Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Wahenga walishasema asiyekubali kushindwa si mshindani. Ila kukubali kushindwa hata kabla mtanange haujapigwa ni ishara mbaya sana.
Chadema kama chama kikuu cha upinzani sasa kinaonyesha dalili zote kuwa kimenyoosha mikono juu. Kama ni vitani sasa wameka silaha chini na wameshakuwa mateka.
Maana ili uweze kukichachafya chama kilichoshika dola lazima kifanye makosa ili upate hoja za kukishambulia na kukikosoa.
Lakini toka JPM aingie madarakani wapinzani wamekosa kabisa wapi wataikosoa serikali ya CCM, Maana huko nyuma ajenda ambayo walizoea kuikamata na kujipatia umaarufu ni ufisadi.
Nashangaa sana mpaka sasa wanashikilia kidedea hoja ya upotevu wa tril 1.5 na kutaka kujipatia umaarufu wakati PAC walitoa majibu bungeni kuwa kulifanyika maridhiano ya kimahesabu na hakuna ufisadi uliofanyika.
Nashangaa pia kuona wafuasi wa Chadema na wanachama wake wanapinga serikali kutekeleza miragi kama SGR, JNHPP, ujenzi wa miundo mbinu kama madaraja na barabara na wanajitoa akili kichwani kuwa hii miradi itakuwa na manufaa makubwa kwa taifa letu.
Lazima watambue kuwa ni kwa kuwa na kiongozi ambaye ana uzalendo wa hali ya juu ndio maana haya mambo yanafanyika. Maana kama mtu ana nia ya kufanya ufisadi alafu yupo ikulu nani atamzuia. Maana hata hiyo tri 6+ inayojenga JNHPP angeliamua kuihamishia Uswisi nani angelijua!
Chadema kama chama kikuu cha upinzani sasa kinaonyesha dalili zote kuwa kimenyoosha mikono juu. Kama ni vitani sasa wameka silaha chini na wameshakuwa mateka.
Maana ili uweze kukichachafya chama kilichoshika dola lazima kifanye makosa ili upate hoja za kukishambulia na kukikosoa.
Lakini toka JPM aingie madarakani wapinzani wamekosa kabisa wapi wataikosoa serikali ya CCM, Maana huko nyuma ajenda ambayo walizoea kuikamata na kujipatia umaarufu ni ufisadi.
Nashangaa sana mpaka sasa wanashikilia kidedea hoja ya upotevu wa tril 1.5 na kutaka kujipatia umaarufu wakati PAC walitoa majibu bungeni kuwa kulifanyika maridhiano ya kimahesabu na hakuna ufisadi uliofanyika.
Nashangaa pia kuona wafuasi wa Chadema na wanachama wake wanapinga serikali kutekeleza miragi kama SGR, JNHPP, ujenzi wa miundo mbinu kama madaraja na barabara na wanajitoa akili kichwani kuwa hii miradi itakuwa na manufaa makubwa kwa taifa letu.
Lazima watambue kuwa ni kwa kuwa na kiongozi ambaye ana uzalendo wa hali ya juu ndio maana haya mambo yanafanyika. Maana kama mtu ana nia ya kufanya ufisadi alafu yupo ikulu nani atamzuia. Maana hata hiyo tri 6+ inayojenga JNHPP angeliamua kuihamishia Uswisi nani angelijua!