Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Wapo wanaoamini kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ndiyo chama mbadala cha kisiasa chenye uwezo wa kushika hatamu ya Uongozi kwa kuunda serikali. Wenye imani hii wanaamini kabisa kuwa CCM imeshindwa kabisa na hivyo ni lazima iondolewe madarakani ili chama kinginge "kipewe nafasi" ya kuliongoza Taifa letu kuelekea kule tunakotaka.
Tukilinganisha uwezo wa watu, rasilimali, historia na mwelekeo kati ya CCM na CHADEMA chama cha CCM kinaiacha CHADEMA kwa mbali sana. Linapokuja swali la mahusiano ndani ya vyama hivyo ni wazi kuwa vyama hivyo vyote havina tofauti sana katika kusababisha migogoro ya ndani, kutumia michakato ya ndani kushughulikia matatizo yao na vile vile kuendesha propaganda dhidi ya kingine.
Hata hivyo tunapoelekea katika Uchaguzi Mkuu ujayo na tukiamua kupima rekodi ya CHADEMA kwa miaka hii karibu 15 iliyopita tunalazimika kujiuliza kama kweli CHADEMA ndicho chama kinachoweza kweli kuliongoza Taifa letu. Na tukiiangalia historia hiyo kwa ukaribu wa miaka hii minne iliyopita tunalazimika kujiuliza kama CHADEMA kimefanya mambo yoyote, kuonesha uongozi katika jambo lolote au kwa namna yoyote ile kuamsha Watanzania katika kujiletea mabadiliko kiasi cha kuweza kustahili mapenzi, imani, na ufuasi wa watu wengi sasa hivi.
Je, yawezekana watu wanaokimbilia CHADEMA sasa hivi au wanaoiamini CHADEMA wanafanya hivyo si kwa sababu ya mapenzi yao kwa CHADEMA ilivyo bali kutokana na chuki yao kwa CCM na utawala wake wa mfumo wa kifisadi kwa miaka 45 iliyopita?
Je, yawezekana katika kutoridhika huku watu wamefumbia mapungufu makubwa ya kimuundo, kiitikadi, kichama na kimwelekeo ya CHADEMA ambayo yanaweza kujitokeza kwa nguvu kubwa endapo chama hicho kitashika madaraka ya nchi na hivyo kuturudisha kwenye "madudu" yale yale ya CCM?
Je, yawezekana kwa kuweka imani pofu (blind faith) kwa kundi la watu ambao wamejithibitisha mara kadhaa kuwa hawajamudu fani na sanaa ya siasa na kuwa ni jopo la watu wenye mtazamo wa kisomi zaidi (elitist) kuliko wa kimwamko wa mabadiliko wanajiandaa kwa kukatishwa tamaa?
Je, yawezekana ndio sababu bado wasomi wengi na watu wengi katika taifa letu bado wanaikumbatia CCM na kuikubali kwa sababu tayari wanajua madudu yake (zimwi likujualo) na hawako tayari bado kuweka imani yao kwa chama hiki au kingine chochote cha upinzani?
Je, yawezekana uongozi wa CHADEMA ulivyo sasa hasa mvutano wa kipuuzi kati ya Freeman Mbowe na Zitto Kabwe ni kikwazo kikubwa zaidi kwa kumuamsha jitu huyu aliyelala (this sleeping giant) kiasi kwamba hawa wawili peke yao kinyume na inavyochukuliwa ndio kikwazo kikubwa zaidi kwa CHADEMA kupiga ile hatua ya lazima mbele? Je, itakuwa bora kama hawa wawili wakaachilia nafasi za juu za uongozi wa Chama ili kukipa chama ule msukumo unahojitajika?
Katika kutafuta majawabu ya maswali haya siyo vyema kwa kweli kuendelea kuikumbatia CCM na madudu yake na kujaribu kuiokoa kwani ndio njia ya haraka ya kuleta mabadiliko ya haraka kuliko kukumbatia upinzani ulivyo sasa?
Tukilinganisha uwezo wa watu, rasilimali, historia na mwelekeo kati ya CCM na CHADEMA chama cha CCM kinaiacha CHADEMA kwa mbali sana. Linapokuja swali la mahusiano ndani ya vyama hivyo ni wazi kuwa vyama hivyo vyote havina tofauti sana katika kusababisha migogoro ya ndani, kutumia michakato ya ndani kushughulikia matatizo yao na vile vile kuendesha propaganda dhidi ya kingine.
Hata hivyo tunapoelekea katika Uchaguzi Mkuu ujayo na tukiamua kupima rekodi ya CHADEMA kwa miaka hii karibu 15 iliyopita tunalazimika kujiuliza kama kweli CHADEMA ndicho chama kinachoweza kweli kuliongoza Taifa letu. Na tukiiangalia historia hiyo kwa ukaribu wa miaka hii minne iliyopita tunalazimika kujiuliza kama CHADEMA kimefanya mambo yoyote, kuonesha uongozi katika jambo lolote au kwa namna yoyote ile kuamsha Watanzania katika kujiletea mabadiliko kiasi cha kuweza kustahili mapenzi, imani, na ufuasi wa watu wengi sasa hivi.
Je, yawezekana watu wanaokimbilia CHADEMA sasa hivi au wanaoiamini CHADEMA wanafanya hivyo si kwa sababu ya mapenzi yao kwa CHADEMA ilivyo bali kutokana na chuki yao kwa CCM na utawala wake wa mfumo wa kifisadi kwa miaka 45 iliyopita?
Je, yawezekana katika kutoridhika huku watu wamefumbia mapungufu makubwa ya kimuundo, kiitikadi, kichama na kimwelekeo ya CHADEMA ambayo yanaweza kujitokeza kwa nguvu kubwa endapo chama hicho kitashika madaraka ya nchi na hivyo kuturudisha kwenye "madudu" yale yale ya CCM?
Je, yawezekana kwa kuweka imani pofu (blind faith) kwa kundi la watu ambao wamejithibitisha mara kadhaa kuwa hawajamudu fani na sanaa ya siasa na kuwa ni jopo la watu wenye mtazamo wa kisomi zaidi (elitist) kuliko wa kimwamko wa mabadiliko wanajiandaa kwa kukatishwa tamaa?
Je, yawezekana ndio sababu bado wasomi wengi na watu wengi katika taifa letu bado wanaikumbatia CCM na kuikubali kwa sababu tayari wanajua madudu yake (zimwi likujualo) na hawako tayari bado kuweka imani yao kwa chama hiki au kingine chochote cha upinzani?
Je, yawezekana uongozi wa CHADEMA ulivyo sasa hasa mvutano wa kipuuzi kati ya Freeman Mbowe na Zitto Kabwe ni kikwazo kikubwa zaidi kwa kumuamsha jitu huyu aliyelala (this sleeping giant) kiasi kwamba hawa wawili peke yao kinyume na inavyochukuliwa ndio kikwazo kikubwa zaidi kwa CHADEMA kupiga ile hatua ya lazima mbele? Je, itakuwa bora kama hawa wawili wakaachilia nafasi za juu za uongozi wa Chama ili kukipa chama ule msukumo unahojitajika?
Katika kutafuta majawabu ya maswali haya siyo vyema kwa kweli kuendelea kuikumbatia CCM na madudu yake na kujaribu kuiokoa kwani ndio njia ya haraka ya kuleta mabadiliko ya haraka kuliko kukumbatia upinzani ulivyo sasa?