CHADEMA imeonyesha udhaifu kuongoza nchi, ijipange upya

Mleta mada anajaribu kujenga hoja kwamba mwanza ilitakiwa ipate Maendeleo makubwa kwa sababu imekuwa ikiongozwa Na Chadema lakini imeshindwa: Na hivyo ndivyo itakavyokuwa Chadema ikishika dola!

kwanza hoja yako umeijenga kwa misingi dhaifu.

pili, umeshindwa kuzingatia kwamba Chadema sasa hivi haina dola, haina uwezo Wa kukasimu, na hata budget ikishapitishwa Chadema haina uwezo wa kupeleka Pesa kwenye manispaa zikatumike. Pesa wanazopata manispaa zinatoka serikali kuu inayoongozwa Na CCM, wakiamua kuwakwamisha wanawakwamisha.

Pia ni vizuri ukaelewa hizi Pesa za matumizi kwenye wilaya zinasimamiwa Na wakurugezi ambao ni waajiriwa Wa serikali. hivyo mkurugenzi anaweza kuamua kukwamisha Maendeleo ya mji kwa manufaa ya bosi wake

katika mazingira haya, Mchango mkubwa wa Meya na Madiwani ni kuhakikisha Pesa iliyopatikana haitumiki vibaya. Ingawa kuna pesa inayopatikana kwa kodi za manispaa Pesa hii ni kidogo

Familia iliyokamilika na kuwa na mshikamano, umoja, ustahimilivu na mwono wa mbali huishi kwa mwendo huo hata wakati wa kipindi cha ukata katika maisha yao. Kilichosababisha jiji la Mwanza kurudi mikononi mwa CCM si ukata wa pesa za maendeleo ingawa inaweza kuwa ni moja ya sababu kati ya nyingi. Kubwa zaidi ninaloona mimi ni follow up.

Ingefaa mmojawapo wa viongozi wa juu Chadema, labda Mnyika ambaye ndiye msemaji angekuja hapa atujibu hili, imekuwaje Madiwani wa Chadema kuwa na kura turufu ya kumwondoa Meya wao wakati walikuwa na nafasi ya kumtahadharisha mambo kabla hayaja haribika au pengine kama maji yalizidi unga, basi wangeyapeleka ngazi ya juu kupata ufumbuzi zaidi kuliko kusubiri moto unaunguza nyumba na kuita zima moto.
 
Mkuu Candid Scope ninakuheshimu sana hapa jamvin lakini Leo sikubaliani na wewe kabisa. Mkuu wa mkoa ni chaguo la ccm sasa unategemea nini? Kodi inakusanywa na serikali ya ccm wakiaamua wanaweza wasipeleke hela nani mwenye uwezo wa kohoji au kudai kwa nguvu mkuu vikwazo vilikuwa ni vingi sana
 
Last edited by a moderator:
Kinga ni bora kuliko kuponya, kama tahadhari ingefanyika mapema sitegemei kama hatua ya kufukuza madiwani ingetokea. Huenda madiwani wale walikata tamaa baada ya kuona uvumilivu umeshindikana.

inavyoonekana wewe umeweka uzi huu kwa lengo la kusulubu tu. Wachangiaji wengi wanakubaliana na hoja zako na kupongeza kuwa inafaa zifanyiwe kazi. Tumeenda mbali zaidi kwa kufafanua baadhi ya maamuzi magumu dhidi ya waliohusika. Uamuzi ambao ni nadra kwa utamaduni ya viongozi wetu ya Tanzania ya leo. Sasa sijui unataka watu waseme nini cha zaidi. Wapinge au waseme tu amina kwa kila kitu bila hata ya kutoa mitizamo yao?
 
