Vawulence
JF-Expert Member
- Jan 4, 2009
- 1,928
- 2,101
Katika mchezo wa karata,mtu anapata ushindi kutokana na atakavyomfanyia timing mpinzani wake. Kadiri unavyokuwa na mahesabu mazuri ndivyo unavyomuweka mpinzani wako kwenye wakati mgumu na huenda ukamfilisi kabisa.
Katika uchunguzi nilioufanya jana jioni na leo,nimegundua kuwa kitendo cha kumuacha mwenyekiti wa ccm akihutubia viti,wabunge wa CHADEMA wamejizolea umaarufu zaidi. Stori kubwa mtaani ni kuwa kama walichofanya ni makosa mbona hakuna sehemu yoyote ya katiba inayosema ni kosa kunyanyuka rais anapohutubia? Wengine wameenda mbali zaidi na kusema kuwa kama italazimu kuwaadhibu ni lazima katiba ibadilishwe kwanza jambo wanalolitaka.
Pia wananchi wengi wamekiri kuwa wabunge wa CHADEMA ni majasiri sana kwani wanajua namna ya kupata haki yao kwa njia mbadala.
Wakizungumzia kuhusu zomea ya wale wa ccm,baadhi ya waliohojiwa wamesema si mara ya kwanza kwa wabunge wa ccm kufanya kosa hilo kwani walishamzomea Kabwe lakini mwisho Kabwe akaonekana shujaa.
Kwa sasa wananchi wengi wako karibu na vyombo vya habari wakisubiri kwa hamu nini kitawapata wabunge wa CHADEMA.
Katika uchunguzi nilioufanya jana jioni na leo,nimegundua kuwa kitendo cha kumuacha mwenyekiti wa ccm akihutubia viti,wabunge wa CHADEMA wamejizolea umaarufu zaidi. Stori kubwa mtaani ni kuwa kama walichofanya ni makosa mbona hakuna sehemu yoyote ya katiba inayosema ni kosa kunyanyuka rais anapohutubia? Wengine wameenda mbali zaidi na kusema kuwa kama italazimu kuwaadhibu ni lazima katiba ibadilishwe kwanza jambo wanalolitaka.
Pia wananchi wengi wamekiri kuwa wabunge wa CHADEMA ni majasiri sana kwani wanajua namna ya kupata haki yao kwa njia mbadala.
Wakizungumzia kuhusu zomea ya wale wa ccm,baadhi ya waliohojiwa wamesema si mara ya kwanza kwa wabunge wa ccm kufanya kosa hilo kwani walishamzomea Kabwe lakini mwisho Kabwe akaonekana shujaa.
Kwa sasa wananchi wengi wako karibu na vyombo vya habari wakisubiri kwa hamu nini kitawapata wabunge wa CHADEMA.