CHADEMA imelitaka Jeshi la Polisi kutoa kauli juu ya watu 40 waliokamatwa kwenye maandamano

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika anazungumza na vyombo vya habari muda huu.


Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika John amelitaka Jeshi la Polisi kutoa kauli juu ya watu 40 waliokamatwa kwenye maandamano ya chama hicho February 16, 2018.

Mnyika amesema kama Polisi wakishindwa kuwapa dhamana na kuwatolea ufafanuzi ifikapo kesho basi wapelekwe Mahakamani.

Mnyika amesema Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, kina taarifa za baadhi ya watu wanadhamiria kuwabambikizia kesi ya mauaji dhidi ya mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji, Akwilina Akwilina, pamoja na kesi ya kufanya maandamano bila ya kuwa na kibali cha jeshi la polisi.

Tunataka Kauli kutoka Serikalini kuhusiana na watu wetu kukamatwa na kushindwa kupelekwa Mahakamani je! Polisi wamepewa agizo na Serikali au laaa? na kama hawatatoa Kauli yoyote basi tutaifungulia mashtaka Serikali kwa kukiuka Sheria. Kaimu Katibu Mkuu Bara CHADEMA , John Mnyika.
 
Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika anazungumza na vyombo vya habari muda huu.


========
Timu ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya utangazaji tutaletea live yanayojiri

Tuko mubashara tunasubiri chochote kutoka akili kubwa.
 
Wajitahidi Sana wawe wanakuja na Solutions na Si kulialia.Ukilia Utawala huu,Ni sawa na Machozi ya Samaki.Nimependa Alichosema Mayor Jacob.Something Must be Done
Kwenda huko, wewe unataka solution ipi. Unafikiri ni rahisi kiasi hicho? Badala ya kuwapongeza kwa jitihada zao katika mazingira haya magumu kabisa unakuja na mbwembwe zako tu huku ukijiweka pembeni.
 
Kwenda huko, wewe unataka solution ipi. Unafikiri ni rahisi kiasi hicho? Badala ya kuwapongeza kwa jitihada zao katika mazingira haya magumu kabisa unakuja na mbwembwe zako tu huku ukijiweka pembeni.
It's very true

Kwa utawala huu wa mkono wa chuma wa serikali ya awamu ya 5 kuendelea kuwepo tu upinzani, bila kununuliwa na CCM hatuna budi kumpongeza
 
It's very true

Kwa utawala huu wa mkono wa chuma wa serikali ya awamu ya 5 kuendelea kuwepo tu upinzani, bila kununuliwa na CCM hatuna budi kumpongeza

Afadhali wewe umenielewa. Mimi nakerwa sana na watu ambao hukaa pembeni na kuanza kulaumu wapinzani eti wanalialia tu bila kuchukua hatua, sasa wanataka wafanyeje? Kwanza kazi waliyokwishaifanya ni kubwa sana wanahitaji support na kutiwa moyo.

Mazingira ya kisiasa kwa sasa ni magumu mno. Wao pia wana nyama, damu na ndugu wanaowategemea. Sasa kama wanaowatetea wenyewe wamekaa pembeni tu na kupepeta mdomo wao wafanyeje? Siku upinzani ukifa nchi hii ndipo utakapoona hata hao CCM wakijutia kwa kuwa kibano kitahamia kwao.
 
kkkkk !
wale maofisa usalama makada waliovamia ofisi za cuf na kushambulia..
waliovamiwa ndio walioshtakiwa
NAHISI KAMA NIMEPANDA GARI DEREVA ANA FRUSTRATION ..
yaani kavurugwa na pombe
yaani kasukumizwa..
kkkkk
 
Back
Top Bottom