Mkuu Candid Scope ninakuheshimu sana hapa jamvin lakini Leo sikubaliani na wewe kabisa. Mkuu wa mkoa ni chaguo la ccm sasa unategemea nini? Kodi inakusanywa na serikali ya ccm wakiaamua wanaweza wasipeleke hela nani mwenye uwezo wa kohoji au kudai kwa nguvu mkuu vikwazo vilikuwa ni vingi sana

Nimekuelewa na hilo nalifahamu, lakini jambo ambalo halijaingia akilini mwangu Uongozi wa Chadema kitaifa ulikuwa wapi hadi kufikia baadhi ya madiwani wake kusalitiana? Ina maana kuna mambo katika chamber yao hayakuwa yanaenda sawa na hivyo kufikia baadhi kukata tamaa. Tunaweza kuongea mangi kwama wamenunuliwa au vinginevyo, lakini matatizo pale jiji la Mwanza yalianza kusikika muda mrefu mtifuani ndani ya madiwani na wabunge Chadema. Je, ngazi za juu walichukua tahadhari au hatua gani kunusuru?

Je, mshikamano kati ya madiwani wa CCM na viongozi wa wilaya na mkoa Mwanza wenyewe kwa wenyewe vina uhusiano gani na madiwani wa Chadema kuwa na turufu ya kura kumwondoa kitini meya wao? Mkuu wa Mkoa hakuwa na kura turufu hiyo. Kama tatizo lilikuwa ni serikali ya CCM kutopeleka pesa za maendeleo jijini Mwanza, mimi sioni kama ndilo tatizo la kuondolewa meya wao na wao wenyewe, kwani walikuwa na nafasi ya kuwatumia madiwani na wabunge wao kuishtaki serikali bungeni itekeleze ilani yake ya maendeleo jijini Mwanza.
 
siyo mwanza tu. Kule moshi wameishia kuiba pesa za walipakodi na kuandaa safari za kisanii eti kwenda kujifunza kufanya usafi Rwanda. Kuna mafagio gani huko ambayo hapa VETA hawawezi kuyafundisha? Wanasahau kuwa Kigali walikuja kujifunza moshi?? Haya angalia majimbo yaliyosikiliwa na CHADEMA UBUNGO NA KAWE. HAKUNA KITU HATA KIMOJA KILICHOFANYIKA MATOKEO YAKE MNYIKA AMEISHIA KUDANDIA KAZI ZINAZOFANYWA NA MAGUFULI NA MIRADI YA MAJI YA SERIKALI. ALIYOA AHADI YA KUJENGA SEKONDARI KILA KATA PALE UBUNGO. TUMAMSUBIRI KWENYE KAMPENI KAMA ATAKUWA BADO YUKO HAI
 
inavyoonekana wewe umeweka uzi huu kwa lengo la kusulubu tu. Wachangiaji wengi wanakubaliana na hoja zako na kupongeza kuwa inafaa zifanyiwe kazi. Tumeenda mbali zaidi kwa kufafanua baadhi ya maamuzi magumu dhidi ya waliohusika. Uamuzi ambao ni nadra kwa utamaduni ya viongozi wetu ya Tanzania ya leo. Sasa sijui unataka watu waseme nini cha zaidi. Wapinge au waseme tu amina kwa kila kitu bila hata ya kutoa mitizamo yao?

NO EXCUSE, mbavu zangu. Ningeshauri watanzania kujenga misingi ya uchumbuzi wa mambo yatokeayo katika maisha yetu iwe siasa, uchumi na megineyo bila woga au kufunikafunika kwa misingi ya kile moyo ukipenda. Mfumo tuliozoea wa kile moyo ukipenda kufumbia macho ndicho kinachotupeleka pabaya.

Kama timu ya mpira ikishindwa inatakiwa kujadili na kutafakari wapi makosa waliyafanya kama ni kosa la safu ya ushambulia? Safu ya kiungo? Safu ya Ulinzi? Kosa la mfumo tuliotumi? Mazoezi? Nk. Maana yake tunatakiwa kujipanga upya kosa kama hilo lisitokee, lakini kunyamazia tu maana yake ni kufunikafunika makosa ambayo tusipokuwa makini yatajirudia.

Tatizo lililojitokeza Mwanza kwa uadilifu na uongozi bora ulitukuka utelezi ule viongozi kitaifa wanaujua sana. Binafsi nisingekubaliana na ile fukuza fukuza, labda onyo maana adhabu kwa mtoto kila mara si kumfukuza ndani ya nyumba vinginevyo amekuwa hatari ya usalama ndio utamkabidhi kwa vyombo vya kumsahihisha ili arudie tabia inayoridhisha.

