera zake. Nakubaliana na wewe kwa hilo. Ni mapungufu katika dhana pana ya demokrasia.

Hata vile, uwanja finyu (mitandao ya kijamii na vyombo vya habari) walio nao upinzani, na wafuasi wao, hata humu JF, hawautumii kunadi na kuelezea sera mbadala zenye tija kwa maendeleo ya nchi. Isipokuwa hutumia mianya hiyo kukebehi, kutukana, kulaumu nk Rais Magufuli na Serikali yake. Mfano mzuri nivwa hivi karibuni kwenye kampeni za uchaguzi wa marudio Kata 43, ambapo kampeni za upinzani hazikulenga kuleta mabadiliko kwenye kata hizo, dhidi ya Serikali. Walitumia muda mwingi kuilaumu Serikali. Kuna ushahidi wa kutisha kuthibitisha hilo.

Kama kweli upinzani una nia ya dhati ya kutawala Tanzania na kuiongoza kwenye mabadiliko chanya ya maendeleo, hakuna sababu ya kulumbana na Serikali kwa maneno ya kejeli na lawama, ilakutekeleza kwa vitendo sera na ilani yao ya uchaguzi katika majimbo wanayoongoza.

BINADAMU HUJIFUNZA KWA MIFANO
 
Niseme tu kuwa hoja zako zinajikita katika upinzani kupata mwanya/uwanja mpana wa kutangaza sera zake. Nakubaliana na wewe kwa hilo. Ni mapungufu katika dhana pana ya demokrasia.

Hata vile, uwanja finyu (mitandao ya kijamii na vyombo vya habari) walio nao upinzani, na wafuasi wao, hata humu JF, hawautumii kunadi na kuelezea sera mbadala zenye tija kwa maendeleo ya nchi. Isipokuwa hutumia mianya hiyo kukebehi, kutukana, kulaumu nk Rais Magufuli na Serikali yake. Mfano mzuri nivwa hivi karibuni kwenye kampeni za uchaguzi wa marudio Kata 43, ambapo kampeni za upinzani hazikulenga kuleta mabadiliko kwenye kata hizo, dhidi ya Serikali. Walitumia muda mwingi kuilaumu Serikali. Kuna ushahidi wa kutisha kuthibitisha hilo.

Kama kweli upinzani una nia ya dhati ya kutawala Tanzania na kuiongoza kwenye mabadiliko chanya ya maendeleo, hakuna sababu ya kulumbana na Serikali kwa maneno ya kejeli na lawama, ilakutekeleza kwa vitendo sera na ilani yao ya uchaguzi katika majimbo wanayoongoza.

BINADAMU HUJIFUNZA KWA MIFANO

Wangalau umepata ninachomaanisha. Ninashukuru kwa hilo. Kuuza sera ni kazi ya chama, hata mimi hili nimekuwa nikiwataka wapinzani wakipata nafasi hata ndogo waonyeshe kipi wanaweza kuwafanyia wananchi kimaendeleo badala ya kujikita kwenye siasa za madaraka tu. Huu ni udhaifu wa wazi wa wapinzani, ila kupitia mijadala ya aina hii watarekebishika. Kukebehi na kulaumu inakubalika kiushindani ila siungi wala sijiwahi kuunga mkono matusi. Kikubwa ambacho mimi sikukubaliana nacho kwenye uchaguzi ule na ambao hata sasa nasisitizi wapinzani kutoshiriki uchaguzi ni tabia za kinyama zilizofanyika. Maana nijuavyo kama mtu hahubiri suluhu ya matatizo ya wananchi basi wananchi ndio waamuzi na sio ukatili na unyama huku ukiratibiwa na vyombo vya dola. Kibaya zaidi ni uporaji wa ushindi kwa washindi halali.

Kejeli sio sawa kwa wapinzani kuzitumia japo ndio siasa zetu kwani hata ccm wanatumia kejeli tena za wazi, ila ccm ndio walioshika mpini hivyo wapinzani wanapaswa kuwa wajanja kwenye hili. Kwenye halmashauri wanazoongoza wapinzani kuna ubunifu unaoonekana japo wanakutana na wakati mgumu kutokana na aina ya siasa zetu kutompa mpinzani wako nafasi ya kung'aa. Fitina za hivi wangalau zinavumilika lakini sio zile la kukatana mapanga na kuachiana vilema vya kudumu, tena kwa uratibu wa vyombo vya usalama. zile sio siasa za nchi yetu.
 
... Kuuza sera ni kazi ya chama, hata mimi hili nimekuwa nikiwataka wapinzani wakipata nafasi hata ndogo waonyeshe kipi wanaweza kuwafanyia wananchi kimaendeleo badala ya kujikita kwenye siasa za madaraka tu. Huu ni udhaifu wa wazi wa wapinzani, ila kupitia mijadala ya aina hii watarekebishika. ...

... wananchi ndio waamuzi na sio [CLOR=RED]ukatili na unyama huku ukiratibiwa na vyombo vya dola[/COLOR]. Kibaya zaidi ni uporaji wa ushindi kwa washindi halali.

... Kwenye halmashauri wanazoongoza wapinzani kuna ubunifu unaoonekana japo wanakutana na wakati mgumu kutokana na aina ya siasa zetu kutompa mpinzani wako nafasi ya kung'aa. ...
JE, hiyo nafasi finyu ya kujinadi inatumika kwa faida au ndiyo hiyo ya kufitinisha wananchi na Serikali kama mataji wa kisiasa!

Hakuna ushahidi wowote unaothibitisha kuwa jitihada za upinzani kuwaletea wananchi maendeleo zinapigwa vita na Serikali. Kama kuna ukweli wa aina hiyo na bado wananchi hao hao wanaimani Serikali na chama chake, basi Watanzania tuna matatizo makubwa.

Kwamba ushindi wa CCM ni wa kutumia nguvu ya vyombo vya dola, na bado mwananchi anakipigia kura hicho chama, na aliyeumizwa hachukui hatua za kisheria, basi tena, Watanzania tuna safari ndefu ya kujiamini.

Hivi pamoja na kuwepo wasomi, wazoefu na nguri wa kisiasa, upinzani, bado hakuna wa kiongozi huko mbunifu wa kupambana na hizo mbinu? Najiuliza tu: Hivi nchi hii ikiongozwa na upinzani kuna kiongozi wa kupambana na nguvu za kisiasa na kiuchumi za mataifa makubwa, au ndiyo itakuwa lalama lalama, kama tunayoishudia sasa dhidi ya nguvu za uongozi wa ndani?

WAKATI NDIYO HUU TUSINYANG'ANYANE VITO KUJENGA NYUMBA MOJA
 
Back
Top Bottom