Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,220
- 9,647
Ndugu zangu Watanzania
Baada ya kufunguliwa na kuruhusiwa kwa mikutano ya vyama vya siasa hapa nchini tulishuhudia mbwembwe na vitisho vya hapa na pale kutoka kwa viongozi na wanachama wa chadema kuwa Wana kwenda kutikisa na kuipa shida CCM.
lakini Cha ajabu Baada ya ufunguzi wa mikutano Yao kilichofuata ni kichekesho na fedheha kubwa Sana, maana badala ya kuwaunganisha wanachama wake wamebaki wamegawanyika na kuanza kutafutana Ni Nani mchawi na msaliti wa chama,Ni Nani Kamanda wa ukweli na Nani aliye ramba asali nyingi,Ni Nani Ni CCM B na Nani anatakiwa kumpisha fulani,Ni Nani amepanda kalewa jukwaani na Nani kazungumza masuala ya wananchi.
Tumeshuhudia Wana chadema wakilaumiana na kutiliana mashaka wao kwa wao,kwamba kwanini Mwenyekiti hajawashambulia Sana CCM ,kwanini amempongeza Mwenyekiti wa CCM,kwanini sauti yake ilikuwa hivi na vile, yaani Sasa chama kina mpasuko mkubwa huku wengi wakimsubili Lisu ili waje wasikie atatukana matusi mangapi,wao furaha Yao Ni kutaka kuona anayepanda jukwaani anaropoka matusi utafikiri kakatika mishipa ya fahamu na kuvuruga ubongo wake.
Kinachowachanganya Zaid Ni mapokeo ya watanzania kwa namna walivyo wapuuza na kuwadharau kwa Sasa,maana wanaona watanzania hawana habari nao,hawana habari na mikutano Yao,wanawakosoa na kuwapinga kila mahali,wanamtetea, kumsemea na kumpongeza Rais Samia kwa uchapa kazi wake uliotukuka na kuahidi kumuunga mkono katika kila hatua ya ujenzi wa Taifa letu.
Kwa Sasa Chadema Imepoteza ule mvuto na ushawishi iliokuwa nao kutokana na utendaji kazi wa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani kufanyia kazi kero na changamoto zote zinazogusa na kuwa kikwazo katika maisha yao,wameona chadema Ni watu wasio na misimamo na vigeu geu,wameona chadema Ni njaa tupu tu na mkusanyiko wa wasaka tonge,ndio sababu ya Kuendelea kuwa na Imani na CCM na serikali yake chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Mama Samia.
CHADEMA kimebaki Ni chama kisicho na dira Wala muelekeo,hakina ajenda Wala Sera kinayoisimamia yenye kuwashawishi watanzania kuwaunga mkono,Hakina watu Wala viongozi wenye ushawishi na wenye kuteka hisia za watanzania,Hawana kiongozi au viongozi wenye uwezo wa Kuiteka mioyo ya watanzania kuweza kuwaunga mkono katika harakati zao,Hakina ngome yoyote kutoka kundi lolote katika jamii yetu,
Ni chama Cha matukio,hakina watu au viongozi wenye uwezo wa kujenga hoja zenye kuvuta hisia za watu,kila mmoja anapuyanga kivyake,Hakuna Sera za pamoja Wala ajenda za pamoja Wala mikakati ya pamoja Wala muelekeo wa pamoja ,ndio maana mwingine anatumia muda wake wote kujitetea kuwa hajalamba asali ,huku mwingine akijitetea kuwa amepoteza mabillioni chamani kana kwamba Ni Saccos au kikoba ambacho wanaangalia nani mwenye Hisa nyingi,
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627
Baada ya kufunguliwa na kuruhusiwa kwa mikutano ya vyama vya siasa hapa nchini tulishuhudia mbwembwe na vitisho vya hapa na pale kutoka kwa viongozi na wanachama wa chadema kuwa Wana kwenda kutikisa na kuipa shida CCM.
lakini Cha ajabu Baada ya ufunguzi wa mikutano Yao kilichofuata ni kichekesho na fedheha kubwa Sana, maana badala ya kuwaunganisha wanachama wake wamebaki wamegawanyika na kuanza kutafutana Ni Nani mchawi na msaliti wa chama,Ni Nani Kamanda wa ukweli na Nani aliye ramba asali nyingi,Ni Nani Ni CCM B na Nani anatakiwa kumpisha fulani,Ni Nani amepanda kalewa jukwaani na Nani kazungumza masuala ya wananchi.
Tumeshuhudia Wana chadema wakilaumiana na kutiliana mashaka wao kwa wao,kwamba kwanini Mwenyekiti hajawashambulia Sana CCM ,kwanini amempongeza Mwenyekiti wa CCM,kwanini sauti yake ilikuwa hivi na vile, yaani Sasa chama kina mpasuko mkubwa huku wengi wakimsubili Lisu ili waje wasikie atatukana matusi mangapi,wao furaha Yao Ni kutaka kuona anayepanda jukwaani anaropoka matusi utafikiri kakatika mishipa ya fahamu na kuvuruga ubongo wake.
Kinachowachanganya Zaid Ni mapokeo ya watanzania kwa namna walivyo wapuuza na kuwadharau kwa Sasa,maana wanaona watanzania hawana habari nao,hawana habari na mikutano Yao,wanawakosoa na kuwapinga kila mahali,wanamtetea, kumsemea na kumpongeza Rais Samia kwa uchapa kazi wake uliotukuka na kuahidi kumuunga mkono katika kila hatua ya ujenzi wa Taifa letu.
Kwa Sasa Chadema Imepoteza ule mvuto na ushawishi iliokuwa nao kutokana na utendaji kazi wa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani kufanyia kazi kero na changamoto zote zinazogusa na kuwa kikwazo katika maisha yao,wameona chadema Ni watu wasio na misimamo na vigeu geu,wameona chadema Ni njaa tupu tu na mkusanyiko wa wasaka tonge,ndio sababu ya Kuendelea kuwa na Imani na CCM na serikali yake chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Mama Samia.
CHADEMA kimebaki Ni chama kisicho na dira Wala muelekeo,hakina ajenda Wala Sera kinayoisimamia yenye kuwashawishi watanzania kuwaunga mkono,Hakina watu Wala viongozi wenye ushawishi na wenye kuteka hisia za watanzania,Hawana kiongozi au viongozi wenye uwezo wa Kuiteka mioyo ya watanzania kuweza kuwaunga mkono katika harakati zao,Hakina ngome yoyote kutoka kundi lolote katika jamii yetu,
Ni chama Cha matukio,hakina watu au viongozi wenye uwezo wa kujenga hoja zenye kuvuta hisia za watu,kila mmoja anapuyanga kivyake,Hakuna Sera za pamoja Wala ajenda za pamoja Wala mikakati ya pamoja Wala muelekeo wa pamoja ,ndio maana mwingine anatumia muda wake wote kujitetea kuwa hajalamba asali ,huku mwingine akijitetea kuwa amepoteza mabillioni chamani kana kwamba Ni Saccos au kikoba ambacho wanaangalia nani mwenye Hisa nyingi,
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627