Sina maana ya kufuga ndumila kuwili, sina maana ya kutetea uovu, lakini uvumilivu tunaishana, kwani wengine wana upeo wa juu na wengine wa kiwango na wanaobaki ni wa chini. Sishangai kama walifikia mahala baadhi kukata tamaa maana wengi waliochaguliwa udiwani na kisha kukabidhiwa kiti cha Umeya pengine hawakuwa na uzoefu katika kuongoza, walihitaji kusaidiwa na wenye uzoefu kuwa karibu kuwapa mbinu. Kama wanye kuwapa nguvu na mbinu walikuwa juu zaidi hawafikikiwi nini tungetegemea kama si baadhi kuanza kuishiwa nguvu na kuamua kugawa turufu ya kura kumwondoa Meya?



 
Ukweli huuma, hakuna sababu ya kufunikafunika ukweli kwani mficha ukweli huumbuka hadharani. Wenye moyo wa uzalendo wa kweli kwa nchi yetu tutaungana kuijenga Chadema kwa kusifia wanapofanikiwa na kuwashutumu wanapoleteza
Mkuu Candid Scope, Mwarobaini ni mchungu lakini hutibu. Mkuu umemaliza, wakifanya vizuri tuwapongeze na vile vile wakifanya vibaya tuwaambie. Binafsi sikufurahishwa na kitendo cha CDM kupoteza nafasi ya Ummeya tena kwa muda mfupi.

Wachangiaji wengi wanasema ni mbinu ya CCM kuiharibia CDM, hiyo ni sawa ila kilichotakiwa ni CDM kutegua hiyo mbinu ili waweze kufanya vizuri. Pande zinazopingana siku zote lazima zije na mbinu tofauti tofauti ili ziweze kushindana (Kumshinda mpinzani wako).

Hivyo ni vizuri CDM wajipange upya kuhakikisha kitu kama hiki hakitokei tena popote pale wanapoongoza. Viinginevyo huu udhaifu utatumika kukimaliza CDM. Thanx Candid.

 
siyo mwanza tu. Kule moshi wameishia kuiba pesa za walipakodi na kuandaa safari za kisanii eti kwenda kujifunza kufanya usafi Rwanda. Kuna mafagio gani huko ambayo hapa VETA hawawezi kuyafundisha? Wanasahau kuwa Kigali walikuja kujifunza moshi?? Haya angalia majimbo yaliyosikiliwa na CHADEMA UBUNGO NA KAWE. HAKUNA KITU HATA KIMOJA KILICHOFANYIKA MATOKEO YAKE MNYIKA AMEISHIA KUDANDIA KAZI ZINAZOFANYWA NA MAGUFULI NA MIRADI YA MAJI YA SERIKALI. ALIYOA AHADI YA KUJENGA SEKONDARI KILA KATA PALE UBUNGO. TUMAMSUBIRI KWENYE KAMPENI KAMA ATAKUWA BADO YUKO HAI


Asante, naona umeenda kusiko, maana unayojadili ni mambo yanayohusu utendaji unaotegemea kupata mshio toka Hazina ambako chungu chake ambacho sisi walipokodi hutumbukiza pesa kimeshikiliwa na serikali ya CCM. Hakuna shaka serikali ya CCM ina uwezo wa kudhoofisha maendeleo ya majimbo yanayoshikiliwa na upinzani kwa sababu za wazi za ushindani wa kisiasa pasipo kuangalia maana ya maendeleo kwa taifa. Akina Mnyika, Mdee na wengineo hawana uhuru wa kwenda kuteka maji ndani ya chungu cha hazina isipokuwa serikali ya CCM iridhie maji yachotwe.

Mada yangu imeegemea zaidi katika kasoro za ufuatiliaji wa viongozi wa ngazi za juu kuhusu uadilifu na utendaji wa halmashauri zinazoshikiliwa nao na hivyo pengine kusababisha hata kusalitiana wenyewe kwa wenyewe.
 
mfumo wa nchi hauruhusu vyama ku thrive hilo ni wazi. Ili tuwe na demokrasia ya kweli tuwe wavumilivu

Nakubaliana na wewe. Upinzani hauwezi kuleta mabadiliko ndani ya serikali ya chama tawala. Serikali itahakikisha maendeleo hayapatikani kwenye majimbo yaliyoshikwa na upinzani. Angalia jimbo la ubungo wananchi wanalalamika hakuna maendeleo. Itabidi kazi kubwa ifanyike kuuelimisha umma juu ya kuleta mabadiliko ya kweli.
 
Jamaa kaandika vitu vya msingi sana. Tatizo naliona wana CDM its like hawataki kuambiwa upungufu,but kwakweli kuanguka kwa utawala wa CDM Mwanza ni kasoro kubwa sana kwa ngazi ya mkoa na taifa pale kinondoni
 
Mkuu Candid Scope ninakuheshimu sana hapa jamvin lakini Leo sikubaliani na wewe kabisa. Mkuu wa mkoa ni chaguo la ccm sasa unategemea nini? Kodi inakusanywa na serikali ya ccm wakiaamua wanaweza wasipeleke hela nani mwenye uwezo wa kohoji au kudai kwa nguvu mkuu vikwazo vilikuwa ni vingi sana

Mkuu vikwazo vipo tena vingi tu, tunachojaribu kujiuliza ni kwamba "Uwajibikaji wa pamoja ulikosekana???". Mbinu zote zilizotumika mpaka Meya kudondoshwa inaonekana kuna sehemu pamepwaya vinginevyo isingetokea. CDM walitakiwa kuuona huu mkakati na kutengeneza mkakati mbadala. Hili halikufanyika kwa sababu hakukuwa na follow up ya kutosha.
 
Kwani maendeleo yanatatuliwa na mbunge,meya au diwani wakuu?au mtoa mada haelewi?ata hivyo meya ni bosi wa halmashauri lakin juu yake mabosi na mafungu ya pesa za vipaumbele vinatoka wap?na halmashauri zinaundwa na wajumbe wangapi wa chama tawala na jambo la msingi katika kuangalia utendaji wa meya kutoka chadema. At the end of the day tunataka watu watendaji na wenye nguvu ya ushawishi kuelekea maendeleo, na sio kumtaja aliefeli ametoka chama gan, we chama kinakusaidia nn?au umetumwa?watanzania hatutak hoja za finyu ka hz ambazo waz zina itikad ndan yake..
 
JF naomba mfuatilie kuna watu wanafuta mawazo yetu kwenye hii forum. Ni vizuri watu wawetayari kusikis yale wasiyopenda kuyasikia. Hiyo ndiyo DEMOKRASIA. Demokrasia siyo tu jina la chama bali ni utaratibu wa kuheshimu mawazo tofauti. Hapa kazi tunayo huwezi kutunyamazisha kwa kufuta maoni yetu maana tutahakikisha yanafika kila kona hata kwa kuytaundika juu ya miti
 
Watanzania pale ambapo chadema inakosea ni vizuri kuikosoa ili kujenga chama imara,ndio hatuwezi kuringanisha ccm na chadema ila tuwe wise kukosoa pale panapotakiwa kukosolewa.ndio hatuwezi kuipa ccm madaraka lakini ni lazima tuikosowe chadema kwa nguvu kwasababu kwa sasa hatuna kimbilio
 
Candid scope umeongea vema, ila critics laazima wawepo, can we be looking insideout sometimes! jambo jema saana umeongea
 
Familia iliyokamilika na kuwa na mshikamano, umoja, ustahimilivu na mwono wa mbali huishi kwa mwendo huo hata wakati wa kipindi cha ukata katika maisha yao. Kilichosababisha jiji la Mwanza kurudi mikononi mwa CCM si ukata wa pesa za maendeleo ingawa inaweza kuwa ni moja ya sababu kati ya nyingi. Kubwa zaidi ninaloona mimi ni follow up.

Ingefaa mmojawapo wa viongozi wa juu Chadema, labda Mnyika ambaye ndiye msemaji angekuja hapa atujibu hili, imekuwaje Madiwani wa Chadema kuwa na kura turufu ya kumwondoa Meya wao wakati walikuwa na nafasi ya kumtahadharisha mambo kabla hayaja haribika au pengine kama maji yalizidi unga, basi wangeyapeleka ngazi ya juu kupata ufumbuzi zaidi kuliko kusubiri moto unaunguza nyumba na kuita zima moto.

kwa hili Mkuu Candid Scope, kilichosababisha jiji la mwanza kurudi CCM si udhaifu wa Chadema bali ni Mbinu chafu za CCM na usaliti wa wale Madiwani wawili wa Chadema. kuwa kiongozi Chadema ukaendelea kuwa na msimamo siku zote na kushinda nguvu ya fedha za kifisadi sio kitu rahisi!
Mbinu waliyotumia CCM ni kutumia wana CDM kumkataa meya, CCM wakahamishia Madiwani wao 2 kwenye jimbo. Na vile vile ukumbuke wakawa wamegawanya jimbo kupata Nyamagana na Ilemela!
Hebu we jiulize jimbo linagawanywa baada ya uchaguzi na uhamisho wa Madiwani! Na madudu mengine kibao ambayo ni kinyume cha sheria Na taratibu. Halafu Leo unakaa unalaumu Chadema!
Chadema kuwafukuza Madiwani wasaliti ni sawa, bora kukosa umeya ambao hata hivyo kwa sababu nilizoeleza kwenye post yangu hapo juu haukuwa na maslahi makubwa kwa wananchi.
najua hata akija Mnyika ataeleza haya tena na mengine zaidi
 
Mkuu Candid Scope ninakuheshimu sana hapa jamvin lakini Leo sikubaliani na wewe kabisa. Mkuu wa mkoa ni chaguo la ccm sasa unategemea nini? Kodi inakusanywa na serikali ya ccm wakiaamua wanaweza wasipeleke hela nani mwenye uwezo wa kohoji au kudai kwa nguvu mkuu vikwazo vilikuwa ni vingi sana

huna hoja ila unajua sana kulaumu.kuongoza halmashauri manake ni kukusanya mapato.danganya wajinga.jiji limewashinda mnaanza kusingizia ccm.kazi hamuwezi nyie kaeni pembeni.
 
Last edited by a moderator:
kwa hili Mkuu Candid Scope, kilichosababisha jiji la mwanza kurudi CCM si udhaifu wa Chadema bali ni Mbinu chafu za CCM na usaliti wa wale Madiwani wawili wa Chadema. kuwa kiongozi Chadema ukaendelea kuwa na msimamo siku zote na kushinda nguvu ya fedha za kifisadi sio kitu rahisi!
Mbinu waliyotumia CCM ni kutumia wana CDM kumkataa meya, CCM wakahamishia Madiwani wao 2 kwenye jimbo. Na vile vile ukumbuke wakawa wamegawanya jimbo kupata Nyamagana na Ilemela!
Hebu we jiulize jimbo linagawanywa baada ya uchaguzi na uhamisho wa Madiwani! Na madudu mengine kibao ambayo ni kinyume cha sheria Na taratibu. Halafu Leo unakaa unalaumu Chadema!
Chadema kuwafukuza Madiwani wasaliti ni sawa, bora kukosa umeya ambao hata hivyo kwa sababu nilizoeleza kwenye post yangu hapo juu haukuwa na maslahi makubwa kwa wananchi.
najua hata akija Mnyika ataeleza haya tena na mengine zaidi

Siko kinyume sana na mchango wa maoni yako. Wengi wetu tunajua dhahiri mbinu iliyotumika kwa vile siasa za siku hizi ni ni za kisayansi zaidi. Wote tuko katika ulimwengu huu wa mwendo na miondoko ya kisayansi na wote wanatumia kiungo kile kile katika kufikiri na kubuni mbinu hizi.

Je, ndau unakubali kwamba viongozi wa Chadema kitaifa walilitelekeza jiji la Mwanza? Maana hatujasikia hatua za awali za maonyo kwa madiwani waliwafukuza, imekuja ghafla tu mambo yalipoharibika. So, kuna kitu kinakosekana hapa ambacho ni follow up toka juu ilikosekana.

Mimi ni mpenda mabadiliko lakini siko tayari kufunikafunika mambo ambayo hayaendi sawa, ni mpenda utanda wazi.
 
Back
Top Bottom